Skip to main content

Makamu wa Rais ameitaka Jamii kuwapa kipaumbele walemavu kwenye maendeleo

Makamu wa Rais ameitaka Jamii kuwapa kipaumbele walemavu kwenye maendeleo



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ameitaka jamii kuhakikisha kuwa watu wenye ulemavu hawaachwi nyuma kwenye nyanja zote za maendeleo.

Makamu wa Rais ameyasema hayo wakati wa maadhimisho ya Siku ya Watu wenye ulemavu duniani iliyofanyika mkoa wa Kusini, Unguja, Zanzibar.

Akihutubia mamia ya watu wenye ulemavu na wasio na ulemavu kwenye kwenye viwanja vya Skuli ya Uzini, Makamu wa Rais alisema tumejumuika leo hapa kuungana na wenzetu duniani kote kuadhimisha kilele cha siku ya Kimataifa ya Watu wenye Ulemavu Duniani ambayo imebeba kauli mbiu isemayo “Mabadiliko kuelekea jamii Jumuishi na Maendeleo Endelevu kwa wote”­­­­­­ ujumbe huu unalenga kuhakikisha kuwa watu wenye ulemavu wanajumuishwa katika mipango yote ya maendeleo ili kuweza kufikia malengo endelevu ya dunia ifikapo mwaka 2030 pia inakwenda sambamba na Dira ya Maendeleo ya Zanzibar ya 2020; Ilani ya Chama Tawala na mpango wa kukuza Uchumi na kupunguza Umasikini Zanzibar (MKUZA III) ambapo masuala ya watu wenye ulemavu yamezingatiwa.”

Tanzania iliridhia mkataba wa kimataifa wa haki za watu wenye ulemavu ambao umeweka misingi madhubuti wa utekelezaji wa masuala mbali mbali kwa ajili ya watu wenye ulemavu, ikiwemo; Usawa, Ushirikishwaji kikamilifu katika mipango ya hifadhi ya jamii na kupunguza umasikini na kuwapatia huduma pamoja na kufanya kazi na taasisi zinazoshughulikia masuala ya watu wenye ulemavu,” alisema Makamu wa Rais.

Makamu wa Rais alitoa rai kwa kusema “kuanzia leo(jana) kila mmoja miongoni mwetu awe askari wa mwenzie katika kuhakikisha kuwa tunalinda haki na usawa wa watu wenye ulemavu”.

Makamu wa Rais aliwaasa wanafamilia kutoficha maovu wanayofanyiwa watu wenye ulemavu, alisema Serikali kwa nguvu zote inakemea vitendo vya ubakaji na udhalilishaji kwa watu wenye ulemavu kwani si vitendo vya kiungwana hata kidogo na kuvitaka vyombo vya ulinzi na usalama kuwashughulikia kikamilifu wahalifu hawa na wakithibitika wafikishwe kwenye vyombo vya sheria ikiwemo mahakama na kutoa adhabu kali dhidi ya wale watakaobainika.

Makamu wa Rais alisema Serikali kwa kushirikiana na Wadau wengine wa Maendeleo pamoja na wananchi itaendelea kuhakikisha kuwa ‘digital technology’ inakuwa rafiki kwa walemavu hususan katika kuwawezesha kupata elimu, vitendea kazi katika maendeo yao pamoja na kuhakikisha wanafikia kirahisi huduma zote za kijamii.


  • Kwa upande wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ilisema itaendelea kuweka mipango thabiti na mathubuti yenye kuhakikisha watu wenye ulemavu wanapata haki za kisiasa, kiuchumi, kijamii na fursa sawa kama wengine na kuahikisha watu wenye ulemavu wanashiriki kikamilifu katika ngazi mbali mbaliza uongozi za kitaifa.

