Skip to main content

Wauguzi kumnyima kura muhimu Kenyatta?

Wauguzi kumnyima kura muhimu Kenyatta?


Nairobi, Kenya. Chama cha Wauguzi Kenya (NNAK) kimejiingiza katika siasa za uchaguzi baada ya kutoa tishio la “kuiaibisha” serikali ya Jubilee kwa madai ya kukawiza majadiliano kuhusu mzozo wa malipo yao.

Wafanyakazi hao wa idara ya afya wanautazama uchaguzi uliopangwa Agosti 8 kama kete yao wakisema kurejeshwa tena mamlakani kwa Rais Uhuru Kenyatta kutakuwa hatarini ikiwa madai yao hayatatekelezwa kwa wakati.

Mwenyekiti wa NNAK, Alfred Obengo alisema: “Tutakuwa na uchaguzi Agosti na sisi tuko 40,000 huku mshindi anatakiwa kupata asilimia 50 jumlisha moja. Idadi yetu haiwezi kupuuzwa.”

Aliongeza: “Kwa hiyo wakati wewe (Rais Uhuru) unaendelea na kampeni, usifikiri hata wakati mmoja kwamba kura za wauguzi si muhimu.”

Waguzi walipiga kambi katika viwanja vya Uhuru Park kulalamikia ukimya wa serikali katika mpango wa malipo ambao wanadai walifikia makubaliano na mwajiri wao.

Walivamia ofisi za Tume ya Mishahara na Marupurupu (SRC) lakini haikusaidia kwani mwenyekiti wa tume hiyo Sarah Serem alisema alikuwa akisubiri mawasiliano kutoka kwa magavana.

Uhuru ahimiza kujitokeza

Naye akitambua tishio la kukosa kura 40,000 Rais Uhuru ameendelea kuwaambia wafuasi wake katika ngome zake muhimu kwamba matokeo ya uchaguzi wa Agosti 8 yataamuliwa na jinsi watakavyojitokeza kumpigia kura na si vinginevyo.

Rais aliwataka wasichezee suala hilo kamwe “kwa kuwa hali halisi ni kuwa mkijitokeza kwa wingi na mnipigie kura, basi huyu mtu wa kutusumbua (mpinzani wake Raila Odinga) kila uchao atakuwa amepata nauli ya kuelekea kwake nyumbani kustaafu.”

Akiwa  katika Kaunti ya Murang’a, Uhuru alisema kuwa “kile sitachoka kuwaambia ni kuwa, kwa wakati huu nawahitaji kwa dhati. Kwa unyenyekevu nawapa tahadhari kuwa mkinichezea mzaha na kura zenu, basi mambo yataishia kwa sisi kushindwa. Mkijitokeza kwa wingi, mambo yatakuwa kwa manufaa yetu.”

Sababu za kususa mdahalo
Kuhusu kutohudhuria kwake mdahalo wa wagombea urais, Uhuru alisema: “Ratiba yangu ya kampeni na ambayo niliwasilisha kwa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka haikuorodhesha mdahalo huo kama jukwaa langu la kampeni.”

Alisema kuwa hadi sasa haoni ni kwa nini kumezuka gumzo kuhusu kususia kwake mdahalo huo ilihali haoni ulikuwa kwa manufaa gani akijitokeze katika ukumbi kujibizana na huyo mtu ambaye kila saa amejawa na uhasama na propaganda dhidi ya serikali yake.

Alisema kuwa kura haziko kwenye runinga na midahalo bali ziko katika mikono ya Wakenya ambao haja yao ni kusaidiwa kujiinua kimaisha “siyo katika safu ya kupewa maneno matupu ya majadiliano.”

Kwingineko Rais Kenyatta alisema aliamua kutoshiriki mdahalo huo kwa kuwa ulikuwa upotevu wa muda.

Kenyatta alisema asingeweza kufanya mdahalo na “mtu ambaye hana agenda kwa nchi hii.”

Popular posts from this blog

Jinsi Wachawi Wanavyo Tumia Mafiga Mabichi Ya Mti Wa Mfausiku Kupika Uchawi Wa Kumvuta Kimapenzi Mtu Aliye Mbali.

