Skip to main content

Waziri Mkuu akoleza moto sakata la vyuo vikuu 19 kufungiwa

Waziri Mkuu akoleza moto sakata la vyuo vikuu 19 kufungiwa


Dar es Salaam. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amepigilia msumari sakata la vyuo vikuu 19 kuzuiwa udahili na kuvitaka kufanyia kazi kasoro zilizoainishwa na Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) badala ya kulumbana.

Juzi, TCU ilivifungia vyuo 19 kudahili wanafunzi pamoja na kuzuia kozi 75 katika vyuo 22 nchini kutokana na kasoro mbalimbali.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Maonyesho ya siku tatu ya Vyuo Vikuu nchini, Majaliwa alivitaka vifuate utaratibu na si vinginevyo.

Waziri Mkuu pia alitoa wito kwa TCU na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (Nacte), kuhakikisha kuwa programu zote zinazotolewa na vyuo vikuu na taasisi za elimu ya juu zinawawezesha wahitimu kupata ajira au kujiajiri na kuhimili ushindani kimataifa.

Aliwataka waweke mikakati ya kuinua viwango vya taaluma ili kuwa na tija kwa maendeleo ya nchi na dunia kwa ujumla, huku akizitaka taasisi za elimu ya juu kuangalia tena mitalaa yake ili iende sambamba na dunia ya kazi na ajenda za maendeleo ya Taifa.

“Waimarishe mfumo wa ithibati na ubora wa elimu na mafunzo ili kuhakikisha wanafunzi wanaohitimu shahada wanachangia maendeleo,” alisema Majaliwa.

Mbali ya Waziri Mkuu, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Profesa Simon Msanjila pia alivitaka vyuo vikuu vilivyoandikiwa barua na kupewa maelekezo ili kufanya marekebisho, kuyawasilisha TCU badala ya kutafuta njia ya mkato.

Aliwataka wenye vyuo kutatua changamoto zao na kuwaambia wasitarajie kwamba watatumia ofisi yoyote ya Serikali au kiongozi kuwasaidia.

Alisema wizara haitakivumilia chuo kikuu chochote kitakachotoa elimu yenye upungufu.

Profesa Msanjila alisema TCU itawachukulia hatua wanaoendelea kujitangaza licha ya kufungiwa kudahili, kwa sababu kufanya hivyo ni kuwadanganya wananchi.

Pia, alivitaka vyuo vikuu kufuata ada ya usajili iliyoelekezwa na Serikali ambayo haipaswi kuzidi Sh10,000.

Maoni ya wadau

Msimamo huo wa Serikali umeungwa mkono na baadhi ya wadau. Mkuu wa Chuo Kikuu cha Aga Khan (AKU), Profesa Joe Lugalla alisema hatua hiyo ni sahihi na inastahili kufanyiwa kazi.

Alisema waliliona hilo mapema ndiyo maana wapo makini katika udahili na kozi wanazotoa, ubora wa kozi hizo, na kuwa na walimu waliobobea katika taaluma mbalimbali.

Alisema wamejikita katika mambo mawili, afya na elimu, kwa sababu hakuna nchi itakayoendelea kama wananchi hawana afya na utaalamu wa kuelewa matatizo na kutafuta mbinu za kuyatatua.

Msemaji wa Chuo Kikuu cha Katoliki Mwenge cha Moshi, Athanas Sing’ambi alisema chuo hicho kimefungiwa kudahili kozi moja ya ‘Bachelor of Arts in Philosophy with Ethics’.

“Tumekubali kwa sababu kozi hiyo haikuwahi kuwa na wanafunzi,” alisema.

Hata hivyo, ofisa mmoja mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu John ambaye hakuwa tayari jina lake kutajwa gazetini alilalamikia uhakiki huo kwa ujumla.

Alisema walipewa barua wiki mbili zilizopita na wamejibu baada ya wiki moja, lakini wanashangaa kabla hawajapata majibu, jina la chuo chao limo katika orodha ya waliozuiliwa kudahili.

“Sipingi maboresho, bali kama wanataka sekta binafsi iwe imara, tungekaa pamoja wakatupa maelezo tukashirikiana nao kutatua changamoto zilizojitokeza kuliko kutukomoa hasa katika kipindi hiki cha udahili,” alisema.

TCU wamezitaja sababu za kuvifungia vyuo hivyo kuwa ni pamoja na kutokuwa na walimu, vifaa na kutokidhi vigezo kitaaluma.