Popular posts from this blog

Jinsi ya kutengeneza SABUNI ya kipande YA KUGANDISHA

Jinsi ya kutengeneza SABUNI ya kipande YA KUGANDISHA Utengenezaji wa sabuni hii una njia nyingi Hatua  ya kwanza Chemsha vipimo 7 vya mafuta ya mawese au mafuta ya shea hadi ifikie hatua ya kimiminika chuja na yaweke kwenye chungu cha mfinyanzi au chombo cha plastiki. Hatua ya pili Pima vipimo 5 vya maji baridi kwenye chombo cha plastiki ongeza kipimo 1cha sodium hydroxide kwa uangalifu mkubwa kwenye maji acha hadi mchanganyiko huo uyeyuke. Subiri mchanganyiko wa sodium hydroxide na mafuta ukaribie kupoa. Hatua ya tatu Taratibu ongeza mchanganyiko wa sodium hydroxide kwenye mawese,huku ukikoroga haraka haraka bila kusitisha ukitumia ubao .hii ni njia nzuri zaidi. Njia ya pili Chemsha mafuta kwenye joto la kadiri ya 55C Changanya maji na sodium hydroxide na uache mchanganyiko huu upoe hadi kufikia joto hilohilo. Baada ya kuandaa mchanyiko wako changanya vimiminika hivyo viwili huku ukikoroga kwanguvu sana kadiri uwezavyo, taratibu sabuni itageuka kuwa laini. Kabla...

Mkuu wa Majeshi mstaafu (CDF), Jenerali George Waitara akemea uwindaji haramu Tarime

Mkuu wa Majeshi mstaafu (CDF), Jenerali George Waitara akemea uwindaji haramu Tarime MWENYEKITI wa Bodi ya Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), Mkuu wa Majeshi mstaafu (CDF), Jenerali George Waitara, amewataka wanachi wilayani Tarime, kuachana na uwindaji haramu, badala yake watumie fursa zilizopo kukuza vipato vyao iii kuondokana na umasikini katika ngazi ya familia.  Pia, amewataka wananchi hao watumie fursa hizo kuwekeza katika miradi na biashara mbalimbali katika maeneo jirani na Hifadhi ya Mbuga ya Serengeti, itakayowawezesha kuwaingizia vipato.  Waitara alitoa wito huo mjini Tarime, juzi, alipokutana na baadhi ya wananchi na kubadilishana nao mawazo, wakati akielekea nyumbani kwake k ij iji cha  Itiry o   kusherekea sikukuu ya Pasaka.  Alitoa ushauri kwa watu wenye nia ya kuwekeza katika miradi mbalimbali ya uzalishaji mali wilayani humo, watumie nafasi hiyo iii kukuza na kuendeleza mji waTarime na wilaya hiyo kwa ...

Bei ya unga sasa ni mara 12 ya mfuko wa Simenti

Bei ya unga sasa ni mara 12 ya mfuko wa Simenti WAKATI bei ya unga wa sembe ikipanda mpaka kufikia kuuzwa kati ya Sh. 2,200 na Sh. 2,500 kwa kilo, ile ya mfuko wa saruji wenye uzito wa kilo 50 imeshuka hadi sh. 9,000, sawa na Sh. 180 kwa kilo. Katika masoko na maduka mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam ambayo Nipashe ilitembelea jana, bei ya sembe ilikuwa ikiuzwa kwa kiasi hicho kwa rejareja huku wauzaji wa jumla wakiuza kiroba cha kilo 50 kwa kati ya sh.100,000 na sh.98,000. Ibrahim Omary, mfanyabiashara wa Kariakoo alisema anauza unga wa sembe kwa Sh. 2,400 kwa kuwa hununua kwa bei kubwa kutoka kwa wazalishaji. Alisema kampuni inayojulikana kwa jina la Mkulima huwauzia unga huo kwa Sh. 98,000 na Mama Neema huwauzia kwa sh. 100,000 kwa kiroba cha kilo 50. Kwenye baadhi ya maduka ya kula ya Kinondoni, unga umekuwa ukiuzwa kati ya Sh. 2,200 na Sh. 2,500. Tandika bei ya wastani ni Sh. 2,200, Mwenge Sh. 2,400, Kimara sh. 2,500 na Yombo Vituka sh. 2,200. ...