Skip to main content

Posts

Showing posts from July, 2017

Okwi ananuka fedha

Okwi ananuka fedha  Mshambuliaji wa Simba, Emmanuel Okwi. KUANZIA leo Jumatano, zitakuwa zimebaki takribani siku 11 kabla ya usajili wa dirisha kubwa Tanzania Bara halijafungwa ambapo timu kadhaa zimekuwa zikiimarisha vikosi vyao. Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limetoa siku 52 kwa timu za Ligi Kuu Bara, Ligi Daraja la Kwanza na Ligi Daraja la Pili kujenga vikosi vyao kwa kufanya usajili kuanzia Juni 15 mpaka Agosti 6, mwaka huu. Tangu kufunguliwa kwa dirisha hilo, kumekuwa na vurugu kwa wachezaji kuhama timu moja kwenda nyingine huku tukishuhudia baadhi ya timu zikigombania mchezaji mmoja na kila upande ikihitaji saini yake. Katika vurugu hizo, kuna wachezaji wamesajili kwa madau makubwa na kuwafanya kuwa wachezaji ghali katika soka la Bongo kwa sasa. Championi ambalo tangu siku ya kwanza ya usajili limekuwa makini kufuatilia mchakato huo, linakuletea tathmini ya kile kilichofanyika mpaka sasa na kubainisha nani amesajili kwa mkwanja mrefu. EMMANUEL OKWI Mganda huy

Wanawake watano wafariki kwa kuchomwa moto

Wanawake watano wafariki kwa kuchomwa moto WANAWAKE watano wameuawa kwa kuchomwa moto Kijiji cha Undomo, Uchama, Nzega mkoani Tabora kwa tuhuma za kuhusika na imani za kishirikina. Kufuatia tukio hilo, Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri ameziagiza kamati za ulinzi za mkoa na wilaya kusitisha mara moja kazi zote za sungusungu kwa madai kwamba sungusungu hao wanahusika na mauaji hayo na kuvitaka vyombo vya usalama kuhakikisha vinawakamata na kuwafikisha mbele ya sheria watu wote wanaohusika. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Wilbroad Mutafungwa amethibitisha kutokea kwa tukio hilo huku akiwataja waliouawa kuwa ni Ester Kaswahili, Njungu Maswari, Christina Said, Kabula Kagito. Kamanda Mutafungwa ameeleza kwamba wamewakamata viongozi wa eneo tukio hilo lilipotokea, akiwemo diwani, Ofisa mtendaji wa kata na Ofisa mtendaji wa kijiji kwa madai kwamba walikuwa wakifahamu kinachoendelea kwenye eneo lao lakini kwa makusudi, waliamua kutotoa taarifa kwa jeshi la polisi, jambo li

Aingia matatani baada ya kupulizia wenzake kemikali usoni

Aingia matatani baada ya kupulizia wenzake kemikali usoni MADALALI wanne wa madini ya Tanzanite (mawe), wanashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kuwaumiza macho kwa kemikali aina ya ‘pepper spray’ baada ya kutofautiana malipo na madalali wenzao waliowauzia madini hayo. Habari kutoka polisi zilithibitisha jana kuwashikilia madalali hao, Schola Mwanga, Margareth Mushi, Sued Mwanga na Dorice Mushi, kwa tuhuma za kufanya kitendo hicho. Hata hivyo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Charles Mkumbo hakuweza kupatikana kutoa ufafanuzi zaidi. Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufani ya Mkoa ya Mount Meru, Dk. Jackline Urio, alithibitisha kupokea wagonjwa watano ambao alisema uchunguzi unaendelea kujua walimwagiwa aina gani ya kemikali. Alisema kutokana na hali zao, wagonjwa hao walitarajiwa kuhamishiwa Hospitali ya Rufani ya KCMC ya mkoani Kilimanjaro, jana. Alisema waliojeruhiwa walikuwa katika biashara ya madini na wakaletwa hapa wakilalamika macho yanauma, wakapewa huduma ya kwanza ya kuw

