Skip to main content

Posts

Showing posts from February, 2017

VIROBA Marufuku Kuanzia Leo

VIROBA Marufuku Kuanzia Leo Mtakumbuka tarehe 20 Februari 2017 Ofisi ya Makamu wa Rais ilitoa tamko la Serikali la utaratibu utakaotumika kutekeleza agizo la kusitisha utengenezaji, uuzaji na matumizi ya pombe kali zinazofungashwa kwenye vifungashio vya plastiki (viroba)kuanzia tarehe 1 Machi 2017.  Utekelezaji wa katazo hili utazingatia Ibara ya 8(1) (b) na 14, Sheria ya Mazingira ya mwaka 2004 na Kanuni zake zilizotungwa kupitia kifungu 230 (2) (f) cha sheria hiyo, na Sheria ya Leseni za Vileo Namba 28 ya mwaka 1968 pamoja na marekebisho yake ya mwaka 2012. Napenda kusisitiza na kuujulisha umma wa Tanzania kuwa utekelezaji wa maamuzi haya ya Serikali kuhusu usitishaji uingizaji, uzalishaji, uuzaji na matumizi ya vifungashio vya plastiki vya kufungia pombe kali utaanza rasmi tarehe 01 Machi, 2017, katika Mikoa yote ya Tanzania Bara. Operesheni ya kukagua utekelezaji wa agizo la serikali la usitishaji utengenezaji, uuzaji na matumizi ya pombe zinazofungashwa k

Waziri Mkuu Anusa Madudu Minada Ya Madini.......Amuagiza Kamishna wa Madini aende Mererani

Waziri Mkuu Anusa Madudu Minada Ya Madini.......Amuagiza Kamishna wa Madini aende Mererani WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema anafuatilia kwa makini minada ya madini inayofanyika nchini kwa sababu anazo taarifa za kukiukwa utaratibu kwenye minada hiyo. Amesema ukiukwaji huo unachangia kutobadilika kwa mapato ya mauzo yatokanayo na mnada hata kama kuna vito viliyokakatwa au havijakatwa. Ametoa kauli hiyo juzi jioni (Jumatatu, Februari 27, 2017) wakati akihitimisha kikao alichokiitisha kwenye makazi yake Oysterbay jijini Dar es Salaam kilichojumuisha Mawaziri wa Fedha pamoja na Nishati, Mkuu wa Mkoa wa Manyara na watendaji wake, Mbunge wa Simanjiro, wamiliki wa mgodi wa Tanzanite One, watumishi waliofukuzwa kazi na wachimbaji wadogo. Alisema licha ya kuwa Kitengo cha Uthaminishaji wa Madini ya Almasi na Vito cha Wizara ya Nishati na Madini (TANSORT) kinasifiwa kwa kuongeza mapato ya madini, bado kuna kazi ya ziada inabidi ifanyike kwenye minada hiyo i

Watano wakamatwa kwa tuhuma za kupatikana na dawa za kulevya

Watano wakamatwa kwa tuhuma za kupatikana na dawa za kulevya Jeshi la polisi mkoani Morogoro limewakamata watuhumiwa watano kwa tuhuma za kupatikana na dawa za kulevya ikiwemo bangi kilo mia moja, mirungi kilo sitini, heroine kete tatu na vifungashio vya dawa hizo katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa Morogoro, ikiwa ni jitihada za kuendeleza vita dhidi ya matumizi na uuzaji wa dawa hizo. Kamanda wa polisi mkoa wa Morogoro Ulrich Matei amesema watuhumiwa hao wamekamatwa katika maeneo tofauti ya mkoa wa Morogoro ikiwemo wilaya za Mvomero, Morogoro manispaa na Kilombero,wakiwemo watuhumiwa waliokuwa wakisafirisha dawa hizo  kwa magari ya abiria, basi la BM Coach huko Mkindo Turiani, na gari ndogo aina ya Hiace maeneo ya Kihonda, pamoja na pikipiki maarufu kama boda boda. Baadhi ya watuhumiwa waliohojiwa kuhusiana na dawa hizo, wamekuwa na majibu tofauti, wengi wakidai kutumwa na watu mizigo hiyo ikiwemo mirungi na bangi, ambapo aliyekuwa amebeba debe nne za bangi kwa kuficha ndiz

