Skip to main content

Aingia matatani baada ya kupulizia wenzake kemikali usoni

Aingia matatani baada ya kupulizia wenzake kemikali usoni


MADALALI wanne wa madini ya Tanzanite (mawe), wanashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kuwaumiza macho kwa kemikali aina ya ‘pepper spray’ baada ya kutofautiana malipo na madalali wenzao waliowauzia madini hayo.

Habari kutoka polisi zilithibitisha jana kuwashikilia madalali hao, Schola Mwanga, Margareth Mushi, Sued Mwanga na Dorice Mushi, kwa tuhuma za kufanya kitendo hicho.

Hata hivyo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Charles Mkumbo hakuweza kupatikana kutoa ufafanuzi zaidi.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufani ya Mkoa ya Mount Meru, Dk. Jackline Urio, alithibitisha kupokea wagonjwa watano ambao alisema uchunguzi unaendelea kujua walimwagiwa aina gani ya kemikali.

Alisema kutokana na hali zao, wagonjwa hao walitarajiwa kuhamishiwa Hospitali ya Rufani ya KCMC ya mkoani Kilimanjaro, jana.

Alisema waliojeruhiwa walikuwa katika biashara ya madini na wakaletwa hapa wakilalamika macho yanauma, wakapewa huduma ya kwanza ya kuwaosha macho kwa kushauriana na madaktari bingwa wa macho wa Dar es Salaam.

Aliwataja wagonjwa hao kuwa ni Sabas Laizer, Lucas Soto, George Nyakila, Moringe Mollel na Ngalama Mapena.

Alisema watu hao walidai kumwagiwa ‘spray’ kwenye macho, majira ya saa 10 na walianza kufikishwa hospitalini hapo mmoja mmoja kuanzia saa 12 jioni.

"Lakini kwa sasa tunawahamishia hospitali ya KCMC kwa sababu kule kuna madaktari bingwa wa macho, watachunguzwa vizuri kujua madhara waliyopata," alisema.

Wakizungumzia tukio hilo lililotokea mtaa wa Pangani jijini hapa, baadhi ya watu walioshuhudia, walidai madalali hao walitaka walipwe fedha (kamisheni) ya kuwauzia mawe hayo.

Lakili walisema madalali waliopewa mawe hayo kuuza walishindwa kuwapa fedha hizo kwa kile walichodai walikuwa bado hawajalipwa.

Walisema hali hiyo ilizua kutoelewana kati yao kiasi cha kuzua ugomvi na ndipo dalali mmoja alipoingia ndani ya gari na kuchukua ‘pepper spray’ na kuwapulizia usoni.

“Pepper spray’ ni aina ya kemikali inayowekwa katika kopo maalum mithili ya dawa ya mbu na ikipulizwa usoni kwa mtu inaumiza macho yake na kuyafanya yasione kwa muda.

Katibu wa Chama cha Madakali mkoani hapa, Noel Olovaroya, alisema tukio hilo lilitokea baada ya kutofautiana katika masuala ya biashara.

Alishukuru daktari bingwa wa hospitali hiyo kwa kuwashughulikia vizuri wagonjwa hao na kuomba serikali kuongeza madaktari wa macho katika hospitali hiyo.

Akizungumza kwa niaba ya madalali wenzake, waliojeruhiwa, Ngalama Mapena ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Madalali wa Madini, alisema chanzo cha tukio hilo ni yeye aliuziwa madini ya Tanzanite na dalali mmoja kwa Sh milioni 3.2 na makubaliano yalikuwa angemlipa kesho yake (juzi)  ambayo ndio siku ya tukio.

"Lakini nikiwa pale baada ya kujibu hivyo nikaona gari RAV 4 rangi nyeusi, wakashuka wanawake wawili ambapo mmoja namfahamu akanipulizia kitu kama perfume usoni na huku akitukana na ghafla nikapoteza fahamu," alisema.
Alisema mwanamke huyo ni dalali mwenzake.

Popular posts from this blog

Jinsi Wachawi Wanavyo Tumia Mafiga Mabichi Ya Mti Wa Mfausiku Kupika Uchawi Wa Kumvuta Kimapenzi Mtu Aliye Mbali.

