Skip to main content

Aingia matatani baada ya kupulizia wenzake kemikali usoni

Aingia matatani baada ya kupulizia wenzake kemikali usoni


MADALALI wanne wa madini ya Tanzanite (mawe), wanashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kuwaumiza macho kwa kemikali aina ya ‘pepper spray’ baada ya kutofautiana malipo na madalali wenzao waliowauzia madini hayo.

Habari kutoka polisi zilithibitisha jana kuwashikilia madalali hao, Schola Mwanga, Margareth Mushi, Sued Mwanga na Dorice Mushi, kwa tuhuma za kufanya kitendo hicho.

Hata hivyo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Charles Mkumbo hakuweza kupatikana kutoa ufafanuzi zaidi.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufani ya Mkoa ya Mount Meru, Dk. Jackline Urio, alithibitisha kupokea wagonjwa watano ambao alisema uchunguzi unaendelea kujua walimwagiwa aina gani ya kemikali.

Alisema kutokana na hali zao, wagonjwa hao walitarajiwa kuhamishiwa Hospitali ya Rufani ya KCMC ya mkoani Kilimanjaro, jana.

Alisema waliojeruhiwa walikuwa katika biashara ya madini na wakaletwa hapa wakilalamika macho yanauma, wakapewa huduma ya kwanza ya kuwaosha macho kwa kushauriana na madaktari bingwa wa macho wa Dar es Salaam.

Aliwataja wagonjwa hao kuwa ni Sabas Laizer, Lucas Soto, George Nyakila, Moringe Mollel na Ngalama Mapena.

Alisema watu hao walidai kumwagiwa ‘spray’ kwenye macho, majira ya saa 10 na walianza kufikishwa hospitalini hapo mmoja mmoja kuanzia saa 12 jioni.

"Lakini kwa sasa tunawahamishia hospitali ya KCMC kwa sababu kule kuna madaktari bingwa wa macho, watachunguzwa vizuri kujua madhara waliyopata," alisema.

Wakizungumzia tukio hilo lililotokea mtaa wa Pangani jijini hapa, baadhi ya watu walioshuhudia, walidai madalali hao walitaka walipwe fedha (kamisheni) ya kuwauzia mawe hayo.

Lakili walisema madalali waliopewa mawe hayo kuuza walishindwa kuwapa fedha hizo kwa kile walichodai walikuwa bado hawajalipwa.

Walisema hali hiyo ilizua kutoelewana kati yao kiasi cha kuzua ugomvi na ndipo dalali mmoja alipoingia ndani ya gari na kuchukua ‘pepper spray’ na kuwapulizia usoni.

“Pepper spray’ ni aina ya kemikali inayowekwa katika kopo maalum mithili ya dawa ya mbu na ikipulizwa usoni kwa mtu inaumiza macho yake na kuyafanya yasione kwa muda.

Katibu wa Chama cha Madakali mkoani hapa, Noel Olovaroya, alisema tukio hilo lilitokea baada ya kutofautiana katika masuala ya biashara.

Alishukuru daktari bingwa wa hospitali hiyo kwa kuwashughulikia vizuri wagonjwa hao na kuomba serikali kuongeza madaktari wa macho katika hospitali hiyo.

Akizungumza kwa niaba ya madalali wenzake, waliojeruhiwa, Ngalama Mapena ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Madalali wa Madini, alisema chanzo cha tukio hilo ni yeye aliuziwa madini ya Tanzanite na dalali mmoja kwa Sh milioni 3.2 na makubaliano yalikuwa angemlipa kesho yake (juzi)  ambayo ndio siku ya tukio.

"Lakini nikiwa pale baada ya kujibu hivyo nikaona gari RAV 4 rangi nyeusi, wakashuka wanawake wawili ambapo mmoja namfahamu akanipulizia kitu kama perfume usoni na huku akitukana na ghafla nikapoteza fahamu," alisema.
Alisema mwanamke huyo ni dalali mwenzake.