Mama, watoto wamwagiwa tindikali

Mama, watoto wamwagiwa tindikali KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA, MOHAMED MPINGA. VUMILIA Shengema (31) na watoto wake wawili wamemwagiwa tindikali wakati wakitokea dukani kwa kile kinachodaiwa ni wivu wa mapenzi. Kutokana na tukio hilo, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya, linamsaka mtuhumiwa huyo, Emmy Kyando (40, mkazi wa Sai jijini Mbeya ambaye aliwafanyia kitendo hicho cha kinyama watu hao. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Mohamed Mpinga, aliwataja wengine waliomwagiwa tindikali kuwa ni Loveness John (11), mwanafunzi wa darasa la sita katika Shule ya Msingi Sinde na  Nancy Peter (5), wakazi wa Mtaa wa Mwanshinga, Kata ya Manga jijini Mbeya. Walimwagiwa na kujeruhiwa na tindikali hiyo usoni, kifuani na mikononi Julai 19, mwaka huu saa tatu usiku. Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mpinga alisema Emmy anadaiwa  kufanya kitendo hicho kutokana na wivu wa kimapenzi kwa kuwa ni mke mwenza  wa mwathirika. Mpinga alifafanua kuwa baada ya mtuhumiwa kufanya kitendo hicho alik

Tegete afurahia kutua majimaji

Tegete afurahia kutua majimaji Jerry Tegete ameonyesha kufurahia kusajiliwa Majimaji ya Songea. Tegete amesema anaamini Majimaji inakuwa maisha yake mapya ya soka na anatamani kufanya vema. “Maisha ya soka haujui utaenda wapi, lakini ninataka kurudisha kiwango changu na kufanya vizuri zaidi nikiwa na Majimaji,” alisema. Tegete ameondoka Mwadui FC na kujiunga na Majimaji ambaye msimu uliopita ilifanya kazi ya ziada kujikomboa isiteremke daraja. Tegete alikuwa kinara katika ufungaji wakati akiichezea Yanga.

Neymar azima tambo za Manchester United

Neymar azima tambo za Manchester United  Baada ya tambo nyingi zilizoletwa na ushindi wa michezo yao yote ya kujiandaa na msimu wa ligi hatimaye usiku wa kuamkia leo ngebe za mashabiki wa Manchester United zilitulizwa. Manchester United walikuwa uwanjani katika mchezo wao wa mwisho barani America waliocheza dhidi ya wababe wa kutoka Hispania klabu ya Barcelona. Mchezo ambao ulijaza mashabiki wengi na huku watu wengi waliutazama kutokana na fomu ya sasa ya United na ubora ambao wakonao klabu ya Barcelona.  Alikuwa Neymar Dos Santos mchezaji anayezungumzwa sana kwa sasa na vyombo vya habari ndiye aliyeimaliza United katika dakika ya 31 ya mchezo. United kupitia kwa Lukaku na Rashford walijitahidi sana kulishambulia sana lango la Barcelona lakini umahiri wa golikipa Jasper Cillessen ulizizima jitihada za United. United sasa wanarudi barani Ulaya kwa michezo miwili ya kirafiki zidi ya Vilarenga nchini Norway na ule zidi Sampdoria kabla ya kukutana na Real Madrid katika fai

Lissu aachiwa kwa dhamana

Lissu aachiwa kwa dhamana Lissu akipelekwa mahakamani. MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imemwachia kwa dhamana Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema) na Rais wa Chama cha Wanasheria nchini, Tundu Lissu mapema leo asubuhi. Lissu ametakiwa kudhaminiwa na wadhamini wawili ambao kila mmoja ataweka bondi ya dhamana ya shilingi milioni 10 huku akiwekewa zuio la kutoka nje ya Mkoa wa Dar es Salaam bila kibali maalum cha mahakama. Aidha kesi yake imepangwa kusikilizwa Agosti 24 mwaka huu baada ya wadhamini wake kukamilisha taratibu zote za kumdhamini. Tundu  Lissu ambaye alikamatwa Alhamisi, Julai 20 mwaka huu, katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) wakati akijiandaa kuelekea Kigali, Rwanda kwenye kikao cha Chama cha Wanasheria cha Afrika Mashariki (EALS), alifikishwa Mahakamani hapo Jumatatu Julai 24 na kusomewa mashtaka  ya kutoa lugha ya uchochezi dhidi ya Serikali, kosa ambalo anadaiwa kulitenda Julai 17. Inadaiwa kuwa maneno hayo yalikuwa na lengo ya

Wauguzi kumnyima kura muhimu Kenyatta?

