Skip to main content

Wauguzi kumnyima kura muhimu Kenyatta?

Wauguzi kumnyima kura muhimu Kenyatta?


Nairobi, Kenya. Chama cha Wauguzi Kenya (NNAK) kimejiingiza katika siasa za uchaguzi baada ya kutoa tishio la “kuiaibisha” serikali ya Jubilee kwa madai ya kukawiza majadiliano kuhusu mzozo wa malipo yao.

Wafanyakazi hao wa idara ya afya wanautazama uchaguzi uliopangwa Agosti 8 kama kete yao wakisema kurejeshwa tena mamlakani kwa Rais Uhuru Kenyatta kutakuwa hatarini ikiwa madai yao hayatatekelezwa kwa wakati.

Mwenyekiti wa NNAK, Alfred Obengo alisema: “Tutakuwa na uchaguzi Agosti na sisi tuko 40,000 huku mshindi anatakiwa kupata asilimia 50 jumlisha moja. Idadi yetu haiwezi kupuuzwa.”

Aliongeza: “Kwa hiyo wakati wewe (Rais Uhuru) unaendelea na kampeni, usifikiri hata wakati mmoja kwamba kura za wauguzi si muhimu.”

Waguzi walipiga kambi katika viwanja vya Uhuru Park kulalamikia ukimya wa serikali katika mpango wa malipo ambao wanadai walifikia makubaliano na mwajiri wao.

Walivamia ofisi za Tume ya Mishahara na Marupurupu (SRC) lakini haikusaidia kwani mwenyekiti wa tume hiyo Sarah Serem alisema alikuwa akisubiri mawasiliano kutoka kwa magavana.

Uhuru ahimiza kujitokeza

Naye akitambua tishio la kukosa kura 40,000 Rais Uhuru ameendelea kuwaambia wafuasi wake katika ngome zake muhimu kwamba matokeo ya uchaguzi wa Agosti 8 yataamuliwa na jinsi watakavyojitokeza kumpigia kura na si vinginevyo.

Rais aliwataka wasichezee suala hilo kamwe “kwa kuwa hali halisi ni kuwa mkijitokeza kwa wingi na mnipigie kura, basi huyu mtu wa kutusumbua (mpinzani wake Raila Odinga) kila uchao atakuwa amepata nauli ya kuelekea kwake nyumbani kustaafu.”

Akiwa  katika Kaunti ya Murang’a, Uhuru alisema kuwa “kile sitachoka kuwaambia ni kuwa, kwa wakati huu nawahitaji kwa dhati. Kwa unyenyekevu nawapa tahadhari kuwa mkinichezea mzaha na kura zenu, basi mambo yataishia kwa sisi kushindwa. Mkijitokeza kwa wingi, mambo yatakuwa kwa manufaa yetu.”

Sababu za kususa mdahalo
Kuhusu kutohudhuria kwake mdahalo wa wagombea urais, Uhuru alisema: “Ratiba yangu ya kampeni na ambayo niliwasilisha kwa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka haikuorodhesha mdahalo huo kama jukwaa langu la kampeni.”

Alisema kuwa hadi sasa haoni ni kwa nini kumezuka gumzo kuhusu kususia kwake mdahalo huo ilihali haoni ulikuwa kwa manufaa gani akijitokeze katika ukumbi kujibizana na huyo mtu ambaye kila saa amejawa na uhasama na propaganda dhidi ya serikali yake.

Alisema kuwa kura haziko kwenye runinga na midahalo bali ziko katika mikono ya Wakenya ambao haja yao ni kusaidiwa kujiinua kimaisha “siyo katika safu ya kupewa maneno matupu ya majadiliano.”

Kwingineko Rais Kenyatta alisema aliamua kutoshiriki mdahalo huo kwa kuwa ulikuwa upotevu wa muda.

Kenyatta alisema asingeweza kufanya mdahalo na “mtu ambaye hana agenda kwa nchi hii.”

Popular posts from this blog

Lema ahoji kushikiliwa mmiliki wa shule ya Lucky Vincent

Lema ahoji kushikiliwa mmiliki wa shule ya Lucky Vincent Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema   Dodoma. Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema amehoji sababu za polisi kumshikilia mmiliki wa shule ya Lucky Vincent badala ya trafiki waliokuwa barabarani siku ya ajali iliyoua watu 35. Akiomba mwongozo wa Spika kuhusu jambo hilo leo, amesema katika eneo husika kuna vizuizi vya ukaguzi vinne lakini trafiki hawakuona kuwa basi hilo lilikuwa kimezidisha watoto na hawakuwa wamefunga mikanda. Amesema badala ya trafiki hao kuchukuliwa hatua, anakamatwa mmiliki ambaye hakuwapo. Akijibu mwongozo huo, Naibu Spika, Dk Tulia Ackson amesema suala hilo halijatokea bungeni.

Jinsi Wachawi Wanavyo Tumia Mafiga Mabichi Ya Mti Wa Mfausiku Kupika Uchawi Wa Kumvuta Kimapenzi Mtu Aliye Mbali.

Jinsi Wachawi Wanavyo Tumia Mafiga Mabichi Ya Mti Wa Mfausiku Kupika Uchawi Wa Kumvuta Kimapenzi Mtu Aliye Mbali. Na. DOKTA  MUNGWA  KABILI …0744 -000  473.  Wachawi  wanaweza  kutumia  uchawi  kumvuta  kimapenzi  mtu  aliye  mbali. Moja  kati  ya  vitu  vinavyo  tumika  katika  uchawi  huu  ni  pamoja  na  mafiga  mabichi  ya  mti  wa  mfausiku  ambayo  hukokwa  kwenye  majani  makavu ya  mgomba  ambayo  hutumika  kama  kuni  au  moto,  kipande  cha  sanda  alichovalishwa  maiti, herufi za  moto,  mti wa hina, pamoja na  vitu  vingine  lukuki. Kufahamu  kuhusu  uchawi wa aina  hii  na  jinsi  ya  kujikinga  nao, fuatilia  sehemu  ya  nne  ya  kitabu “ ...

Bei ya unga sasa ni mara 12 ya mfuko wa Simenti

Bei ya unga sasa ni mara 12 ya mfuko wa Simenti WAKATI bei ya unga wa sembe ikipanda mpaka kufikia kuuzwa kati ya Sh. 2,200 na Sh. 2,500 kwa kilo, ile ya mfuko wa saruji wenye uzito wa kilo 50 imeshuka hadi sh. 9,000, sawa na Sh. 180 kwa kilo. Katika masoko na maduka mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam ambayo Nipashe ilitembelea jana, bei ya sembe ilikuwa ikiuzwa kwa kiasi hicho kwa rejareja huku wauzaji wa jumla wakiuza kiroba cha kilo 50 kwa kati ya sh.100,000 na sh.98,000. Ibrahim Omary, mfanyabiashara wa Kariakoo alisema anauza unga wa sembe kwa Sh. 2,400 kwa kuwa hununua kwa bei kubwa kutoka kwa wazalishaji. Alisema kampuni inayojulikana kwa jina la Mkulima huwauzia unga huo kwa Sh. 98,000 na Mama Neema huwauzia kwa sh. 100,000 kwa kiroba cha kilo 50. Kwenye baadhi ya maduka ya kula ya Kinondoni, unga umekuwa ukiuzwa kati ya Sh. 2,200 na Sh. 2,500. Tandika bei ya wastani ni Sh. 2,200, Mwenge Sh. 2,400, Kimara sh. 2,500 na Yombo Vituka sh. 2,200. ...