Haya ndio Makabila 125 ya TANZANIA

Haya ndio Makabila 125 ya TANZANIA Hii ni orodha ya makabila ya watu ambao wamekuwa wanaishi tangu zamani katika eneo ambalo sasa linaitwa Tanzania, pamoja na makabila yaliyogawiwa na mipaka baina ya Tanzania na nchi za jirani. Waalagwa (pia wanaitwa Wasi) Waakiek Waarusha Waassa Wabarabaig (pia wanaitwa Wamang'ati) Wabembe Wabena Wabende Wabondei Wabungu (au Wawungu) Waburunge Wachagga Wadatoga Wadhaiso Wadigo Wadoe Wafipa Wagogo Wagorowa (pia wanaitwa Wafiome) Wagweno Waha Wahadzabe (pia wanaitwa Wahadza na Watindiga) Wahangaza Wahaya Wahehe Waikizu Waikoma Wairaqw (pia wanaitwa Wambulu) Waisanzu Wajiji Wajita Wakabwa Wakaguru Wakahe Wakami Wakara (pia wanaitwa Waregi) Wakerewe Wakimbu Wakinga Wakisankasa Wakisi Wakonongo Wakuria Wakutu Wakw'adza Wakwavi Wakwaya Wakwere (pia wanaitwa Wanghwele) Wakwifa Walambya Waluguru Waluo Wamaasai Wamachinga Wamagoma Wamakonde Wamakua (au Wamakhuwa) Wamakwe (pia wanaitw

Waandamanaji wapanda mgomba katikati ya barabara Nairobi

Waandamanaji wapanda mgomba katikati ya barabara Nairobi   Wahudumu wa magari ya usafiri nchi Kenya, yanayofahamika kama matatu wamefanya maandamano kulalamikia hali mbaya ya barabara kwenye mitaa ya mji mkuu Nairobi. Kituo kimoja cha redio kimetuma picha ya waandamanaji wakipanda mgomba wa ndizi barabarani kwenye mtaa wa Kayole, kama njia ya kusema kuwa barabara iyo inaweza kuwa bora kwa kilimo kuliko iwe barabara ya magari.

Urusi na China zatumia kura turufu kuisaidia Syria

Urusi na China zatumia kura turufu kuisaidia Syria Urusi na China zimetumia kura turufu kuzuia jaribio la Umoja wa Mataifa la kutaka kuiwekea vikwazo serikali ya Syria. Marekani, Uingereza na nchi nyengine katika Baraza la Usalama, zilitaka kuiadhibu Damascus kwa tuhuma za kutumia silaha za sumu katika maeneo ya waasi. Ni mara ya saba sasa Urusi inatumia kura yake ya VETO kuikinga serikali ya Rais Assad na tuhuma za kimataifa. Katika hotuba yake iliyojawa hisia kabla ya kura, balozi wa Uingereza katika Umoja wa Mataifa, Matthew Rycroft, alisimulia kifo cha mwathirika mmoja ambae alipelekwa katika hospitali baada ya shambulio la gesi yenye sumu. Hata hivyo, kwa upande wake, balozi wa China katika Umoja wa Mataifa, Liu Jieyi, ameliambia Baraza la Usalama kwamba bado hakuna vilelezo kwamba serikali ya Syria imetumia silaha za kemikali. Naye Rais Vladmir Putin amesema vikwazo vitazuia jitihada za mazungumzo ya amani yanayoendelea Geneva baina ya serikali na wapinzani wake. Marekani

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya March 1

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya March 1

Tucta yawakingia kifua wadaiwa HESLB

Tucta yawakingia kifua wadaiwa HESLB Dar es Salaam.   Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (Tucta) limetoa siku 14 kwa Serikali kuwarejeshea wafanyakazi fedha za mikopo ya elimu ya juu wanazokatwa kimakosa vinginevyo watafanya uamuzi mgumu Akizungumza leo (Jumanne) Rais wa Tucta, Tumaini Nyamhokwa amesema wafanyakazi hao waliingia mkataba na Bodi ya Mikopo ya wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) ya kukatwa asilimia nane. Amesema baada ya sheria mpya iliyopitishwa Agosti 2016 imebadilisha na sasa wanakatwa asilimia 15 bila kujali walikopa lini mikopo hiyo. "Tunataka waliokopa kabla ya kupitishwa sheria hii waendelee kukatwa asilimia nane na siyo asilimia 15 wanayokatwa" amesema.

