Skip to main content

Zitto awajibu Chadema

Zitto awajibu Chadema


Mbunge wa Kigoma Mjini ambaye pia ni Kiongozi Mkuu wa chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe amewajibu baadhi ya watu wanaomkosoa na kumuita msaliti kutokana na kitendo cha kumsifia Rais John Magufuli alipokuwa ziarani jimboni humo.

Zitto alijibu mapigo hayo jana wakati akizungumza na wananchi wa Kigoma Mjini, ambapo alisema asingeweza kumkosoa Rais Magufuli wakati ule kwa kuwa alikuwa mgeni jimboni kwake, pia alikuwa anafanya shughuli za maendeleo ya wananchi wa jimboni kwake.

“Rais alikuja hapa akafungua mradi wa maji tukaenda ziwa Tanganyika, kuna watu walikasirika sababu Rais alinisifia sana, hawezi akaja Kigoma mtu akanisema mimi vibaya msingekubali, na mgeni akija siwezi nikaanza kumsema vibaya, mgeni akija unamkaribisha anafanya kazi yake anaondoka, kwani rais akienda kwenye majimbo yao wanamsema, rais alikwenda Bukoba Mjini wakati wa tetemeko, mbunge wa jimbo hilo alimsema ? alikwenda Arumeru kwa mdogo wangu Joshua Nasari, alimsema rais kwa nini akija kigoma mimi ndio nimseme,” alihoji Zitto.

Aliongeza kuwa “Mimi hamkunifundisha kuwa mazwazwa wazee mlinifundisha adabu na kuhakikisha maendeleo yanapatikana lakini sio kwamba rais akikosea hatutamsema tutamsema, na tumeshamsema sana, sisi ndio chama cha mwisho kufanya mkutano wa ziara, tukaja operesheni ya linda demokrasia tumemaliza mikutano ikapigwa marufuku.”

“Lakini toka serikali ya awamu ya tano iingie madarakani uhuru umeanza kuminywa sasa ni lazima, hatuwezi kukaa kimya haki ya watu kuwa na mawazo tofauti hatuwezi kuikalia kimya hata kidogo, lakini wakati huo huo hatuwezi tukasimamisha kila kitu kusubiri haki ya kuwa na mawazo huru, lazima haki ya mawazo huru ipiganiwe wakati tunapigania maendeleo,” amesema

Popular posts from this blog

Jinsi Wachawi Wanavyo Tumia Mafiga Mabichi Ya Mti Wa Mfausiku Kupika Uchawi Wa Kumvuta Kimapenzi Mtu Aliye Mbali.

Jinsi Wachawi Wanavyo Tumia Mafiga Mabichi Ya Mti Wa Mfausiku Kupika Uchawi Wa Kumvuta Kimapenzi Mtu Aliye Mbali. Na. DOKTA  MUNGWA  KABILI …0744 -000  473.  Wachawi  wanaweza  kutumia  uchawi  kumvuta  kimapenzi  mtu  aliye  mbali. Moja  kati  ya  vitu  vinavyo  tumika  katika  uchawi  huu  ni  pamoja  na  mafiga  mabichi  ya  mti  wa  mfausiku  ambayo  hukokwa  kwenye  majani  makavu ya  mgomba  ambayo  hutumika  kama  kuni  au  moto,  kipande  cha  sanda  alichovalishwa  maiti, herufi za  moto,  mti wa hina, pamoja na  vitu  vingine  lukuki. Kufahamu  kuhusu  uchawi wa aina  hii  na  jinsi  ya  kujikinga  nao, fuatilia  sehemu  ya  nne  ya  kitabu “ KITANDA  CHA  SOKWE  MTU” kama  ifuatavyo : SEHEMU  YA  PILI   YA  KITABU  “ KITANDA  CHA  SOKWE  MTU “ Wachawi   wakishindwa  kukutengenezea  kesi  kubwa  basi  waatakufunga  kwenye  kifungo  cha  mapenzi.  Katika  vifungo  vyote anavyo  fungwa  mwanadamu  hakuna  kifungo  kibaya  kama  kifungo  cha  mape

Faida nyingine za kula chungwa

Faida nyingine za kula chungwa Siku kadhaa zilizopita tuliangalia kwa uchache kuhusu faida za kula chungwa hivyo, pia siku ya leo naomba tuendelee kwa kuangalia faida nyingine za kula chungwa. 1. Ulaji wa machungwa husaidia kutibu mapafu. Chungwa pia lina kiasi kikubwa cha Vitamin B6 na Madini ya Chuma (iron), virubisho ambavyo ni muhimu kwa uzalishaji wa seli nyekundu za damu, ambazo hufanya kazi ya kusafirisha hewa ya oksjeni mwilini, hivyo kuwa muhimu kwa kujikinga na ugonjwa wa mapafu. 2. Husaidia kuimarisha mifupa ya meno. Chungwa lina kiasi kingi cha madini ya kalisi (calcium) ambayo ni muhimu kwa uimarishaji wa mifupa na meno. 3. Husaidia kupunguza kiwango cha mafuta mwilini. Virutubisho vilivyomo kwenye chungwa, hasa kwenye maganda yake, hupunguza kiwango cha mafuta mabaya mwilini (bad cholesterol). Hivyo kwa wenye tatizo la lehemu wanashauriwa kula machungwa pamoja na nyama zake. 4. Hupunguza kupatwa magonjwa wa figo. Ulaji wa machungwa mara kwa mara, ukusaid

Je, unajua Binadamu anatakiwa kulala masaa mangapi?

Je, unajua Binadamu anatakiwa kulala masaa mangapi? Unafikili ni wazo zuri kuamka  saa 11 za asubuhi na kufanya mazoezi? Je, ingekuwa vipi kama ungetumia muda huo kulala? Wataalamu wa afya wanashauri kuwa binadamu kwa kwaida anapaswa kulala angalau masaa 7 wakati wa usiku ili kuupa mwili afya bora. Kulala kwa muda mfupi au masaa machache husababisha matatizo ya afya, ikiwa ni pamoja na shinikizo la damu, unyogovu, ugonjwa wa kisukari, na kupunguzwa kinga kukabiliana na chanjo. Ni vyema ukatumia muda wako vizuri mchana ili usiku ukapata muda mwafaka wa kuweza kuupumzisha mwili ili kuepukana na magonjwa hatari ya shinikizo la damu, kisukari na kupungua kwa kinga mwilini. Najua mazingira yetu waafrika ya kimaisha wakati mwingine yanachangamoto nyingi, lakini pale upatapo mwanya kidogo tu, basi utumie yani "kila penye tundu, penyeza lupia" au wawenzetu wazungu wanasema "one chance two goals".