Wauguzi kumnyima kura muhimu Kenyatta? Nairobi, Kenya. Chama cha Wauguzi Kenya (NNAK) kimejiingiza katika siasa za uchaguzi baada ya kutoa tishio la “kuiaibisha” serikali ya Jubilee kwa madai ya kukawiza majadiliano kuhusu mzozo wa malipo yao. Wafanyakazi hao wa idara ya afya wanautazama uchaguzi uliopangwa Agosti 8 kama kete yao wakisema kurejeshwa tena mamlakani kwa Rais Uhuru Kenyatta kutakuwa hatarini ikiwa madai yao hayatatekelezwa kwa wakati. Mwenyekiti wa NNAK, Alfred Obengo alisema: “Tutakuwa na uchaguzi Agosti na sisi tuko 40,000 huku mshindi anatakiwa kupata asilimia 50 jumlisha moja. Idadi yetu haiwezi kupuuzwa.” Aliongeza: “Kwa hiyo wakati wewe (Rais Uhuru) unaendelea na kampeni, usifikiri hata wakati mmoja kwamba kura za wauguzi si muhimu.” Waguzi walipiga kambi katika viwanja vya Uhuru Park kulalamikia ukimya wa serikali katika mpango wa malipo ambao wanadai walifikia makubaliano na mwajiri wao. Walivamia ofisi za Tume ya Mishahara na Marupurupu (SRC) lakin

Waziri Mkuu akoleza moto sakata la vyuo vikuu 19 kufungiwa

Waziri Mkuu akoleza moto sakata la vyuo vikuu 19 kufungiwa Dar es Salaam. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amepigilia msumari sakata la vyuo vikuu 19 kuzuiwa udahili na kuvitaka kufanyia kazi kasoro zilizoainishwa na Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) badala ya kulumbana. Juzi, TCU ilivifungia vyuo 19 kudahili wanafunzi pamoja na kuzuia kozi 75 katika vyuo 22 nchini kutokana na kasoro mbalimbali. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Maonyesho ya siku tatu ya Vyuo Vikuu nchini, Majaliwa alivitaka vifuate utaratibu na si vinginevyo. Waziri Mkuu pia alitoa wito kwa TCU na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (Nacte), kuhakikisha kuwa programu zote zinazotolewa na vyuo vikuu na taasisi za elimu ya juu zinawawezesha wahitimu kupata ajira au kujiajiri na kuhimili ushindani kimataifa. Aliwataka waweke mikakati ya kuinua viwango vya taaluma ili kuwa na tija kwa maendeleo ya nchi na dunia kwa ujumla, huku akizitaka taasisi za elimu ya juu kuangalia tena mitalaa yake ili iende sambamba na du

Wanachama wa dhehebu haramu la Yesu wakamatwa China

Wanachama wa dhehebu haramu la Yesu wakamatwa China Baadhi ya wanachama wa kundi hilo ni maarufu kwa kumpiga mwanamke hadi kufa kwenye duka la McDonald mwaka 2014 Polisi nchini China wamewakamata wanachama 18 wa dhehebu lililopigwa marufukua. Baadhi ya wanachama wa kundi hilo ni maarufu kwa kumpiga mwanamke hadi kufa kwenye duka la McDonald mwaka 2014, baada ya mwanamke huyo kukataaa kuwapa namba yake ya simu. Dhehebu hilo linalofahamika kama Church of Almighty God lilianzishwa miaka ya 1990 na linadai kuwa Yesu alirudi duniani kama mwanamke nchini China Serikali ya China mara kwa mara huvamia madhehebu na kuwakamata wanachama wengi kwa miaka kadhaa. Wakati wa kuwakamata polisi pia walichukua kompiuta na vitabu vinavyotumiwa na dhehebu hilo. Imani ya dhehebu hilo ni kuwa Yesu alirudi duniani kama mwanamke. Mtu pekee anayedai kuwasiliana na mwanamke huyo ni mwalimu wa zamani Zhao Weishan, ambaye alilianzisha miaka 25 iliyopita na sasa ametorokea Marekani.

