Skip to main content

Charles Hillary Ateuliwa Kamati Ya Kuhamasisha Serengeti Boys

Charles Hillary Ateuliwa Kamati Ya Kuhamasisha Serengeti Boys

MWANDISHI nguli wa habari na mtangazaji nyota wa kimataifa, Charles Hillary ameteuliwa kuongoza Kamati ya watu 10 watakaohamasisha kuwaunganisha Watanzania kwa pamoja ili kuichangia timu ya vijana chini ya umri wa chini ya miaka 17, Serengeti Boys.

Uteuzi huo umetangazwa leo na Waziri Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Moses Nnauye mbele ya wanafamilia ya mpira wa miguu waliohudhuria kongamano ya kujadili juu ya ushiriki wa Tanzania katika michuano ya kimataifa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mada ilikuwa ni Tanzania kushiriki michuano ya Olimpiki Tanzania, lakini kwa kuwa kuna jambo la usoni la timu ya Serengeti Boys kucheza fainali za Kombe la Dunia huko Gabon kuanzia Mei 21, mwaka huu, Waziri Nape atakatangaza kamati ya kuhamamsisha ili Watanzania kwa pamoja waweze kuchangia.

Akitangaza kamati hiyo, Nape alisema kwamba Katibu wa Kamati hiyo atakuwa Mwesigwa Selestine ambaye ni Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) wakati wajumbe ni Mtangazaji wa Radio ya EFM, Maulidi Kitenge; Mkurugenzi wa Mahusiano wa kampuni ya Airtel Tanzania, Beatrice Singano na Mrembo wa Tanzania wa mwaka 1999, Hoyce Temu.

Pia wamo Mkurugenzi wa Habari katika Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hassan Abbas; Mkurugenzi wa Global Publishers Limited, Eric Shigongo; bosi wa radio Clous, Ruge Mutahaba pamoja wa wasanii wa kizazi kipya Diamond Platnums na Ally ‘King’ Kiba.

Pamoja na hayo, katika kongamano hilo na wadau wa soka wadau ikiwamo Serikali iliridhia kuwa mshiriki wa karibu kwa kila hatua kuanzia Bodi ya Mfuko wa Maendeleo ya timu za taifa, Kamati ya Hamasa kwa lengo la kupanga pamoja na kushirikiana kwa pamoja.

Wameazimia kuwa na chanzo cha fedha cha kueleweka ili kufanikisha program mbalimbali za timu za taifa ikiwamo ya U23 ambayo inatakiwa kushiriki kwenye michuano ya Olimpiki. Serikali imepanga kuwa pamoja badala ya kile kinachoitwa kudandia matokeo mafanikio bila kushiriki maandalizi.

Kadhalika wameazimia mpira kuwa jambo la nchi ili hamasa inayotangazwa iguse wadau wote kwa maana ya Watanzania wote.

Pia chanzo cha kupata vipaji kiwe pia kutoka mashuleni (Umitashumta na Umiseta) ambako Mheshimiwa Waziri Nape mbali ya kuthibitisha kuwa mwaka huu itafanyika tofauti na mwaka jana, pia aliagiza kuwa isiwe kama matamasha.

Popular posts from this blog

Jinsi Wachawi Wanavyo Tumia Mafiga Mabichi Ya Mti Wa Mfausiku Kupika Uchawi Wa Kumvuta Kimapenzi Mtu Aliye Mbali.

Jinsi Wachawi Wanavyo Tumia Mafiga Mabichi Ya Mti Wa Mfausiku Kupika Uchawi Wa Kumvuta Kimapenzi Mtu Aliye Mbali. Na. DOKTA  MUNGWA  KABILI …0744 -000  473.  Wachawi  wanaweza  kutumia  uchawi  kumvuta  kimapenzi  mtu  aliye  mbali. Moja  kati  ya  vitu  vinavyo  tumika  katika  uchawi  huu  ni  pamoja  na  mafiga  mabichi  ya  mti  wa  mfausiku  ambayo  hukokwa  kwenye  majani  makavu ya  mgomba  ambayo  hutumika  kama  kuni  au  moto,  kipande  cha  sanda  alichovalishwa  maiti, herufi za  moto,  mti wa hina, pamoja na  vitu  vingine  lukuki. Kufahamu  kuhusu  uchawi wa aina  hii  na  jinsi  ya  kujikinga  nao, fuatilia  sehemu  ya  nne  ya  kitabu “ KITANDA  CHA  SOKWE  MTU” kama  ifuatavyo : SEHEMU  YA  PILI   YA  KITABU  “ KITANDA  CHA  SOKWE  MTU “ Wachawi   wakishindwa  kukutengenezea  kesi  kubwa  basi  waatakufunga  kwenye  kifungo  cha  mapenzi.  Katika  vifungo  vyote anavyo  fungwa  mwanadamu  hakuna  kifungo  kibaya  kama  kifungo  cha  mape

Faida nyingine za kula chungwa

Faida nyingine za kula chungwa Siku kadhaa zilizopita tuliangalia kwa uchache kuhusu faida za kula chungwa hivyo, pia siku ya leo naomba tuendelee kwa kuangalia faida nyingine za kula chungwa. 1. Ulaji wa machungwa husaidia kutibu mapafu. Chungwa pia lina kiasi kikubwa cha Vitamin B6 na Madini ya Chuma (iron), virubisho ambavyo ni muhimu kwa uzalishaji wa seli nyekundu za damu, ambazo hufanya kazi ya kusafirisha hewa ya oksjeni mwilini, hivyo kuwa muhimu kwa kujikinga na ugonjwa wa mapafu. 2. Husaidia kuimarisha mifupa ya meno. Chungwa lina kiasi kingi cha madini ya kalisi (calcium) ambayo ni muhimu kwa uimarishaji wa mifupa na meno. 3. Husaidia kupunguza kiwango cha mafuta mwilini. Virutubisho vilivyomo kwenye chungwa, hasa kwenye maganda yake, hupunguza kiwango cha mafuta mabaya mwilini (bad cholesterol). Hivyo kwa wenye tatizo la lehemu wanashauriwa kula machungwa pamoja na nyama zake. 4. Hupunguza kupatwa magonjwa wa figo. Ulaji wa machungwa mara kwa mara, ukusaid

Je, unajua Binadamu anatakiwa kulala masaa mangapi?

Je, unajua Binadamu anatakiwa kulala masaa mangapi? Unafikili ni wazo zuri kuamka  saa 11 za asubuhi na kufanya mazoezi? Je, ingekuwa vipi kama ungetumia muda huo kulala? Wataalamu wa afya wanashauri kuwa binadamu kwa kwaida anapaswa kulala angalau masaa 7 wakati wa usiku ili kuupa mwili afya bora. Kulala kwa muda mfupi au masaa machache husababisha matatizo ya afya, ikiwa ni pamoja na shinikizo la damu, unyogovu, ugonjwa wa kisukari, na kupunguzwa kinga kukabiliana na chanjo. Ni vyema ukatumia muda wako vizuri mchana ili usiku ukapata muda mwafaka wa kuweza kuupumzisha mwili ili kuepukana na magonjwa hatari ya shinikizo la damu, kisukari na kupungua kwa kinga mwilini. Najua mazingira yetu waafrika ya kimaisha wakati mwingine yanachangamoto nyingi, lakini pale upatapo mwanya kidogo tu, basi utumie yani "kila penye tundu, penyeza lupia" au wawenzetu wazungu wanasema "one chance two goals".