Skip to main content

Okwi ananuka fedha

Okwi ananuka fedha


 Mshambuliaji wa Simba, Emmanuel Okwi.

KUANZIA leo Jumatano, zitakuwa zimebaki takribani siku 11 kabla ya usajili wa dirisha kubwa Tanzania Bara halijafungwa ambapo timu kadhaa zimekuwa zikiimarisha vikosi vyao. Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limetoa siku 52 kwa timu za Ligi Kuu Bara, Ligi Daraja la Kwanza na Ligi Daraja la Pili kujenga vikosi vyao kwa kufanya usajili kuanzia Juni 15 mpaka Agosti 6, mwaka huu.

Tangu kufunguliwa kwa dirisha hilo, kumekuwa na vurugu kwa wachezaji kuhama timu moja kwenda nyingine huku tukishuhudia baadhi ya timu zikigombania mchezaji mmoja na kila upande ikihitaji saini yake. Katika vurugu hizo, kuna wachezaji wamesajili kwa madau makubwa na kuwafanya kuwa wachezaji ghali katika soka la Bongo kwa sasa. Championi ambalo tangu siku ya kwanza ya usajili limekuwa makini kufuatilia mchakato huo, linakuletea tathmini ya kile kilichofanyika mpaka sasa na kubainisha nani amesajili kwa mkwanja mrefu.

EMMANUEL OKWI
Mganda huyu mpaka sasa ndiye mchezaji aliyenunuliwa kwa dau kubwa akijiunga na Simba akitokea Villa ya Uganda, ambapo mpaka mchakato wake unakamilika wa kujiunga na timu hiyo amechota kiasi cha milioni 115. Fedha hizo zilizotolewa na Simba kumpa Okwi zinamfanya kuwa mchezaji ghali kwenye usajili huu.
 Haruna Niyonzima.

HARUNA NIYONZIMA
Bado mashabiki wa Yanga wanauguza donda la kuondokewa na nyota wao kipenzi, Haruna

Niyonzima ambaye ameikacha timu hiyo na kutua kwa wapinzani wao Simba kwa usajili uliowakosti dola 50 (sawa na milioni 115 za Kitanzania) ambapo fedha hizo zinamfanya aingie daraja moja na Okwi.

Mnyarwanda huyu nae ni mmoja wa wachezaji nyota ambao wamesajiliwa kwa dau kubwa katika dirisha hili la usajili akiwa sambamba na Mganda, Emmanuel Okwi.
Mshambuliaji mpya wa Yanga,Ibrahim Ajibu.

IBRAHIM AJIBU

Ndiye mchezaji ghali kwa upande wa wachezaji wa ndani ya nchi baada ya klabu ya Yanga kutumia milioni 70 kukamilisha mchakato wa kumtoa Simba na kumshusha kwenye kikosi chao. Ukimuondoa Okwi na Niyonzima, mshambuliaji huyu naye anafuata kwenye orodha ya wachezaji waliovuta mkwanja mnene kwenye kipindi hiki cha usajili.

ROSTAND YOUTHE

Ameletwa ndani ya Yanga kurithi mikoba ya makipa, Deogratius Munishi ‘Dida’ na Ally Mustapha ‘Barthez’ ambao kwa msimu ujao hawataonekana na kikosi hicho. Barthez ameenda Singida United na Dida yeye yupo kwenye hatua za kutua Afrika Kusini. Kipa huyu raia wa Cameroon naye hayupo mbali kwenye orodha ya wachezaji ghali kwenye msimu huu baada ya kusaini mkataba wa miaka miwili wa kuwatumikia mabingwa hao wa ligi kuu msimu uliopita baada ya kutia kibindoni milioni 40.

MBARAKA YUSUPH

Straika ambaye ameanza msimu mpya kwa majanga
bada ya kupigwa kisu ‘operesheni’ ambayo itamuweka nje kwa wiki sita ambapo muda huo utamfanya akose mechi za awali za timu yake mpya ya Azam. Mpaka usajili wake unakamilika wa kujiunga na kikosi hicho cha Wauza lambalamba, Mbaraka aliyepachika kambani mabao 12 msimu uliopita amevuna kiasi cha milioni 40.

SHOMARY KAPOMBE

Beki kisiki wa Azam, Shomary Kapombe kwa msimu ujao ataonekana akiwa ndani ya uzi wa Simba baada ya kukubali kujiunga na timu hiyo kwa mkataba wa miaka miwili. Kapombe naye ni miongoni mwa wachezaji ghali katika dirisha hili la usajili baada ya kutia kibindoni milioni 35 zilizofanikisha usajili wake kutua ndani ya timu hiyo. Wachezaji wengine ghali kwenye dirisha hili la usajili ni pamoja na kipa Aishi Manula (kutoka Azam kwenda Simba, milioni 35), kiraka, Erasto Nyoni (milioni 30), John Bocco (milioni 35) na kipa Emmanuel Mseja (aliyetoka Mbao kwenda Simba milioni 25).

