Skip to main content

Wauguzi kumnyima kura muhimu Kenyatta?

Wauguzi kumnyima kura muhimu Kenyatta?


Nairobi, Kenya. Chama cha Wauguzi Kenya (NNAK) kimejiingiza katika siasa za uchaguzi baada ya kutoa tishio la “kuiaibisha” serikali ya Jubilee kwa madai ya kukawiza majadiliano kuhusu mzozo wa malipo yao.

Wafanyakazi hao wa idara ya afya wanautazama uchaguzi uliopangwa Agosti 8 kama kete yao wakisema kurejeshwa tena mamlakani kwa Rais Uhuru Kenyatta kutakuwa hatarini ikiwa madai yao hayatatekelezwa kwa wakati.

Mwenyekiti wa NNAK, Alfred Obengo alisema: “Tutakuwa na uchaguzi Agosti na sisi tuko 40,000 huku mshindi anatakiwa kupata asilimia 50 jumlisha moja. Idadi yetu haiwezi kupuuzwa.”

Aliongeza: “Kwa hiyo wakati wewe (Rais Uhuru) unaendelea na kampeni, usifikiri hata wakati mmoja kwamba kura za wauguzi si muhimu.”

Waguzi walipiga kambi katika viwanja vya Uhuru Park kulalamikia ukimya wa serikali katika mpango wa malipo ambao wanadai walifikia makubaliano na mwajiri wao.

Walivamia ofisi za Tume ya Mishahara na Marupurupu (SRC) lakini haikusaidia kwani mwenyekiti wa tume hiyo Sarah Serem alisema alikuwa akisubiri mawasiliano kutoka kwa magavana.

Uhuru ahimiza kujitokeza

Naye akitambua tishio la kukosa kura 40,000 Rais Uhuru ameendelea kuwaambia wafuasi wake katika ngome zake muhimu kwamba matokeo ya uchaguzi wa Agosti 8 yataamuliwa na jinsi watakavyojitokeza kumpigia kura na si vinginevyo.

Rais aliwataka wasichezee suala hilo kamwe “kwa kuwa hali halisi ni kuwa mkijitokeza kwa wingi na mnipigie kura, basi huyu mtu wa kutusumbua (mpinzani wake Raila Odinga) kila uchao atakuwa amepata nauli ya kuelekea kwake nyumbani kustaafu.”

Akiwa  katika Kaunti ya Murang’a, Uhuru alisema kuwa “kile sitachoka kuwaambia ni kuwa, kwa wakati huu nawahitaji kwa dhati. Kwa unyenyekevu nawapa tahadhari kuwa mkinichezea mzaha na kura zenu, basi mambo yataishia kwa sisi kushindwa. Mkijitokeza kwa wingi, mambo yatakuwa kwa manufaa yetu.”

Sababu za kususa mdahalo
Kuhusu kutohudhuria kwake mdahalo wa wagombea urais, Uhuru alisema: “Ratiba yangu ya kampeni na ambayo niliwasilisha kwa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka haikuorodhesha mdahalo huo kama jukwaa langu la kampeni.”

Alisema kuwa hadi sasa haoni ni kwa nini kumezuka gumzo kuhusu kususia kwake mdahalo huo ilihali haoni ulikuwa kwa manufaa gani akijitokeze katika ukumbi kujibizana na huyo mtu ambaye kila saa amejawa na uhasama na propaganda dhidi ya serikali yake.

Alisema kuwa kura haziko kwenye runinga na midahalo bali ziko katika mikono ya Wakenya ambao haja yao ni kusaidiwa kujiinua kimaisha “siyo katika safu ya kupewa maneno matupu ya majadiliano.”

Kwingineko Rais Kenyatta alisema aliamua kutoshiriki mdahalo huo kwa kuwa ulikuwa upotevu wa muda.

Kenyatta alisema asingeweza kufanya mdahalo na “mtu ambaye hana agenda kwa nchi hii.”