Jinsi Wachawi Wanavyo Tumia Mafiga Mabichi Ya Mti Wa Mfausiku Kupika Uchawi Wa Kumvuta Kimapenzi Mtu Aliye Mbali. Na. DOKTA  MUNGWA  KABILI …0744 -000  473.  Wachawi  wanaweza  kutumia  uchawi  kumvuta  kimapenzi  mtu  aliye  mbali. Moja  kati  ya  vitu  vinavyo  tumika  katika  uchawi  huu  ni  pamoja  na  mafiga  mabichi  ya  mti  wa  mfausiku  ambayo  hukokwa  kwenye  majani  makavu ya  mgomba  ambayo  hutumika  kama  kuni  au  moto,  kipande  cha  sanda  alichovalishwa  maiti, herufi za  moto,  mti wa hina, pamoja na  vitu  vingine  lukuki. Kufahamu  kuhusu  uchawi wa aina  hii  na  jinsi  ya  kujikinga  nao, fuatilia  sehemu  ya  nne  ya  kitabu “ KITANDA  CHA  SOKWE  MTU” kama  ifuatavyo : SEHEMU  YA  PILI   YA  KITABU  “ KITANDA  CHA  SOKWE  MTU “ Wachawi   wakishindwa  kukutengenezea  kesi  kubwa  basi  waatakufunga  kwenye  kifungo  cha  mapenzi.  Katika  vifungo  vyote anavyo  fungwa  mwanadamu  hakuna  kifungo  kibaya  kama  kifungo  cha  mape

Faida nyingine za kula chungwa

Faida nyingine za kula chungwa Siku kadhaa zilizopita tuliangalia kwa uchache kuhusu faida za kula chungwa hivyo, pia siku ya leo naomba tuendelee kwa kuangalia faida nyingine za kula chungwa. 1. Ulaji wa machungwa husaidia kutibu mapafu. Chungwa pia lina kiasi kikubwa cha Vitamin B6 na Madini ya Chuma (iron), virubisho ambavyo ni muhimu kwa uzalishaji wa seli nyekundu za damu, ambazo hufanya kazi ya kusafirisha hewa ya oksjeni mwilini, hivyo kuwa muhimu kwa kujikinga na ugonjwa wa mapafu. 2. Husaidia kuimarisha mifupa ya meno. Chungwa lina kiasi kingi cha madini ya kalisi (calcium) ambayo ni muhimu kwa uimarishaji wa mifupa na meno. 3. Husaidia kupunguza kiwango cha mafuta mwilini. Virutubisho vilivyomo kwenye chungwa, hasa kwenye maganda yake, hupunguza kiwango cha mafuta mabaya mwilini (bad cholesterol). Hivyo kwa wenye tatizo la lehemu wanashauriwa kula machungwa pamoja na nyama zake. 4. Hupunguza kupatwa magonjwa wa figo. Ulaji wa machungwa mara kwa mara, ukusaid

Je, unajua Binadamu anatakiwa kulala masaa mangapi?

Je, unajua Binadamu anatakiwa kulala masaa mangapi? Unafikili ni wazo zuri kuamka  saa 11 za asubuhi na kufanya mazoezi? Je, ingekuwa vipi kama ungetumia muda huo kulala? Wataalamu wa afya wanashauri kuwa binadamu kwa kwaida anapaswa kulala angalau masaa 7 wakati wa usiku ili kuupa mwili afya bora. Kulala kwa muda mfupi au masaa machache husababisha matatizo ya afya, ikiwa ni pamoja na shinikizo la damu, unyogovu, ugonjwa wa kisukari, na kupunguzwa kinga kukabiliana na chanjo. Ni vyema ukatumia muda wako vizuri mchana ili usiku ukapata muda mwafaka wa kuweza kuupumzisha mwili ili kuepukana na magonjwa hatari ya shinikizo la damu, kisukari na kupungua kwa kinga mwilini. Najua mazingira yetu waafrika ya kimaisha wakati mwingine yanachangamoto nyingi, lakini pale upatapo mwanya kidogo tu, basi utumie yani "kila penye tundu, penyeza lupia" au wawenzetu wazungu wanasema "one chance two goals".