Jinsi Wachawi Wanavyo Tumia Mafiga Mabichi Ya Mti Wa Mfausiku Kupika Uchawi Wa Kumvuta Kimapenzi Mtu Aliye Mbali. Na. DOKTA  MUNGWA  KABILI …0744 -000  473.  Wachawi  wanaweza  kutumia  uchawi  kumvuta  kimapenzi  mtu  aliye  mbali. Moja  kati  ya  vitu  vinavyo  tumika  katika  uchawi  huu  ni  pamoja  na  mafiga  mabichi  ya  mti  wa  mfausiku  ambayo  hukokwa  kwenye  majani  makavu ya  mgomba  ambayo  hutumika  kama  kuni  au  moto,  kipande  cha  sanda  alichovalishwa  maiti, herufi za  moto,  mti wa hina, pamoja na  vitu  vingine  lukuki. Kufahamu  kuhusu  uchawi wa aina  hii  na  jinsi  ya  kujikinga  nao, fuatilia  sehemu  ya  nne  ya  kitabu “ KITANDA  CHA  SOKWE  MTU” kama  ifuatavyo : SEHEMU  YA  PILI   YA  KITABU  “ KITANDA  CHA  SOKWE  MTU “ Wachawi   wakishindwa  kukutengenezea  kesi  kubwa  basi  waatakufunga  kwenye  kifungo  cha  mapenzi.  Katika  vifungo  vyote anavyo  fungwa  mwanadamu  hakuna  kifungo  kibaya  kama  kifungo  cha  mape

Faida nyingine za kula chungwa

Faida nyingine za kula chungwa Siku kadhaa zilizopita tuliangalia kwa uchache kuhusu faida za kula chungwa hivyo, pia siku ya leo naomba tuendelee kwa kuangalia faida nyingine za kula chungwa. 1. Ulaji wa machungwa husaidia kutibu mapafu. Chungwa pia lina kiasi kikubwa cha Vitamin B6 na Madini ya Chuma (iron), virubisho ambavyo ni muhimu kwa uzalishaji wa seli nyekundu za damu, ambazo hufanya kazi ya kusafirisha hewa ya oksjeni mwilini, hivyo kuwa muhimu kwa kujikinga na ugonjwa wa mapafu. 2. Husaidia kuimarisha mifupa ya meno. Chungwa lina kiasi kingi cha madini ya kalisi (calcium) ambayo ni muhimu kwa uimarishaji wa mifupa na meno. 3. Husaidia kupunguza kiwango cha mafuta mwilini. Virutubisho vilivyomo kwenye chungwa, hasa kwenye maganda yake, hupunguza kiwango cha mafuta mabaya mwilini (bad cholesterol). Hivyo kwa wenye tatizo la lehemu wanashauriwa kula machungwa pamoja na nyama zake. 4. Hupunguza kupatwa magonjwa wa figo. Ulaji wa machungwa mara kwa mara, ukusaid

Je, unajua Binadamu anatakiwa kulala masaa mangapi?

Je, unajua Binadamu anatakiwa kulala masaa mangapi? Unafikili ni wazo zuri kuamka  saa 11 za asubuhi na kufanya mazoezi? Je, ingekuwa vipi kama ungetumia muda huo kulala? Wataalamu wa afya wanashauri kuwa binadamu kwa kwaida anapaswa kulala angalau masaa 7 wakati wa usiku ili kuupa mwili afya bora. Kulala kwa muda mfupi au masaa machache husababisha matatizo ya afya, ikiwa ni pamoja na shinikizo la damu, unyogovu, ugonjwa wa kisukari, na kupunguzwa kinga kukabiliana na chanjo. Ni vyema ukatumia muda wako vizuri mchana ili usiku ukapata muda mwafaka wa kuweza kuupumzisha mwili ili kuepukana na magonjwa hatari ya shinikizo la damu, kisukari na kupungua kwa kinga mwilini. Najua mazingira yetu waafrika ya kimaisha wakati mwingine yanachangamoto nyingi, lakini pale upatapo mwanya kidogo tu, basi utumie yani "kila penye tundu, penyeza lupia" au wawenzetu wazungu wanasema "one chance two goals".