Popular posts from this blog

Lema ahoji kushikiliwa mmiliki wa shule ya Lucky Vincent

Lema ahoji kushikiliwa mmiliki wa shule ya Lucky Vincent Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema   Dodoma. Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema amehoji sababu za polisi kumshikilia mmiliki wa shule ya Lucky Vincent badala ya trafiki waliokuwa barabarani siku ya ajali iliyoua watu 35. Akiomba mwongozo wa Spika kuhusu jambo hilo leo, amesema katika eneo husika kuna vizuizi vya ukaguzi vinne lakini trafiki hawakuona kuwa basi hilo lilikuwa kimezidisha watoto na hawakuwa wamefunga mikanda. Amesema badala ya trafiki hao kuchukuliwa hatua, anakamatwa mmiliki ambaye hakuwapo. Akijibu mwongozo huo, Naibu Spika, Dk Tulia Ackson amesema suala hilo halijatokea bungeni.

Bei ya unga sasa ni mara 12 ya mfuko wa Simenti

Bei ya unga sasa ni mara 12 ya mfuko wa Simenti WAKATI bei ya unga wa sembe ikipanda mpaka kufikia kuuzwa kati ya Sh. 2,200 na Sh. 2,500 kwa kilo, ile ya mfuko wa saruji wenye uzito wa kilo 50 imeshuka hadi sh. 9,000, sawa na Sh. 180 kwa kilo. Katika masoko na maduka mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam ambayo Nipashe ilitembelea jana, bei ya sembe ilikuwa ikiuzwa kwa kiasi hicho kwa rejareja huku wauzaji wa jumla wakiuza kiroba cha kilo 50 kwa kati ya sh.100,000 na sh.98,000. Ibrahim Omary, mfanyabiashara wa Kariakoo alisema anauza unga wa sembe kwa Sh. 2,400 kwa kuwa hununua kwa bei kubwa kutoka kwa wazalishaji. Alisema kampuni inayojulikana kwa jina la Mkulima huwauzia unga huo kwa Sh. 98,000 na Mama Neema huwauzia kwa sh. 100,000 kwa kiroba cha kilo 50. Kwenye baadhi ya maduka ya kula ya Kinondoni, unga umekuwa ukiuzwa kati ya Sh. 2,200 na Sh. 2,500. Tandika bei ya wastani ni Sh. 2,200, Mwenge Sh. 2,400, Kimara sh. 2,500 na Yombo Vituka sh. 2,200. ...

Jinsi ya kutengeneza SABUNI ya kipande YA KUGANDISHA

Jinsi ya kutengeneza SABUNI ya kipande YA KUGANDISHA Utengenezaji wa sabuni hii una njia nyingi Hatua  ya kwanza Chemsha vipimo 7 vya mafuta ya mawese au mafuta ya shea hadi ifikie hatua ya kimiminika chuja na yaweke kwenye chungu cha mfinyanzi au chombo cha plastiki. Hatua ya pili Pima vipimo 5 vya maji baridi kwenye chombo cha plastiki ongeza kipimo 1cha sodium hydroxide kwa uangalifu mkubwa kwenye maji acha hadi mchanganyiko huo uyeyuke. Subiri mchanganyiko wa sodium hydroxide na mafuta ukaribie kupoa. Hatua ya tatu Taratibu ongeza mchanganyiko wa sodium hydroxide kwenye mawese,huku ukikoroga haraka haraka bila kusitisha ukitumia ubao .hii ni njia nzuri zaidi. Njia ya pili Chemsha mafuta kwenye joto la kadiri ya 55C Changanya maji na sodium hydroxide na uache mchanganyiko huu upoe hadi kufikia joto hilohilo. Baada ya kuandaa mchanyiko wako changanya vimiminika hivyo viwili huku ukikoroga kwanguvu sana kadiri uwezavyo, taratibu sabuni itageuka kuwa laini. Kabla...