Zitto awajibu Chadema

Zitto awajibu Chadema Mbunge wa Kigoma Mjini ambaye pia ni Kiongozi Mkuu wa chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe amewajibu baadhi ya watu wanaomkosoa na kumuita msaliti kutokana na kitendo cha kumsifia Rais John Magufuli alipokuwa ziarani jimboni humo. Zitto alijibu mapigo hayo jana wakati akizungumza na wananchi wa Kigoma Mjini, ambapo alisema asingeweza kumkosoa Rais Magufuli wakati ule kwa kuwa alikuwa mgeni jimboni kwake, pia alikuwa anafanya shughuli za maendeleo ya wananchi wa jimboni kwake. “Rais alikuja hapa akafungua mradi wa maji tukaenda ziwa Tanganyika, kuna watu walikasirika sababu Rais alinisifia sana, hawezi akaja Kigoma mtu akanisema mimi vibaya msingekubali, na mgeni akija siwezi nikaanza kumsema vibaya, mgeni akija unamkaribisha anafanya kazi yake anaondoka, kwani rais akienda kwenye majimbo yao wanamsema, rais alikwenda Bukoba Mjini wakati wa tetemeko, mbunge wa jimbo hilo alimsema ? alikwenda Arumeru kwa mdogo wangu Joshua Nasari, alimsema rais kwa ni

Kontena 10 dawa kulevya zakamatwa

Kontena 10 dawa kulevya zakamatwa Kamishna Rogers Sianga Mamlaka ya kudhibiti na kupambana na dawa za kulevya nchini imekamata makontena 10 yaliyokuwa na kemikali aina ya ethanol yenye ujazo wa lita 200000 (Laki mbili) kupitia bandari ya Dar es salaam kutokea nchini Swaziland. Taarifa iliyotolewa na Kamishna Mkuu wa kupambana na dawa za kulevya nchini Rogers Sianga inasema kuwa kemikali ziliingizwa nchini na kampuni ya 'Hamid Ibrahim Saambaya' na kusema kwamba makontena hayo yamekamatwa kutokana na kampuni hiyo kutofuata miongozo na ya sheria zilizopo kutoka katika mamlaka husika za kujihusisha na kemikali bashirifu. Taarifa ya Sianga imedai kuwa kampuni hiyo imekuwa ikiingiza kemikali hizo nchini tangu mwaka 2016 na kufikia jumla ya ujazo wa lita milioni moja na nusu na kwamba kampuni hiyo haijawahi kusajiliwa wala kuweka kumbukumbu wapi kemikali hizo zinakopelekwa. "Pamoja na kwamba kemikali hizo zinatumika kwa matumizi mengine viwandani kama kutengene

Shilole afungukia mume atakae muoa

Shilole afungukia mume atakae muoa Zuwena Mohammed, ‘Shilole’. MSANII wa Bongo Fleva, Zuwena Mohammed, ‘Shilole’ amefunguka kuwa mwanaume atakayemuoa atawashangaza wengi kwani atakuwa ni wa tofauti na watu wanavyodhani. Akizun-gumza na Showbiz Xtra, Shilole alisema watu watashangaa kwa mwanaume atakayemuoa kwa sababu atakuwa ni mwanaume wa kawaida ila mwenye mapenzi ya dhati. “Wengi watamshangaa sana mwanaume atakayekuja kunioa, kwa sababu atakuwa ni wa kawaida tofauti na niliowahi ku-date nao. Kikubwa ni kupata penzi la dhati na heshima, maisha yanasonga,” alisema.

Idriss, Madee wapeana makavu

Idriss, Madee wapeana makavu  MSHINDI wa Big Brother Africa mwaka 2014, Idriss Sultan na msanii wa Bongo Fleva Madee Ally a.k.a ‘Shineida’ wamerushiana madongo kwenye mtandao ya kijamii wa Twitter. Idriss alianza kuuwasha moto kwa kuandika maneno yafuatayo kwenye ukurasa wake wa Twitter: “Ukiona msanii ana nyimbo mbaya jua moja tu, ana marafiki wanafiki balaa, yaani ni waongo ile mbaya.” Baada ya kuiona posti hiyo, ndipo Madee akavunja ukimya kwa kukomenti maneno ambayo mashabiki wameyatafsiri kama dongo kwa Idriss. “Na je ukiona kijana kapata hela nyingi na zikaisha ghafla na yeye ana marafiki wa aina gani?”

Umesikia alichokisema Shaffih Dauda Kuhusu Kukamatwa na TAKUKURU?

