Skip to main content

Mama, watoto wamwagiwa tindikali

Mama, watoto wamwagiwa tindikali


KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA, MOHAMED MPINGA.

VUMILIA Shengema (31) na watoto wake wawili wamemwagiwa tindikali wakati wakitokea dukani kwa kile kinachodaiwa ni wivu wa mapenzi.

Kutokana na tukio hilo, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya, linamsaka mtuhumiwa huyo, Emmy Kyando (40, mkazi wa Sai jijini Mbeya ambaye aliwafanyia kitendo hicho cha kinyama watu hao.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Mohamed Mpinga, aliwataja wengine waliomwagiwa tindikali kuwa ni Loveness John (11), mwanafunzi wa darasa la sita katika Shule ya Msingi Sinde na  Nancy Peter (5), wakazi wa Mtaa wa Mwanshinga, Kata ya Manga jijini Mbeya.

Walimwagiwa na kujeruhiwa na tindikali hiyo usoni, kifuani na mikononi Julai 19, mwaka huu saa tatu usiku.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mpinga alisema Emmy anadaiwa  kufanya kitendo hicho kutokana na wivu wa kimapenzi kwa kuwa ni mke mwenza  wa mwathirika.

Mpinga alifafanua kuwa baada ya mtuhumiwa kufanya kitendo hicho alikimbia  kusikojulikana na wasamaria wema waliwakuta waathirika wakiwa katika hali mbaya na kuwapeleka katika Hospitali ya Rufani ya Mbeya kwa ajili ya kupata matibabu.

Kamanda Mpinga alieleza kuwa juhudi za kumtafuta mtuhumiwa  kwa kushirikiana na mume wa muathirika huyo  aliyefahamika kwa jina la Lausi Kidagile ambaye naye ni mkazi wa Sae zinaendelea.

 “Jeshi la Polisi linalaani vikali kitendo hicho na tunaomba mwananchi yeyote mwenye taarifa zitakazofanikisha  kumkamata mtuhumiwa atupatie ili hatua za kisheria zichukuliwe,” alisema Kamanda Mpinga.

Akizungumza na Nipashe kwa taabu akiwa wadi namba mbili katika Hospitali ya Rufani Kanda ya Mbeya, muathirika wa tukio hilo, Vumilia Shangema, alisema mtuhumiwa alikuwa akimtolea lugha za vitisho mara kwa mara na aliahidi kuwa kuna siku atamjeruhi.

 “Nikiwa njiani  na wanangu ghafla nikaona mwanamke mmoja niliyemfahamu kwa jina la Emmy akinimwagia kitu usoni na sikuweza kuona tena, lakini nikakumbuka kuwa Emmy  aliwahi kuniambia kuwa atanifanyizia huku akinitolea vitisho vikali vilivyotishia usalama wa maisha yangu,” alisema  Shangema.

Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufani Kanda ya Mbeya, Goodlove Mbwanji, alithibitisha kuwapokea wagonjwa katika hali mbaya hususani mama wa watoto Shangema, akiwa ameharibika usoni na macho kutokuona kabisa huku mtoto Loveness akiendelea kupata matibabu na afya yake kuimarika pamoja na Nancy ambaye alitibiwa na kuruhusiwa.

Mbwanji alisema wanaendelea na matibabu kwa mama huyo na kwamba idara ya upasuaji pamoja na madaktari wengine bingwa wamemuwekea uangalizi mzuri ili apate matibabu stahiki.

Popular posts from this blog

Jinsi ya kutengeneza SABUNI ya kipande YA KUGANDISHA

Jinsi ya kutengeneza SABUNI ya kipande YA KUGANDISHA Utengenezaji wa sabuni hii una njia nyingi Hatua  ya kwanza Chemsha vipimo 7 vya mafuta ya mawese au mafuta ya shea hadi ifikie hatua ya kimiminika chuja na yaweke kwenye chungu cha mfinyanzi au chombo cha plastiki. Hatua ya pili Pima vipimo 5 vya maji baridi kwenye chombo cha plastiki ongeza kipimo 1cha sodium hydroxide kwa uangalifu mkubwa kwenye maji acha hadi mchanganyiko huo uyeyuke. Subiri mchanganyiko wa sodium hydroxide na mafuta ukaribie kupoa. Hatua ya tatu Taratibu ongeza mchanganyiko wa sodium hydroxide kwenye mawese,huku ukikoroga haraka haraka bila kusitisha ukitumia ubao .hii ni njia nzuri zaidi. Njia ya pili Chemsha mafuta kwenye joto la kadiri ya 55C Changanya maji na sodium hydroxide na uache mchanganyiko huu upoe hadi kufikia joto hilohilo. Baada ya kuandaa mchanyiko wako changanya vimiminika hivyo viwili huku ukikoroga kwanguvu sana kadiri uwezavyo, taratibu sabuni itageuka kuwa laini. Kabla...

Mkuu wa Majeshi mstaafu (CDF), Jenerali George Waitara akemea uwindaji haramu Tarime

Mkuu wa Majeshi mstaafu (CDF), Jenerali George Waitara akemea uwindaji haramu Tarime MWENYEKITI wa Bodi ya Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), Mkuu wa Majeshi mstaafu (CDF), Jenerali George Waitara, amewataka wanachi wilayani Tarime, kuachana na uwindaji haramu, badala yake watumie fursa zilizopo kukuza vipato vyao iii kuondokana na umasikini katika ngazi ya familia.  Pia, amewataka wananchi hao watumie fursa hizo kuwekeza katika miradi na biashara mbalimbali katika maeneo jirani na Hifadhi ya Mbuga ya Serengeti, itakayowawezesha kuwaingizia vipato.  Waitara alitoa wito huo mjini Tarime, juzi, alipokutana na baadhi ya wananchi na kubadilishana nao mawazo, wakati akielekea nyumbani kwake k ij iji cha  Itiry o   kusherekea sikukuu ya Pasaka.  Alitoa ushauri kwa watu wenye nia ya kuwekeza katika miradi mbalimbali ya uzalishaji mali wilayani humo, watumie nafasi hiyo iii kukuza na kuendeleza mji waTarime na wilaya hiyo kwa ...

Bei ya unga sasa ni mara 12 ya mfuko wa Simenti

Bei ya unga sasa ni mara 12 ya mfuko wa Simenti WAKATI bei ya unga wa sembe ikipanda mpaka kufikia kuuzwa kati ya Sh. 2,200 na Sh. 2,500 kwa kilo, ile ya mfuko wa saruji wenye uzito wa kilo 50 imeshuka hadi sh. 9,000, sawa na Sh. 180 kwa kilo. Katika masoko na maduka mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam ambayo Nipashe ilitembelea jana, bei ya sembe ilikuwa ikiuzwa kwa kiasi hicho kwa rejareja huku wauzaji wa jumla wakiuza kiroba cha kilo 50 kwa kati ya sh.100,000 na sh.98,000. Ibrahim Omary, mfanyabiashara wa Kariakoo alisema anauza unga wa sembe kwa Sh. 2,400 kwa kuwa hununua kwa bei kubwa kutoka kwa wazalishaji. Alisema kampuni inayojulikana kwa jina la Mkulima huwauzia unga huo kwa Sh. 98,000 na Mama Neema huwauzia kwa sh. 100,000 kwa kiroba cha kilo 50. Kwenye baadhi ya maduka ya kula ya Kinondoni, unga umekuwa ukiuzwa kati ya Sh. 2,200 na Sh. 2,500. Tandika bei ya wastani ni Sh. 2,200, Mwenge Sh. 2,400, Kimara sh. 2,500 na Yombo Vituka sh. 2,200. ...