Skip to main content

Okwi ananuka fedha

Okwi ananuka fedha


 Mshambuliaji wa Simba, Emmanuel Okwi.

KUANZIA leo Jumatano, zitakuwa zimebaki takribani siku 11 kabla ya usajili wa dirisha kubwa Tanzania Bara halijafungwa ambapo timu kadhaa zimekuwa zikiimarisha vikosi vyao. Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limetoa siku 52 kwa timu za Ligi Kuu Bara, Ligi Daraja la Kwanza na Ligi Daraja la Pili kujenga vikosi vyao kwa kufanya usajili kuanzia Juni 15 mpaka Agosti 6, mwaka huu.

Tangu kufunguliwa kwa dirisha hilo, kumekuwa na vurugu kwa wachezaji kuhama timu moja kwenda nyingine huku tukishuhudia baadhi ya timu zikigombania mchezaji mmoja na kila upande ikihitaji saini yake. Katika vurugu hizo, kuna wachezaji wamesajili kwa madau makubwa na kuwafanya kuwa wachezaji ghali katika soka la Bongo kwa sasa. Championi ambalo tangu siku ya kwanza ya usajili limekuwa makini kufuatilia mchakato huo, linakuletea tathmini ya kile kilichofanyika mpaka sasa na kubainisha nani amesajili kwa mkwanja mrefu.

EMMANUEL OKWI
Mganda huyu mpaka sasa ndiye mchezaji aliyenunuliwa kwa dau kubwa akijiunga na Simba akitokea Villa ya Uganda, ambapo mpaka mchakato wake unakamilika wa kujiunga na timu hiyo amechota kiasi cha milioni 115. Fedha hizo zilizotolewa na Simba kumpa Okwi zinamfanya kuwa mchezaji ghali kwenye usajili huu.
 Haruna Niyonzima.

HARUNA NIYONZIMA
Bado mashabiki wa Yanga wanauguza donda la kuondokewa na nyota wao kipenzi, Haruna

Niyonzima ambaye ameikacha timu hiyo na kutua kwa wapinzani wao Simba kwa usajili uliowakosti dola 50 (sawa na milioni 115 za Kitanzania) ambapo fedha hizo zinamfanya aingie daraja moja na Okwi.

Mnyarwanda huyu nae ni mmoja wa wachezaji nyota ambao wamesajiliwa kwa dau kubwa katika dirisha hili la usajili akiwa sambamba na Mganda, Emmanuel Okwi.
Mshambuliaji mpya wa Yanga,Ibrahim Ajibu.

IBRAHIM AJIBU

Ndiye mchezaji ghali kwa upande wa wachezaji wa ndani ya nchi baada ya klabu ya Yanga kutumia milioni 70 kukamilisha mchakato wa kumtoa Simba na kumshusha kwenye kikosi chao. Ukimuondoa Okwi na Niyonzima, mshambuliaji huyu naye anafuata kwenye orodha ya wachezaji waliovuta mkwanja mnene kwenye kipindi hiki cha usajili.

ROSTAND YOUTHE

Ameletwa ndani ya Yanga kurithi mikoba ya makipa, Deogratius Munishi ‘Dida’ na Ally Mustapha ‘Barthez’ ambao kwa msimu ujao hawataonekana na kikosi hicho. Barthez ameenda Singida United na Dida yeye yupo kwenye hatua za kutua Afrika Kusini. Kipa huyu raia wa Cameroon naye hayupo mbali kwenye orodha ya wachezaji ghali kwenye msimu huu baada ya kusaini mkataba wa miaka miwili wa kuwatumikia mabingwa hao wa ligi kuu msimu uliopita baada ya kutia kibindoni milioni 40.

MBARAKA YUSUPH

Straika ambaye ameanza msimu mpya kwa majanga
bada ya kupigwa kisu ‘operesheni’ ambayo itamuweka nje kwa wiki sita ambapo muda huo utamfanya akose mechi za awali za timu yake mpya ya Azam. Mpaka usajili wake unakamilika wa kujiunga na kikosi hicho cha Wauza lambalamba, Mbaraka aliyepachika kambani mabao 12 msimu uliopita amevuna kiasi cha milioni 40.