Popular posts from this blog

Jinsi Wachawi Wanavyo Tumia Mafiga Mabichi Ya Mti Wa Mfausiku Kupika Uchawi Wa Kumvuta Kimapenzi Mtu Aliye Mbali.

Jinsi Wachawi Wanavyo Tumia Mafiga Mabichi Ya Mti Wa Mfausiku Kupika Uchawi Wa Kumvuta Kimapenzi Mtu Aliye Mbali. Na. DOKTA  MUNGWA  KABILI …0744 -000  473.  Wachawi  wanaweza  kutumia  uchawi  kumvuta  kimapenzi  mtu  aliye  mbali. Moja  kati  ya  vitu  vinavyo  tumika  katika  uchawi  huu  ni  pamoja  na  mafiga  mabichi  ya  mti  wa  mfausiku  ambayo  hukokwa  kwenye  majani  makavu ya  mgomba  ambayo  hutumika  kama  kuni  au  moto,  kipande  cha  sanda  alichovalishwa  maiti, herufi za  moto,  mti wa hina, pamoja na  vitu  vingine  lukuki. Kufahamu  kuhusu  uchawi wa aina  hii  na  jinsi  ya  kujikinga  nao, fuatilia  sehemu  ya  nne  ya  kitabu “ KITANDA  CHA  SOKWE  MTU” kama  ifuatavyo : SEHEMU  YA  PILI   YA  KITABU  “ KITANDA  CHA  SOKWE  MTU “ Wachawi   wakishindwa  kukutengenezea  kesi  kubwa  basi  waatakufunga  kwenye  kifungo  cha  mapenzi.  Katika  vifungo  vyote anavyo  fungwa  mwanadamu  hakuna  kifungo  kibaya  kama  kifungo  cha  mape

Faida nyingine za kula chungwa

Faida nyingine za kula chungwa Siku kadhaa zilizopita tuliangalia kwa uchache kuhusu faida za kula chungwa hivyo, pia siku ya leo naomba tuendelee kwa kuangalia faida nyingine za kula chungwa. 1. Ulaji wa machungwa husaidia kutibu mapafu. Chungwa pia lina kiasi kikubwa cha Vitamin B6 na Madini ya Chuma (iron), virubisho ambavyo ni muhimu kwa uzalishaji wa seli nyekundu za damu, ambazo hufanya kazi ya kusafirisha hewa ya oksjeni mwilini, hivyo kuwa muhimu kwa kujikinga na ugonjwa wa mapafu. 2. Husaidia kuimarisha mifupa ya meno. Chungwa lina kiasi kingi cha madini ya kalisi (calcium) ambayo ni muhimu kwa uimarishaji wa mifupa na meno. 3. Husaidia kupunguza kiwango cha mafuta mwilini. Virutubisho vilivyomo kwenye chungwa, hasa kwenye maganda yake, hupunguza kiwango cha mafuta mabaya mwilini (bad cholesterol). Hivyo kwa wenye tatizo la lehemu wanashauriwa kula machungwa pamoja na nyama zake. 4. Hupunguza kupatwa magonjwa wa figo. Ulaji wa machungwa mara kwa mara, ukusaid

Je, unajua Binadamu anatakiwa kulala masaa mangapi?

Je, unajua Binadamu anatakiwa kulala masaa mangapi? Unafikili ni wazo zuri kuamka  saa 11 za asubuhi na kufanya mazoezi? Je, ingekuwa vipi kama ungetumia muda huo kulala? Wataalamu wa afya wanashauri kuwa binadamu kwa kwaida anapaswa kulala angalau masaa 7 wakati wa usiku ili kuupa mwili afya bora. Kulala kwa muda mfupi au masaa machache husababisha matatizo ya afya, ikiwa ni pamoja na shinikizo la damu, unyogovu, ugonjwa wa kisukari, na kupunguzwa kinga kukabiliana na chanjo. Ni vyema ukatumia muda wako vizuri mchana ili usiku ukapata muda mwafaka wa kuweza kuupumzisha mwili ili kuepukana na magonjwa hatari ya shinikizo la damu, kisukari na kupungua kwa kinga mwilini. Najua mazingira yetu waafrika ya kimaisha wakati mwingine yanachangamoto nyingi, lakini pale upatapo mwanya kidogo tu, basi utumie yani "kila penye tundu, penyeza lupia" au wawenzetu wazungu wanasema "one chance two goals".