Skip to main content

Aingia matatani baada ya kupulizia wenzake kemikali usoni

Aingia matatani baada ya kupulizia wenzake kemikali usoni


MADALALI wanne wa madini ya Tanzanite (mawe), wanashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kuwaumiza macho kwa kemikali aina ya ‘pepper spray’ baada ya kutofautiana malipo na madalali wenzao waliowauzia madini hayo.

Habari kutoka polisi zilithibitisha jana kuwashikilia madalali hao, Schola Mwanga, Margareth Mushi, Sued Mwanga na Dorice Mushi, kwa tuhuma za kufanya kitendo hicho.

Hata hivyo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Charles Mkumbo hakuweza kupatikana kutoa ufafanuzi zaidi.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufani ya Mkoa ya Mount Meru, Dk. Jackline Urio, alithibitisha kupokea wagonjwa watano ambao alisema uchunguzi unaendelea kujua walimwagiwa aina gani ya kemikali.

Alisema kutokana na hali zao, wagonjwa hao walitarajiwa kuhamishiwa Hospitali ya Rufani ya KCMC ya mkoani Kilimanjaro, jana.

Alisema waliojeruhiwa walikuwa katika biashara ya madini na wakaletwa hapa wakilalamika macho yanauma, wakapewa huduma ya kwanza ya kuwaosha macho kwa kushauriana na madaktari bingwa wa macho wa Dar es Salaam.

Aliwataja wagonjwa hao kuwa ni Sabas Laizer, Lucas Soto, George Nyakila, Moringe Mollel na Ngalama Mapena.

Alisema watu hao walidai kumwagiwa ‘spray’ kwenye macho, majira ya saa 10 na walianza kufikishwa hospitalini hapo mmoja mmoja kuanzia saa 12 jioni.

"Lakini kwa sasa tunawahamishia hospitali ya KCMC kwa sababu kule kuna madaktari bingwa wa macho, watachunguzwa vizuri kujua madhara waliyopata," alisema.

Wakizungumzia tukio hilo lililotokea mtaa wa Pangani jijini hapa, baadhi ya watu walioshuhudia, walidai madalali hao walitaka walipwe fedha (kamisheni) ya kuwauzia mawe hayo.

Lakili walisema madalali waliopewa mawe hayo kuuza walishindwa kuwapa fedha hizo kwa kile walichodai walikuwa bado hawajalipwa.

Walisema hali hiyo ilizua kutoelewana kati yao kiasi cha kuzua ugomvi na ndipo dalali mmoja alipoingia ndani ya gari na kuchukua ‘pepper spray’ na kuwapulizia usoni.

“Pepper spray’ ni aina ya kemikali inayowekwa katika kopo maalum mithili ya dawa ya mbu na ikipulizwa usoni kwa mtu inaumiza macho yake na kuyafanya yasione kwa muda.

Katibu wa Chama cha Madakali mkoani hapa, Noel Olovaroya, alisema tukio hilo lilitokea baada ya kutofautiana katika masuala ya biashara.

Alishukuru daktari bingwa wa hospitali hiyo kwa kuwashughulikia vizuri wagonjwa hao na kuomba serikali kuongeza madaktari wa macho katika hospitali hiyo.

Akizungumza kwa niaba ya madalali wenzake, waliojeruhiwa, Ngalama Mapena ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Madalali wa Madini, alisema chanzo cha tukio hilo ni yeye aliuziwa madini ya Tanzanite na dalali mmoja kwa Sh milioni 3.2 na makubaliano yalikuwa angemlipa kesho yake (juzi)  ambayo ndio siku ya tukio.

"Lakini nikiwa pale baada ya kujibu hivyo nikaona gari RAV 4 rangi nyeusi, wakashuka wanawake wawili ambapo mmoja namfahamu akanipulizia kitu kama perfume usoni na huku akitukana na ghafla nikapoteza fahamu," alisema.
Alisema mwanamke huyo ni dalali mwenzake.

Popular posts from this blog

Jinsi ya kutengeneza SABUNI ya kipande YA KUGANDISHA

Jinsi ya kutengeneza SABUNI ya kipande YA KUGANDISHA Utengenezaji wa sabuni hii una njia nyingi Hatua  ya kwanza Chemsha vipimo 7 vya mafuta ya mawese au mafuta ya shea hadi ifikie hatua ya kimiminika chuja na yaweke kwenye chungu cha mfinyanzi au chombo cha plastiki. Hatua ya pili Pima vipimo 5 vya maji baridi kwenye chombo cha plastiki ongeza kipimo 1cha sodium hydroxide kwa uangalifu mkubwa kwenye maji acha hadi mchanganyiko huo uyeyuke. Subiri mchanganyiko wa sodium hydroxide na mafuta ukaribie kupoa. Hatua ya tatu Taratibu ongeza mchanganyiko wa sodium hydroxide kwenye mawese,huku ukikoroga haraka haraka bila kusitisha ukitumia ubao .hii ni njia nzuri zaidi. Njia ya pili Chemsha mafuta kwenye joto la kadiri ya 55C Changanya maji na sodium hydroxide na uache mchanganyiko huu upoe hadi kufikia joto hilohilo. Baada ya kuandaa mchanyiko wako changanya vimiminika hivyo viwili huku ukikoroga kwanguvu sana kadiri uwezavyo, taratibu sabuni itageuka kuwa laini. Kabla...

Mkuu wa Majeshi mstaafu (CDF), Jenerali George Waitara akemea uwindaji haramu Tarime

Mkuu wa Majeshi mstaafu (CDF), Jenerali George Waitara akemea uwindaji haramu Tarime MWENYEKITI wa Bodi ya Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), Mkuu wa Majeshi mstaafu (CDF), Jenerali George Waitara, amewataka wanachi wilayani Tarime, kuachana na uwindaji haramu, badala yake watumie fursa zilizopo kukuza vipato vyao iii kuondokana na umasikini katika ngazi ya familia.  Pia, amewataka wananchi hao watumie fursa hizo kuwekeza katika miradi na biashara mbalimbali katika maeneo jirani na Hifadhi ya Mbuga ya Serengeti, itakayowawezesha kuwaingizia vipato.  Waitara alitoa wito huo mjini Tarime, juzi, alipokutana na baadhi ya wananchi na kubadilishana nao mawazo, wakati akielekea nyumbani kwake k ij iji cha  Itiry o   kusherekea sikukuu ya Pasaka.  Alitoa ushauri kwa watu wenye nia ya kuwekeza katika miradi mbalimbali ya uzalishaji mali wilayani humo, watumie nafasi hiyo iii kukuza na kuendeleza mji waTarime na wilaya hiyo kwa ...

SADC YALIPONGEZA BARAZA LA USALAMA LA UN KWA KUONGEZA MUDA KWA MISHENI YA ULINZI DRC

SADC YALIPONGEZA BARAZA LA USALAMA LA UN KWA KUONGEZA MUDA KWA MISHENI YA ULINZI DRC 1 2 3 4 5 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) kuhusu mkutano wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa uliofanyika New York, Marekani na kupitisha Azimio la kuongeza muda kwa vikosi vya usalama vilivyopo DRC. Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy. Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza Mhe. Mahiga (hayupo pichani). Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mwenyekiti wa Kamati ya Mawaziri ya Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (Mb). akihutubia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa Jijini New York, Marekani. TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ambaye pia ni Mwenyekiti wa...