Popular posts from this blog

Jinsi Wachawi Wanavyo Tumia Mafiga Mabichi Ya Mti Wa Mfausiku Kupika Uchawi Wa Kumvuta Kimapenzi Mtu Aliye Mbali.

Jinsi Wachawi Wanavyo Tumia Mafiga Mabichi Ya Mti Wa Mfausiku Kupika Uchawi Wa Kumvuta Kimapenzi Mtu Aliye Mbali. Na. DOKTA  MUNGWA  KABILI …0744 -000  473.  Wachawi  wanaweza  kutumia  uchawi  kumvuta  kimapenzi  mtu  aliye  mbali. Moja  kati  ya  vitu  vinavyo  tumika  katika  uchawi  huu  ni  pamoja  na  mafiga  mabichi  ya  mti  wa  mfausiku  ambayo  hukokwa  kwenye  majani  makavu ya  mgomba  ambayo  hutumika  kama  kuni  au  moto,  kipande  cha  sanda  alichovalishwa  maiti, herufi za  moto,  mti wa hina, pamoja na  vitu  vingine  lukuki. Kufahamu  kuhusu  uchawi wa aina  hii  na  jinsi  ya  kujikinga  nao, fuatilia  sehemu  ya  nne  ya  kitabu “ KITANDA  CHA  SOKWE  MTU” kama  ifuatavyo : SEHEMU  YA  PILI   YA  KITABU  “ KITANDA  CHA  SOKWE  MTU “ Wachawi   wakishindwa  kukutengenezea  kesi  kubwa  basi  waatakufunga  kwenye  kifungo  cha  mapenzi.  Katika  vifungo  vyote anavyo  fungwa  mwanadamu  hakuna  kifungo  kibaya  kama  kifungo  cha  mape

Faida nyingine za kula chungwa

Faida nyingine za kula chungwa Siku kadhaa zilizopita tuliangalia kwa uchache kuhusu faida za kula chungwa hivyo, pia siku ya leo naomba tuendelee kwa kuangalia faida nyingine za kula chungwa. 1. Ulaji wa machungwa husaidia kutibu mapafu. Chungwa pia lina kiasi kikubwa cha Vitamin B6 na Madini ya Chuma (iron), virubisho ambavyo ni muhimu kwa uzalishaji wa seli nyekundu za damu, ambazo hufanya kazi ya kusafirisha hewa ya oksjeni mwilini, hivyo kuwa muhimu kwa kujikinga na ugonjwa wa mapafu. 2. Husaidia kuimarisha mifupa ya meno. Chungwa lina kiasi kingi cha madini ya kalisi (calcium) ambayo ni muhimu kwa uimarishaji wa mifupa na meno. 3. Husaidia kupunguza kiwango cha mafuta mwilini. Virutubisho vilivyomo kwenye chungwa, hasa kwenye maganda yake, hupunguza kiwango cha mafuta mabaya mwilini (bad cholesterol). Hivyo kwa wenye tatizo la lehemu wanashauriwa kula machungwa pamoja na nyama zake. 4. Hupunguza kupatwa magonjwa wa figo. Ulaji wa machungwa mara kwa mara, ukusaid

Je, unajua Binadamu anatakiwa kulala masaa mangapi?

Je, unajua Binadamu anatakiwa kulala masaa mangapi? Unafikili ni wazo zuri kuamka  saa 11 za asubuhi na kufanya mazoezi? Je, ingekuwa vipi kama ungetumia muda huo kulala? Wataalamu wa afya wanashauri kuwa binadamu kwa kwaida anapaswa kulala angalau masaa 7 wakati wa usiku ili kuupa mwili afya bora. Kulala kwa muda mfupi au masaa machache husababisha matatizo ya afya, ikiwa ni pamoja na shinikizo la damu, unyogovu, ugonjwa wa kisukari, na kupunguzwa kinga kukabiliana na chanjo. Ni vyema ukatumia muda wako vizuri mchana ili usiku ukapata muda mwafaka wa kuweza kuupumzisha mwili ili kuepukana na magonjwa hatari ya shinikizo la damu, kisukari na kupungua kwa kinga mwilini. Najua mazingira yetu waafrika ya kimaisha wakati mwingine yanachangamoto nyingi, lakini pale upatapo mwanya kidogo tu, basi utumie yani "kila penye tundu, penyeza lupia" au wawenzetu wazungu wanasema "one chance two goals".