Skip to main content

Onyo Zito Latolewa Kampeni za Uchaguzi Katika Jimbo la Nyalandu

Onyo Zito Latolewa Kampeni za Uchaguzi Katika Jimbo la Nyalandu

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk. Rehema Nchimbi, ameonya kuwa watu watakaovuruga mikutano ya kampeni za uchaguzi mdogo wa ubunge Jimbo la Singida Kaskazini, serikali itawashughulikia kwa mujibu wa sheria.

Dk. Nchimbi alitoa onyo hilo katika Kijiji cha Mtinko Wilaya ya Singida Vijijini alipokuwa akitoa taarifa ya mafanikio ya serikali ya awamu ya tano kwenye uzinduzi wa kampeni hizo.

Alisisitiza kwamba ili watambue kuwa ni mtumishi aliyetumwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM), ajitokeze mtu yeyote na kuthubutu kuvuruga ratiba ya mikutano ya kampeni.

Hata hivyo, aliwahakikishia wananchi kuwa mikutano ya kampeni itakuwa salama pamoja na uchaguzi huo kwani serikali imejipanga kikamilifu kudhibiti yeyote atakayeonekana anataka kuvuruga uchaguzi huo.

“Na ole wake na atokee mtu yeyote yule mwingine atakaeingilia katika njia hii ya uchaguzi salama, amani na utulivu ndipo mtakapotambua kwamba nimetumwa na serikali ya Chama Cha Mapinduzi,” alisema na kuongeza:

“Jiandaeni vizuri na wakati wa kura mjitokeze kwa wingi kupiga kura na kumchagua mgombea wa CCM, na siyo mwingine.”

Dk.Nchimbi aliyataja baadhi ya mafanikio yaliyopo katika jimbo hilo ni bomba na mafuta kutoka Horiri Uganda hadi Tanga ambalo kwa Singida Kaskazini lina sifa ya pekee yake na litakuwa limenyanyuka kiuchumi kuliko sehemu yeyote litakapopita.

“Na hapa Singida Kaskazini kutajengwa kambi, patajengwa kituo watakuja wataalamu na mabingwa wa hilo bomba ambao watakaa hapa kwa zaidi ya miaka mia moja, hawatakaa pengine bali watakuja kukaa Singida Kaskazini,”alisema.

Uchaguzi huo unafanyika baada ya aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Lazaro Nyalandu (CCM), kujiuzulu na kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Popular posts from this blog

Jinsi Wachawi Wanavyo Tumia Mafiga Mabichi Ya Mti Wa Mfausiku Kupika Uchawi Wa Kumvuta Kimapenzi Mtu Aliye Mbali.

Jinsi Wachawi Wanavyo Tumia Mafiga Mabichi Ya Mti Wa Mfausiku Kupika Uchawi Wa Kumvuta Kimapenzi Mtu Aliye Mbali. Na. DOKTA  MUNGWA  KABILI …0744 -000  473.  Wachawi  wanaweza  kutumia  uchawi  kumvuta  kimapenzi  mtu  aliye  mbali. Moja  kati  ya  vitu  vinavyo  tumika  katika  uchawi  huu  ni  pamoja  na  mafiga  mabichi  ya  mti  wa  mfausiku  ambayo  hukokwa  kwenye  majani  makavu ya  mgomba  ambayo  hutumika  kama  kuni  au  moto,  kipande  cha  sanda  alichovalishwa  maiti, herufi za  moto,  mti wa hina, pamoja na  vitu  vingine  lukuki. Kufahamu  kuhusu  uchawi wa aina  hii  na  jinsi  ya  kujikinga  nao, fuatilia  sehemu  ya  nne  ya  kitabu “ KITANDA  CHA  SOKWE  MTU” kama  ifuatavyo : SEHEMU  YA  PILI   YA  KITABU  “ KITANDA  CHA  SOKWE  MTU “ Wachawi   wakishindwa  kukutengenezea  kesi  kubwa  basi  waatakufunga  kwenye  kifungo  cha  mapenzi.  Katika  vifungo  vyote anavyo  fungwa  mwanadamu  hakuna  kifungo  kibaya  kama  kifungo  cha  mape

Faida nyingine za kula chungwa

Faida nyingine za kula chungwa Siku kadhaa zilizopita tuliangalia kwa uchache kuhusu faida za kula chungwa hivyo, pia siku ya leo naomba tuendelee kwa kuangalia faida nyingine za kula chungwa. 1. Ulaji wa machungwa husaidia kutibu mapafu. Chungwa pia lina kiasi kikubwa cha Vitamin B6 na Madini ya Chuma (iron), virubisho ambavyo ni muhimu kwa uzalishaji wa seli nyekundu za damu, ambazo hufanya kazi ya kusafirisha hewa ya oksjeni mwilini, hivyo kuwa muhimu kwa kujikinga na ugonjwa wa mapafu. 2. Husaidia kuimarisha mifupa ya meno. Chungwa lina kiasi kingi cha madini ya kalisi (calcium) ambayo ni muhimu kwa uimarishaji wa mifupa na meno. 3. Husaidia kupunguza kiwango cha mafuta mwilini. Virutubisho vilivyomo kwenye chungwa, hasa kwenye maganda yake, hupunguza kiwango cha mafuta mabaya mwilini (bad cholesterol). Hivyo kwa wenye tatizo la lehemu wanashauriwa kula machungwa pamoja na nyama zake. 4. Hupunguza kupatwa magonjwa wa figo. Ulaji wa machungwa mara kwa mara, ukusaid

Je, unajua Binadamu anatakiwa kulala masaa mangapi?

Je, unajua Binadamu anatakiwa kulala masaa mangapi? Unafikili ni wazo zuri kuamka  saa 11 za asubuhi na kufanya mazoezi? Je, ingekuwa vipi kama ungetumia muda huo kulala? Wataalamu wa afya wanashauri kuwa binadamu kwa kwaida anapaswa kulala angalau masaa 7 wakati wa usiku ili kuupa mwili afya bora. Kulala kwa muda mfupi au masaa machache husababisha matatizo ya afya, ikiwa ni pamoja na shinikizo la damu, unyogovu, ugonjwa wa kisukari, na kupunguzwa kinga kukabiliana na chanjo. Ni vyema ukatumia muda wako vizuri mchana ili usiku ukapata muda mwafaka wa kuweza kuupumzisha mwili ili kuepukana na magonjwa hatari ya shinikizo la damu, kisukari na kupungua kwa kinga mwilini. Najua mazingira yetu waafrika ya kimaisha wakati mwingine yanachangamoto nyingi, lakini pale upatapo mwanya kidogo tu, basi utumie yani "kila penye tundu, penyeza lupia" au wawenzetu wazungu wanasema "one chance two goals".