Umesikia alichokisema Shaffih Dauda Kuhusu Kukamatwa na TAKUKURU? Jumatano ya July 26 2017 zilienea taarifa za kukamatwa na TAKUKURU kwa mwenyekiti wa chama cha mpira Dar es Salaam DRFA Almas Kasongo, mgombea wa nafasi ya ujumbe wa kamati ya utendaji ya TFF kanda ya Dar es Salaam na mchambuzi wa habari za michezo Tanzania Shaffih Dauda pamoja na wanafamilia wengine wa mpira Mwanza. Taarifa zilizokuwa zimeripotiwa kukamatwa kwa watu hao zinadai ni viashiria vya rushwa na kuhusishwa na kampeni za chini kwa chini za uchaguzi Mkuu wa TFF, hivyo TAKUKURU ikawakamata kwa mahojiano yaliyodumu kwa saa kadhaa kabala ya kuwaachia kwa dhamana. Baada ya kurejea Dar es Salaam akitokea Mwanza Shaffih Dauda alipokuwa amekwenda na viongozi wa DRFA kwa ajili ya uzinduzi wa Ndondo Cup kupitia Clouds FM ameeleza tukio la kukamatwa kwao lilivyokuwa ambalo linadaiwa kulenga kuwachafua katika uchaguzi Mkuu wa TFF. “Nimehojiwa na TAKUKURU nikiwa Mwanza kwa ajili ya uzinduzi wa Ndondo Cup ambay

Coutinho aomba kwenda Barcelona

Coutinho aomba kwenda Barcelona Bado dirisha la usajili linaendelea kushika kasika kasi na taarifa za chini chini zinadai kiungo wa Liverpool Phellipe Coutinho amemuomba kocha wake Jurgen Klopp amruhusu kwenda Barcelona. Inafahamika kwamba Barca wanaihitaji sahihi ya Coutinho na wameshatuma ofa kwa Liverpool na wameshafanya mazungumzo na Coutinho ambaye yuko tayari kujiunga nao wakati wowote. Taarifa nyingine za usajili ni kwamba baada ya habari kuzagaa kwamba Mbappe anakwenda Real Madrid sasa Pep Gurdiola maeingia katika mapambano na anataka kutoa kitita kikubwa zaidi kwa Monaco ili kumnasa Mbappe. Kocha wa Chelsea Antonio Conte amesema kwa sasa Harry Kane ndiye striker anayemkubali sana nje ya Chelsea lakini hawezi kumnunua kwani ana uhakika bei yake kwa sasa itakuwa iko juu sana. Kiungo Jack Wilshaire hataki kuondoka nje ya jiji la London na anaona kama Arsenal wataamua kumuuza ni bora wamuuze humo humo London huku West Ham ikitajwa kama sehemu ambayo anaelekea Wilsha

Miaka miwili ya Lowassa nje ya CCM

Miaka miwili ya Lowassa nje ya CCM Dar es Salaam. Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa leo ametimiza miaka miwili tangu aweke historia ya kuwa kiongozi wa kwanza wa ngazi ya juu serikalini kuihama CCM na anasema hajutii uamuzi wake, yuko imara na licha ya kuzuiwa kufanya mikutano, kura zake zinazidi kuongezeka. Lowassa alichomoka CCM Julai 27, 2015 ikiwa ni siku chache baada ya Kamati Kuu ya CCM kuondoa jina lake na mengine katika kinyang’anyiro cha urais, uamuzi ambao ulizua mtafaruku mkubwa uliosababisha wajumbe wa Halmashauri Kuu kuimba wimbo wa kuonyesha kuwa na imani naye wakati mwenyekiti wa wakati huo, Jakaya Kikwete akiingia mkutanoni. Siku moja baada ya kujiengua CCM, Lowassa alitangaza kujiunga na Chadema, chama ambacho kilimpa fursa ya kuendeleza “Safari ya Matumaini” aliyoianzisha CCM, kwa kushirikiana na vyama vingine vitatu vilivyoundwa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa). Akihojiwa na Mwananchi jana kuhusu miaka yake miwili nje ya CCM, Lowassa alisema pam

VIDEO: Lissu achiwa Kwa Dhamana Asimulia Alivyoombwa kupimwa Mkojo

VIDEO: Lissu achiwa Kwa Dhamana Asimulia Alivyoombwa kupimwa Mkojo Mahakama ya hakimu Mkazi Kisutu imempa dhamana Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Tundu Lissu . Hakimu Mkazi Mkuu Wilbard Mashauri ametoa uamuzi huo leo baada ya  Kusikiliza hoja za pande zote mbili. Hata Hivyo Lissu ameesimulia alivyakataa kupimwa mkojo wake na Mkema Mkuu wa Serikali. Tazama hapa Full Video.