Popular posts from this blog

Jinsi ya kutengeneza SABUNI ya kipande YA KUGANDISHA

Jinsi ya kutengeneza SABUNI ya kipande YA KUGANDISHA Utengenezaji wa sabuni hii una njia nyingi Hatua  ya kwanza Chemsha vipimo 7 vya mafuta ya mawese au mafuta ya shea hadi ifikie hatua ya kimiminika chuja na yaweke kwenye chungu cha mfinyanzi au chombo cha plastiki. Hatua ya pili Pima vipimo 5 vya maji baridi kwenye chombo cha plastiki ongeza kipimo 1cha sodium hydroxide kwa uangalifu mkubwa kwenye maji acha hadi mchanganyiko huo uyeyuke. Subiri mchanganyiko wa sodium hydroxide na mafuta ukaribie kupoa. Hatua ya tatu Taratibu ongeza mchanganyiko wa sodium hydroxide kwenye mawese,huku ukikoroga haraka haraka bila kusitisha ukitumia ubao .hii ni njia nzuri zaidi. Njia ya pili Chemsha mafuta kwenye joto la kadiri ya 55C Changanya maji na sodium hydroxide na uache mchanganyiko huu upoe hadi kufikia joto hilohilo. Baada ya kuandaa mchanyiko wako changanya vimiminika hivyo viwili huku ukikoroga kwanguvu sana kadiri uwezavyo, taratibu sabuni itageuka kuwa laini. Kabla...

Mkuu wa Majeshi mstaafu (CDF), Jenerali George Waitara akemea uwindaji haramu Tarime

Mkuu wa Majeshi mstaafu (CDF), Jenerali George Waitara akemea uwindaji haramu Tarime MWENYEKITI wa Bodi ya Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), Mkuu wa Majeshi mstaafu (CDF), Jenerali George Waitara, amewataka wanachi wilayani Tarime, kuachana na uwindaji haramu, badala yake watumie fursa zilizopo kukuza vipato vyao iii kuondokana na umasikini katika ngazi ya familia.  Pia, amewataka wananchi hao watumie fursa hizo kuwekeza katika miradi na biashara mbalimbali katika maeneo jirani na Hifadhi ya Mbuga ya Serengeti, itakayowawezesha kuwaingizia vipato.  Waitara alitoa wito huo mjini Tarime, juzi, alipokutana na baadhi ya wananchi na kubadilishana nao mawazo, wakati akielekea nyumbani kwake k ij iji cha  Itiry o   kusherekea sikukuu ya Pasaka.  Alitoa ushauri kwa watu wenye nia ya kuwekeza katika miradi mbalimbali ya uzalishaji mali wilayani humo, watumie nafasi hiyo iii kukuza na kuendeleza mji waTarime na wilaya hiyo kwa ...

Bei ya unga sasa ni mara 12 ya mfuko wa Simenti

Bei ya unga sasa ni mara 12 ya mfuko wa Simenti WAKATI bei ya unga wa sembe ikipanda mpaka kufikia kuuzwa kati ya Sh. 2,200 na Sh. 2,500 kwa kilo, ile ya mfuko wa saruji wenye uzito wa kilo 50 imeshuka hadi sh. 9,000, sawa na Sh. 180 kwa kilo. Katika masoko na maduka mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam ambayo Nipashe ilitembelea jana, bei ya sembe ilikuwa ikiuzwa kwa kiasi hicho kwa rejareja huku wauzaji wa jumla wakiuza kiroba cha kilo 50 kwa kati ya sh.100,000 na sh.98,000. Ibrahim Omary, mfanyabiashara wa Kariakoo alisema anauza unga wa sembe kwa Sh. 2,400 kwa kuwa hununua kwa bei kubwa kutoka kwa wazalishaji. Alisema kampuni inayojulikana kwa jina la Mkulima huwauzia unga huo kwa Sh. 98,000 na Mama Neema huwauzia kwa sh. 100,000 kwa kiroba cha kilo 50. Kwenye baadhi ya maduka ya kula ya Kinondoni, unga umekuwa ukiuzwa kati ya Sh. 2,200 na Sh. 2,500. Tandika bei ya wastani ni Sh. 2,200, Mwenge Sh. 2,400, Kimara sh. 2,500 na Yombo Vituka sh. 2,200. ...