SHOMARY KAPOMBE

Beki kisiki wa Azam, Shomary Kapombe kwa msimu ujao ataonekana akiwa ndani ya uzi wa Simba baada ya kukubali kujiunga na timu hiyo kwa mkataba wa miaka miwili. Kapombe naye ni miongoni mwa wachezaji ghali katika dirisha hili la usajili baada ya kutia kibindoni milioni 35 zilizofanikisha usajili wake kutua ndani ya timu hiyo. Wachezaji wengine ghali kwenye dirisha hili la usajili ni pamoja na kipa Aishi Manula (kutoka Azam kwenda Simba, milioni 35), kiraka, Erasto Nyoni (milioni 30), John Bocco (milioni 35) na kipa Emmanuel Mseja (aliyetoka Mbao kwenda Simba milioni 25).

Popular posts from this blog

Lema ahoji kushikiliwa mmiliki wa shule ya Lucky Vincent

Lema ahoji kushikiliwa mmiliki wa shule ya Lucky Vincent Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema   Dodoma. Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema amehoji sababu za polisi kumshikilia mmiliki wa shule ya Lucky Vincent badala ya trafiki waliokuwa barabarani siku ya ajali iliyoua watu 35. Akiomba mwongozo wa Spika kuhusu jambo hilo leo, amesema katika eneo husika kuna vizuizi vya ukaguzi vinne lakini trafiki hawakuona kuwa basi hilo lilikuwa kimezidisha watoto na hawakuwa wamefunga mikanda. Amesema badala ya trafiki hao kuchukuliwa hatua, anakamatwa mmiliki ambaye hakuwapo. Akijibu mwongozo huo, Naibu Spika, Dk Tulia Ackson amesema suala hilo halijatokea bungeni.

Bei ya unga sasa ni mara 12 ya mfuko wa Simenti

Bei ya unga sasa ni mara 12 ya mfuko wa Simenti WAKATI bei ya unga wa sembe ikipanda mpaka kufikia kuuzwa kati ya Sh. 2,200 na Sh. 2,500 kwa kilo, ile ya mfuko wa saruji wenye uzito wa kilo 50 imeshuka hadi sh. 9,000, sawa na Sh. 180 kwa kilo. Katika masoko na maduka mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam ambayo Nipashe ilitembelea jana, bei ya sembe ilikuwa ikiuzwa kwa kiasi hicho kwa rejareja huku wauzaji wa jumla wakiuza kiroba cha kilo 50 kwa kati ya sh.100,000 na sh.98,000. Ibrahim Omary, mfanyabiashara wa Kariakoo alisema anauza unga wa sembe kwa Sh. 2,400 kwa kuwa hununua kwa bei kubwa kutoka kwa wazalishaji. Alisema kampuni inayojulikana kwa jina la Mkulima huwauzia unga huo kwa Sh. 98,000 na Mama Neema huwauzia kwa sh. 100,000 kwa kiroba cha kilo 50. Kwenye baadhi ya maduka ya kula ya Kinondoni, unga umekuwa ukiuzwa kati ya Sh. 2,200 na Sh. 2,500. Tandika bei ya wastani ni Sh. 2,200, Mwenge Sh. 2,400, Kimara sh. 2,500 na Yombo Vituka sh. 2,200. ...

Jinsi ya kutengeneza SABUNI ya kipande YA KUGANDISHA

Jinsi ya kutengeneza SABUNI ya kipande YA KUGANDISHA Utengenezaji wa sabuni hii una njia nyingi Hatua  ya kwanza Chemsha vipimo 7 vya mafuta ya mawese au mafuta ya shea hadi ifikie hatua ya kimiminika chuja na yaweke kwenye chungu cha mfinyanzi au chombo cha plastiki. Hatua ya pili Pima vipimo 5 vya maji baridi kwenye chombo cha plastiki ongeza kipimo 1cha sodium hydroxide kwa uangalifu mkubwa kwenye maji acha hadi mchanganyiko huo uyeyuke. Subiri mchanganyiko wa sodium hydroxide na mafuta ukaribie kupoa. Hatua ya tatu Taratibu ongeza mchanganyiko wa sodium hydroxide kwenye mawese,huku ukikoroga haraka haraka bila kusitisha ukitumia ubao .hii ni njia nzuri zaidi. Njia ya pili Chemsha mafuta kwenye joto la kadiri ya 55C Changanya maji na sodium hydroxide na uache mchanganyiko huu upoe hadi kufikia joto hilohilo. Baada ya kuandaa mchanyiko wako changanya vimiminika hivyo viwili huku ukikoroga kwanguvu sana kadiri uwezavyo, taratibu sabuni itageuka kuwa laini. Kabla...