Soma Ujumbe huu, Usipuuzie usije ukaingia mkenge

Soma Ujumbe huu, Usipuuzie usije ukaingia mkenge KUTOKA JESHI LA POLICE: USALAMA WA MAISHA YAKO Usinunue simu za Android kwa mtu usiyemjua. Hiyo ni hatari kwani hujui huyo jamaa kaitoa wapi, mwisho wa siku unapewa kesi ya wizi au mauaji. Inawezekana simu hiyo iliibiwa kwa mtu aliyeuawa.   Usimpe mtu usiyemjua simu yako apige sehemu yoyote.   Unapoiona line njiani ipo chini, usitake kuiokota na kuiweka simuni mwako ujue ina shilingi ngapi ili uchukue salio. Simu inapoibiwa au mwenye simu kuuawa, line hutupwa, unapoiweka simuni mwako,simuyako inahusishwa na tukio hilo Unapoweka salio, hakikisha karatasi ya vocha unaichana. Unapoitupa, watu wanaweza kufanya mauaji, wakachukua karatasi ya vocha ile na kuweka sehemu ya tukio au pale ulipoitupa kukatokea tukio na wewe kuhusishwa.  Usikubali kumsajilia mtu line yake kwa jina lako, hata kama baba yako, usikubali. Kumbuka namba yako umesajiliwa, moja ya matukio hayo yakitokea na namba yako kuonekana, moja kwa moja unakuwa mtuh

Raia wa Ufaransa wamtaka 'Obama kuwania urais nchini humo'

Raia wa Ufaransa wamtaka 'Obama kuwania urais nchini humo' Ombi la mtandao la kumtaka Barrack Obama kuwania urais katika uchaguzi mkuu nchini Ufaransa limewavutia takriban wafuasi 42,000. Mabango ya kampeni yanayosomeka ''Oui, on Peut'' ikimaanisha kauli mbiu ya kmpeni ya Obama ''Yes we can'' yametumika mjini Paris. Bwana Obama sio raia wa Ufaransa hivyobasi hawezi kugombea urais. Lakini wale wanaofanya mzaha huo wanasema kuwa lengo lao ni kuonyesha kwamba hakuna wagombea wazuri . Ujumbe wao kwa wagombea hao kama alivyosema mmoja ya waandalizi wa ombi hilo ni ''jamani hamufai'. Wapiga kura wa Ufaransa watashiriki katika uchaguzi mkuu mnamo tarehe 25 mwezi Aprili na iwapo wagombea hawatapata asilimia 50 ya kura katika raundi ya kwanza basi wapiga kura watarudi tena mnamo tarehe 7 mwezi Mei ili kuamua kati ya wagombea wawili waliopata kura nyingi. Mgombea mwenye umaarufu katika uchaguzi huo ni Marine Le Pen ambaye amenufaiki na

Bei mpya za mafuta zimepanda

Bei mpya za mafuta zimepanda Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imetangaza bei elekezi za mafuta ya petroli na dizeli kwa mwezi Machi mwaka huu ambapo mafuta ya petroli na disel kwa bei za jumla na reja reja imepanda. Meneja Uhusiano na Mawasiliano wa Ewura Bw. Titus Kaguo amesema bei hizo zimepanda kutokana na mabadiliko katika soko la dunia ambapo kwa upande wa mafuta ya rejareja, petroli imepanda kwa wastani wa Shilingi 102 kwa lita sawa na asilimia 5.18 huku dizeli ikiwa imepanda kwa shilingi 51 kwa lita sawa na ongezeko la asilimia 2.76. Bw. Kaguo amesema bei hizo mpya zitaanza kutumika rasmi kesho Machi 01, na zitabadilika kulingana na nguvu ya soko katika mkoa husika ambapo kwa jiji la Dar es Salaam, lita moja ya petroli itauzwa kwa shilingi 2,060 na dizeli Shilingi 1,913 huku kukiwa hakuna mabadiliko yoyote ya bei kwa upande wa mafuta ya taa.

