Skip to main content

Mama, watoto wamwagiwa tindikali

Mama, watoto wamwagiwa tindikali


KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA, MOHAMED MPINGA.

VUMILIA Shengema (31) na watoto wake wawili wamemwagiwa tindikali wakati wakitokea dukani kwa kile kinachodaiwa ni wivu wa mapenzi.

Kutokana na tukio hilo, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya, linamsaka mtuhumiwa huyo, Emmy Kyando (40, mkazi wa Sai jijini Mbeya ambaye aliwafanyia kitendo hicho cha kinyama watu hao.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Mohamed Mpinga, aliwataja wengine waliomwagiwa tindikali kuwa ni Loveness John (11), mwanafunzi wa darasa la sita katika Shule ya Msingi Sinde na  Nancy Peter (5), wakazi wa Mtaa wa Mwanshinga, Kata ya Manga jijini Mbeya.

Walimwagiwa na kujeruhiwa na tindikali hiyo usoni, kifuani na mikononi Julai 19, mwaka huu saa tatu usiku.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mpinga alisema Emmy anadaiwa  kufanya kitendo hicho kutokana na wivu wa kimapenzi kwa kuwa ni mke mwenza  wa mwathirika.

Mpinga alifafanua kuwa baada ya mtuhumiwa kufanya kitendo hicho alikimbia  kusikojulikana na wasamaria wema waliwakuta waathirika wakiwa katika hali mbaya na kuwapeleka katika Hospitali ya Rufani ya Mbeya kwa ajili ya kupata matibabu.

Kamanda Mpinga alieleza kuwa juhudi za kumtafuta mtuhumiwa  kwa kushirikiana na mume wa muathirika huyo  aliyefahamika kwa jina la Lausi Kidagile ambaye naye ni mkazi wa Sae zinaendelea.

 “Jeshi la Polisi linalaani vikali kitendo hicho na tunaomba mwananchi yeyote mwenye taarifa zitakazofanikisha  kumkamata mtuhumiwa atupatie ili hatua za kisheria zichukuliwe,” alisema Kamanda Mpinga.

Akizungumza na Nipashe kwa taabu akiwa wadi namba mbili katika Hospitali ya Rufani Kanda ya Mbeya, muathirika wa tukio hilo, Vumilia Shangema, alisema mtuhumiwa alikuwa akimtolea lugha za vitisho mara kwa mara na aliahidi kuwa kuna siku atamjeruhi.

 “Nikiwa njiani  na wanangu ghafla nikaona mwanamke mmoja niliyemfahamu kwa jina la Emmy akinimwagia kitu usoni na sikuweza kuona tena, lakini nikakumbuka kuwa Emmy  aliwahi kuniambia kuwa atanifanyizia huku akinitolea vitisho vikali vilivyotishia usalama wa maisha yangu,” alisema  Shangema.

Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufani Kanda ya Mbeya, Goodlove Mbwanji, alithibitisha kuwapokea wagonjwa katika hali mbaya hususani mama wa watoto Shangema, akiwa ameharibika usoni na macho kutokuona kabisa huku mtoto Loveness akiendelea kupata matibabu na afya yake kuimarika pamoja na Nancy ambaye alitibiwa na kuruhusiwa.

Mbwanji alisema wanaendelea na matibabu kwa mama huyo na kwamba idara ya upasuaji pamoja na madaktari wengine bingwa wamemuwekea uangalizi mzuri ili apate matibabu stahiki.

Popular posts from this blog

Jinsi Wachawi Wanavyo Tumia Mafiga Mabichi Ya Mti Wa Mfausiku Kupika Uchawi Wa Kumvuta Kimapenzi Mtu Aliye Mbali.

