Skip to main content

Posts

Onyo Zito Latolewa Kampeni za Uchaguzi Katika Jimbo la Nyalandu

Recent posts

Tundu Lissu Kataja Kitu Ambacho Hatakisahau Tangu Apelekwe Nairobi

Tundu Lissu Kataja Kitu Ambacho Hatakisahau Tangu Apelekwe Nairobi Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Antiphas Lissu amekiri kwamba hatakuja kusahau tukio la mkazi wa Iringa aliyekwenda hospitali Nairobui alikolazwa kwa ajili ya kumuombea ili apate kupona baada ya kupigwa risasi na watu wasiojulikana. Lissu ameyasema hayo wakati akifanya mahojiano na chombo kimoja cha habari nchini, amedai kwamba mama huyo alimgusa sana kwa upendo aliouonyesha juu yake huku akizingatia kwamba ametokea mbali sana huku akionekana ni mtu wa hali ya chini. "Ukiwa mgonjwa kisha akaja mtu kukutembelea ni faraja sana. Nawashukuru maelfu ya watanzania na watu wote waliofika Nairobi kunijulia hali. Lakini sitakaa kuweza kumsahau mama mmoja aliyetoka Iringa kwa ajili ya kuja kuniombea," Lissu. Lissu ameongeza "Aliniambia Mheshimiwa nimetokea Iringa na mpaka nimefika hapa nimetumia siku tano. Nikamwambia mama asante niombee kisha akapiga magoti na kuniombea. Alinig

TRA Wakomaa na Askofu Kakobe.....Wadai Hawana muda wa Kubishana nae Zaidi ya Kuchunguza Utajiri wake

TRA Wakomaa na Askofu Kakobe.....Wadai Hawana muda wa Kubishana nae Zaidi ya Kuchunguza Utajiri wake Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), imemuibukia kivingine, Askofu wa Kanisa la Full Gosper Bible Fellowship (FGBF), Zakaria Kakobe, kuhusu utajiri alionao ikisema haina muda wa kulumbana naye, bali inatekeleza maelekezo ya Kamishna Mkuu. Aidha, mamlaka hiyo imesema haitaki kuwa kwenye malumbano na askofu huyo wakati ikiendelea na uchunguzi dhidi ya vitega uchumi vyake na kuangalia kama analipa kodi ya serikali. Mkurugenzi wa Elimu kwa Mlipakodi wa TRA, Richard Kayombo, jana alisema maofisa wao wanaendelea kutekeleza tamko la Kamishna Mkuu wa TRA, Charles Kichere, la kuchunguza utajiri wa Askofu Kakobe. "Sisi (TRA) hatutaki kuwa kwenye malumbano na Kakoke, tulichosema tumeishia hapo. Alichosema Kamishna Mkuu tunaishia hapohapo, hatutakiwi kujibishana naye," Kayombo alisema. Katika mkutano wake na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Jumam

Rais Magufuli Aomboleza Msiba Wa Mke Wa Naibu Waziri Kangi Lugola

Rais Magufuli Aomboleza Msiba Wa Mke Wa Naibu Waziri Kangi Lugola Mhe. Rais John Pombe Magufuli akitia saini kitabu cha maombelezo nyumbani kwa Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Kangi Alphaxard Lugola aliyefiwa na Mkewe Kamishna Msaidizi wa Polisi Mary Lugola ambaye alikuwa Afisa Mnadhimu Kikosi cha Polisi Reli Tanzania.  Alifariki dunia jana tarehe 01 Januari 2018 katika hospitali ya Rabinisia Memorial Tegeta Jijini Dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu. Msiba upo Gerezani Railway Club Jijini Dar es Salaam. Picha na Ikulu.  

Spika Ndugai Amjibu Tundu Lissu

Spika Ndugai Amjibu Tundu Lissu Spika  wa Bunge Job Ndugai amefunguka na kusema Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu pamoja na familia yake hawatambui kuwa Serikali hasa Bunge limeanza kufanya mazungumzo na watu wanaotaka kumsafirisha kwenda nje kwa matibabu zaidi. Ndugai amedai anatambua kuwa Tundu Lissu atasafirishwa na kwenda kwa matibabu zaidi nje ya Kenya ingawa hajajua ni lini lakini amesema kuwa watu ambao wamepanga kumpeleka huko kwenye matibabu tayari walishamtafuta yeye na kusema watashirikiana nao katika masuala ya matibabu. "Ni kweli kwamba atapelekwa nje zaidi ya Nairobi ila bado sijui mpaka sasa ni lini kwa kuwa sijajua tarehe bado japo nadhani itakuwa hivi karibuni na wale wanaomgharamia kumpeleka nje wameshawasiliana na mimi na hakika familia ya Lissu hata Tundu Lissu mwenyewe hajui hilo, anafikiri ni wao peke yao lakini najua na walishafika kwangu na kusema watagharamia wao" alisema Ndugai Spika Ndugai alizidi kueleza kuw

Mh. Sugu aitwa Polisi kuhojiwa

Mh. Sugu aitwa Polisi kuhojiwa Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi 'Sugu' na mratibu wa chama hicho Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Emmanuel Masonga wameitwa Polisi wakisema hawajui sababu ya wito huo. Hata hivyo, wawili hao wamesema wanahisi wito huo unatokana na mkutano wa hadhara alioitisha Sugu katika viwanja vya Shule ya Msingi Mwenge jijini Mbeya. Akizungumza kwa simu leo Jumanne Januari 2,2018 Sugu amesema juzi jioni alipigiwa simu na  Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Mbeya (RCO) kwamba pamoja na Masonga wafike jana ofisini kwake kuzungumza lakini alimueleza ilikuwa ni siku ya sikukuu hivyo itakuwa ngumu kwenda, hivyo walikubaliana wafike leo. "Walinipigia simu juzi jioni wakinitaka mimi na Masonga twende makao makuu ya polisi jana, nikawaambia itakuwa ni sikukuu hivyo tukakubaliana leo asubuhi, hivyo tupo njiani tunaelekea huko kuitika wito. Sijajua sababu, lakini nadhani ni uchochezi," amesema Sugu. Masonga amesema a

Tuhuma Mpya Za Tundu Lissu kwa Spika na Bunge

Tuhuma Mpya Za Tundu Lissu kwa Spika na Bunge Mbunge wa Singida Mashariki kupitia CHADEMA, Tundu Lissu ambaye yuko Nairobi nchini Kenya kwa matibabu, amesema kuwa Bunge la Tanzania halijatoa pesa yoyote kugharamia matibabu yake, kauli ambayo inatofautiana na Bunge ambayo ilisema imetuma fedha. Akizungumza kwenye mahojiano na moja ya television za hapa nchini, Tundu Lissu amesema hakuna pesa yoyote iliyotolewa na Bunge wala serikali, kwa ajili ya matibabu yake huko nchini Kenya. "Bunge halijatoa hata senti moja ya matibabu yangu, serikali haijatoa hata senti moja, familia yangu na ndugu zangu inasema mbunge amelazwa tangu Septemba 7, Spika wa Bunge hajaenda, Naibu Spika wa Bunge hajaenda, Katibu wa Bunge hajaenda, Tume ya huduma za Bunge haijaja, haijatoa hata senti 10 kugharamia matibabu yangu", amesema Tundu Lissu. Mnamo Septemba 7, 2017, Mbunge Tundu Lisu alipigwa risasi na watu wasiojulikana, tukio ambalo limemfanya alazwe hospitali kwa