Watu 6000 kuajiriwa katika Kiwanda cha Vigae Chalinze

Watu 6000 kuajiriwa katika Kiwanda cha Vigae Chalinze Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa (TIC), Clifford Tandari akizungumza na waandishi wa habari juu ya hatua ya uwekezaji wa viwanda uliofikiwa katika nchi naja  jijini Dar es Salaam. KIWANDA  cha Vigae cha Twayfod kinatarajia kuajiri watu 4000 wa moja kwa moja na pamoja na ajira za muda mfupi 2000. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Uwekezaji  nchini, Clifford Tandari amesema kauli ya Rais Dk.John Magufuli ya Tanzania ya viwanda imeanza kutimia. Tandari amesema kuwa wanaendelea kuchakata makampuni mbalimbali ambayo yameonyesha dhamira ya kutaka kuwekeza katika sekta ya viwanda hivyo ni fursa ya watanzania kuchangamkia ajira zinazojitokeza. Ameongeza kuwa kiwanda cha vigae kitakachojengwa katika mji wa Chalinze kitatumia malighafi zinazozalishwa hapa nchini ambapo kuna maeneo yatapata mapato yatayotokana na malighafi hizo. Ameongeza kuwa kiwanda cha vigae kitaanza hivi karibuni h

Serikali yabaini Bandari bubu ya dawa za kulevya.

Serikali yabaini Bandari bubu ya dawa za kulevya. Serikali imewaagiza watendaji wa mkoa wa Tanga kuhakikisha kuwa wanafanya operesheni maalum ya vyombo vya ulinzi na usalama katika eneo la bandari bubu ya Kigombe iliyopo pembeni mwa bahari ya Hindi,baada ya kubaini kuwepo kuwa eneo hilo ndio lango kuu la uingizaji dawa za kulevya,usafirishaji wahamiaji haramu kutoka nchi jirani ya kenya na uvuvi haramu wa mabomu. Akizungumza na kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa Tanga,watendaji wa serikali pamoja na wananchi wa eneo la Kigombe,naibu waziri wa kilimo,mifugo na uvuvi mheshimiwa William Ole Nasha amesema ni lazima operesheni zifanywe kila wakati kwa sababu eneo la Kigombe limebainika kuwa ni kunafanyika uhalifu wa kimataifa ikiwemo kusafirisha binadamu kutoka nchi moja kwenda nyingine. Awali mbunge wa jimbo la Muheza mheshimiwa balozi Adad Rajab amesema mbali na uhalifu wa kimataifa kufanyika katika eneo la bandari ya Kigombe,pia vijana wengi wamekuwa wakitumia vyombo vya majini k

Charles Hillary Ateuliwa Kamati Ya Kuhamasisha Serengeti Boys

Charles Hillary Ateuliwa Kamati Ya Kuhamasisha Serengeti Boys MWANDISHI  nguli wa habari na mtangazaji nyota wa kimataifa, Charles Hillary ameteuliwa kuongoza Kamati ya watu 10 watakaohamasisha kuwaunganisha Watanzania kwa pamoja ili kuichangia timu ya vijana chini ya umri wa chini ya miaka 17, Serengeti Boys. Uteuzi huo umetangazwa leo na Waziri Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Moses Nnauye mbele ya wanafamilia ya mpira wa miguu waliohudhuria kongamano ya kujadili juu ya ushiriki wa Tanzania katika michuano ya kimataifa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Mada ilikuwa ni Tanzania kushiriki michuano ya Olimpiki Tanzania, lakini kwa kuwa kuna jambo la usoni la timu ya Serengeti Boys kucheza fainali za Kombe la Dunia huko Gabon kuanzia Mei 21, mwaka huu, Waziri Nape atakatangaza kamati ya kuhamamsisha ili Watanzania kwa pamoja waweze kuchangia. Akitangaza kamati hiyo, Nape alisema kwamba Katibu wa Kamati hiyo atakuwa Mwesigwa Selestine ambaye ni Katibu Mkuu wa Shirikisho la