Jinsi Wachawi Wanavyo Tumia Mafiga Mabichi Ya Mti Wa Mfausiku Kupika Uchawi Wa Kumvuta Kimapenzi Mtu Aliye Mbali. Na. DOKTA  MUNGWA  KABILI …0744 -000  473.  Wachawi  wanaweza  kutumia  uchawi  kumvuta  kimapenzi  mtu  aliye  mbali. Moja  kati  ya  vitu  vinavyo  tumika  katika  uchawi  huu  ni  pamoja  na  mafiga  mabichi  ya  mti  wa  mfausiku  ambayo  hukokwa  kwenye  majani  makavu ya  mgomba  ambayo  hutumika  kama  kuni  au  moto,  kipande  cha  sanda  alichovalishwa  maiti, herufi za  moto,  mti wa hina, pamoja na  vitu  vingine  lukuki. Kufahamu  kuhusu  uchawi wa aina  hii  na  jinsi  ya  kujikinga  nao, fuatilia  sehemu  ya  nne  ya  kitabu “ KITANDA  CHA  SOKWE  MTU” kama  ifuatavyo : SEHEMU  YA  PILI   YA  KITABU  “ KITANDA  CHA  SOKWE  MTU “ Wachawi   wakishindwa  kukutengenezea  kesi  kubwa  basi  waatakufunga  kwenye  kifungo  cha  mapenzi.  Katika  vifungo  vyote anavyo  fungwa  mwanadamu  hakuna  kifungo  kibaya  kama  kifungo  cha  mape

Faida nyingine za kula chungwa

Faida nyingine za kula chungwa Siku kadhaa zilizopita tuliangalia kwa uchache kuhusu faida za kula chungwa hivyo, pia siku ya leo naomba tuendelee kwa kuangalia faida nyingine za kula chungwa. 1. Ulaji wa machungwa husaidia kutibu mapafu. Chungwa pia lina kiasi kikubwa cha Vitamin B6 na Madini ya Chuma (iron), virubisho ambavyo ni muhimu kwa uzalishaji wa seli nyekundu za damu, ambazo hufanya kazi ya kusafirisha hewa ya oksjeni mwilini, hivyo kuwa muhimu kwa kujikinga na ugonjwa wa mapafu. 2. Husaidia kuimarisha mifupa ya meno. Chungwa lina kiasi kingi cha madini ya kalisi (calcium) ambayo ni muhimu kwa uimarishaji wa mifupa na meno. 3. Husaidia kupunguza kiwango cha mafuta mwilini. Virutubisho vilivyomo kwenye chungwa, hasa kwenye maganda yake, hupunguza kiwango cha mafuta mabaya mwilini (bad cholesterol). Hivyo kwa wenye tatizo la lehemu wanashauriwa kula machungwa pamoja na nyama zake. 4. Hupunguza kupatwa magonjwa wa figo. Ulaji wa machungwa mara kwa mara, ukusaid

Je, unajua Binadamu anatakiwa kulala masaa mangapi?

Je, unajua Binadamu anatakiwa kulala masaa mangapi? Unafikili ni wazo zuri kuamka  saa 11 za asubuhi na kufanya mazoezi? Je, ingekuwa vipi kama ungetumia muda huo kulala? Wataalamu wa afya wanashauri kuwa binadamu kwa kwaida anapaswa kulala angalau masaa 7 wakati wa usiku ili kuupa mwili afya bora. Kulala kwa muda mfupi au masaa machache husababisha matatizo ya afya, ikiwa ni pamoja na shinikizo la damu, unyogovu, ugonjwa wa kisukari, na kupunguzwa kinga kukabiliana na chanjo. Ni vyema ukatumia muda wako vizuri mchana ili usiku ukapata muda mwafaka wa kuweza kuupumzisha mwili ili kuepukana na magonjwa hatari ya shinikizo la damu, kisukari na kupungua kwa kinga mwilini. Najua mazingira yetu waafrika ya kimaisha wakati mwingine yanachangamoto nyingi, lakini pale upatapo mwanya kidogo tu, basi utumie yani "kila penye tundu, penyeza lupia" au wawenzetu wazungu wanasema "one chance two goals".