Skip to main content

Onyo Zito Latolewa Kampeni za Uchaguzi Katika Jimbo la Nyalandu

Onyo Zito Latolewa Kampeni za Uchaguzi Katika Jimbo la Nyalandu

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk. Rehema Nchimbi, ameonya kuwa watu watakaovuruga mikutano ya kampeni za uchaguzi mdogo wa ubunge Jimbo la Singida Kaskazini, serikali itawashughulikia kwa mujibu wa sheria.

Dk. Nchimbi alitoa onyo hilo katika Kijiji cha Mtinko Wilaya ya Singida Vijijini alipokuwa akitoa taarifa ya mafanikio ya serikali ya awamu ya tano kwenye uzinduzi wa kampeni hizo.

Alisisitiza kwamba ili watambue kuwa ni mtumishi aliyetumwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM), ajitokeze mtu yeyote na kuthubutu kuvuruga ratiba ya mikutano ya kampeni.

Hata hivyo, aliwahakikishia wananchi kuwa mikutano ya kampeni itakuwa salama pamoja na uchaguzi huo kwani serikali imejipanga kikamilifu kudhibiti yeyote atakayeonekana anataka kuvuruga uchaguzi huo.

“Na ole wake na atokee mtu yeyote yule mwingine atakaeingilia katika njia hii ya uchaguzi salama, amani na utulivu ndipo mtakapotambua kwamba nimetumwa na serikali ya Chama Cha Mapinduzi,” alisema na kuongeza:

“Jiandaeni vizuri na wakati wa kura mjitokeze kwa wingi kupiga kura na kumchagua mgombea wa CCM, na siyo mwingine.”

Dk.Nchimbi aliyataja baadhi ya mafanikio yaliyopo katika jimbo hilo ni bomba na mafuta kutoka Horiri Uganda hadi Tanga ambalo kwa Singida Kaskazini lina sifa ya pekee yake na litakuwa limenyanyuka kiuchumi kuliko sehemu yeyote litakapopita.

“Na hapa Singida Kaskazini kutajengwa kambi, patajengwa kituo watakuja wataalamu na mabingwa wa hilo bomba ambao watakaa hapa kwa zaidi ya miaka mia moja, hawatakaa pengine bali watakuja kukaa Singida Kaskazini,”alisema.

Uchaguzi huo unafanyika baada ya aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Lazaro Nyalandu (CCM), kujiuzulu na kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Popular posts from this blog

Lema ahoji kushikiliwa mmiliki wa shule ya Lucky Vincent

Lema ahoji kushikiliwa mmiliki wa shule ya Lucky Vincent Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema   Dodoma. Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema amehoji sababu za polisi kumshikilia mmiliki wa shule ya Lucky Vincent badala ya trafiki waliokuwa barabarani siku ya ajali iliyoua watu 35. Akiomba mwongozo wa Spika kuhusu jambo hilo leo, amesema katika eneo husika kuna vizuizi vya ukaguzi vinne lakini trafiki hawakuona kuwa basi hilo lilikuwa kimezidisha watoto na hawakuwa wamefunga mikanda. Amesema badala ya trafiki hao kuchukuliwa hatua, anakamatwa mmiliki ambaye hakuwapo. Akijibu mwongozo huo, Naibu Spika, Dk Tulia Ackson amesema suala hilo halijatokea bungeni.

Jinsi Wachawi Wanavyo Tumia Mafiga Mabichi Ya Mti Wa Mfausiku Kupika Uchawi Wa Kumvuta Kimapenzi Mtu Aliye Mbali.

Jinsi Wachawi Wanavyo Tumia Mafiga Mabichi Ya Mti Wa Mfausiku Kupika Uchawi Wa Kumvuta Kimapenzi Mtu Aliye Mbali. Na. DOKTA  MUNGWA  KABILI …0744 -000  473.  Wachawi  wanaweza  kutumia  uchawi  kumvuta  kimapenzi  mtu  aliye  mbali. Moja  kati  ya  vitu  vinavyo  tumika  katika  uchawi  huu  ni  pamoja  na  mafiga  mabichi  ya  mti  wa  mfausiku  ambayo  hukokwa  kwenye  majani  makavu ya  mgomba  ambayo  hutumika  kama  kuni  au  moto,  kipande  cha  sanda  alichovalishwa  maiti, herufi za  moto,  mti wa hina, pamoja na  vitu  vingine  lukuki. Kufahamu  kuhusu  uchawi wa aina  hii  na  jinsi  ya  kujikinga  nao, fuatilia  sehemu  ya  nne  ya  kitabu “ ...

Bei ya unga sasa ni mara 12 ya mfuko wa Simenti

Bei ya unga sasa ni mara 12 ya mfuko wa Simenti WAKATI bei ya unga wa sembe ikipanda mpaka kufikia kuuzwa kati ya Sh. 2,200 na Sh. 2,500 kwa kilo, ile ya mfuko wa saruji wenye uzito wa kilo 50 imeshuka hadi sh. 9,000, sawa na Sh. 180 kwa kilo. Katika masoko na maduka mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam ambayo Nipashe ilitembelea jana, bei ya sembe ilikuwa ikiuzwa kwa kiasi hicho kwa rejareja huku wauzaji wa jumla wakiuza kiroba cha kilo 50 kwa kati ya sh.100,000 na sh.98,000. Ibrahim Omary, mfanyabiashara wa Kariakoo alisema anauza unga wa sembe kwa Sh. 2,400 kwa kuwa hununua kwa bei kubwa kutoka kwa wazalishaji. Alisema kampuni inayojulikana kwa jina la Mkulima huwauzia unga huo kwa Sh. 98,000 na Mama Neema huwauzia kwa sh. 100,000 kwa kiroba cha kilo 50. Kwenye baadhi ya maduka ya kula ya Kinondoni, unga umekuwa ukiuzwa kati ya Sh. 2,200 na Sh. 2,500. Tandika bei ya wastani ni Sh. 2,200, Mwenge Sh. 2,400, Kimara sh. 2,500 na Yombo Vituka sh. 2,200. ...