Taarifa ya TFDA kuhusu dawa P-500® Paracetamol kuingia Tanzania

Taarifa ya TFDA kuhusu dawa P-500® Paracetamol kuingia Tanzania Baada ya kuzuka taarifa ya kuingia nchini Dawa aina ya  P-500® Paracetamol Tablets IP inayodaiwa kuwa na virusi vya Machupo,  Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania, TFDA ambayo ni Wakala wa Wizara ya Afya wa kudhibiti usalama, ubora na ufanisi wa chakula, Dawa, Vipodozi na Vifaa Tiba nchini imekanusha kuwepo kwa dawa hiyo nchini. Kwa mujibu wa taarifa kwa umma iliyotolewa na  Mkurugenzi  wa mamlaka hiyo imeeleza kuwa Dawa hiyo inayotengenezwa na kampuni ya  Apex Laboratories Private Limited-Tamil Nadu  ya  India   haijasajiliwa nchini na haipo kwenye soko la Tanzania. Aidha Mamlaka imewataka Wananchi kutoendelea kusambaza taarifa za uvumi ambazo zina lengo la kuwaogopesha na kuzua taharuki kwa wananchi kabla ya kupata ufafanuzi kutoka mamlaka husika.

Daraja La Bonyokwa-Kinyerezi lafunguliwa Rasmi na Meya wa Ilala

Daraja La Bonyokwa-Kinyerezi lafunguliwa Rasmi na Meya wa Ilala    Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, Charles Kuyeko, akikiwa amekata utepe ikiwa ni ishara ya  kufungua rasmi  daraja linalounganisha Kata ya Bonyokwa na Kata ya Kinyerezi katika Manispaa ya Ilala, jijini Dar es salaam.  Mbunge wa Viti Maalumu, Anatropia Theonesti (Chadema) akihutubia wakati wa ufunguzi wa daraja hilo MSTAHIKI MEYA  wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, Charles Kuyeko jana alifungua rasmi daraja linalounganisha Kata ya Bonyokwa na Kata ya Kinyerezi katika Manispaa ya Ilala, jijini Dar es salaam. Awali akizungumza katika hafla hiyo Mhandisi wa Manispaa ya Ilala ndugu Benjamin Maziku alisema  daraja hili limejengwa kwa takribani mwaka mmoja na kugharimu Tsh.million  478 hadi kukamilika kwake leo hii. Ujenzi wa daraja hili umesua sua kwa siku nyingi kutokana na sababu mbali mbali lakini kutokana na usimamizi imara wa Mstahiki Meya wa Ilala Mhe. Charles Kuyeko sasa histor

Irene Uwoya: Wasanii tusikubali kutawaliwa na siasa

Irene Uwoya: Wasanii tusikubali kutawaliwa na siasa Baada ya kashikashi za hapa na pale ya wasanii wa bongo movie kuingia kwenye siasa huku Wema Sepetu akihamia CHADEMA na kusema anaidai CCM, swahiba wake, Batuli amekanusha. Wakati vita vya maneno vikiendelea, mwenzao, Irene Uwoya amewachana. Irene ametumia ukurasa wake wa Instagram kuandika maneno yenye busara ndani: Katika maisha siku zote ushauri unaruhusiwa kutolewa au kupokelewa… Lakin sio lazima mtu kupokea ushauri unaotolewa… Kila mtu anauhuru wakuamua kitu ambacho anahisi kinamfaa kwenye maisha sababu… Sazingine kwenye maisha Kuna sehemu inafika unacho jiskia kwenye moyo wako sio rahisi mtu mwingine kujiskia … Sasa ni mbaya sana kuishi kwa hisia… Ifikie Wakati tujitaidi kuheshimu hisia Za mtu… Lakin pia kunavitu vingine nazani Nivyema vkabaki kwa wausika wavinaowahusu…yani sio lazima kuongea kila kitu kwenye jamiii… Watu wanatamani sazingine kuskia vtu ambavyo wanahisi vinafaida kwa Jamaniii… Kunavitu vingine ukiongea