Skip to main content

Viongozi wa TSSF watiwa mbaroni

Viongozi wa TSSF watiwa mbaroni



Viongozi wa  Taasisi ya Kusaidia Jamii ( TSSF) ambayo ilitangaza kuwa inatoa mikopo ya elimu ya juu wamekamatwa na polisi baada ya kugundulika kuwa ni matapeli.

Wakurugenzi hao wamekamatwa jana Jumatatu jioni mara tu baada ya mkutano wa waandishi wa habari na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, William Ole Nasha wa kuelezea kuhusu uchunguzi uliofanyika baada ya Mbunge wa Mafinga Mjini (CCM), Cosato Chumi kuomba mwongozo bungeni.

Chumi alitaka ufafanuzi kuhusu uhalali wa taasisi hiyo baada ya kutangaza kutoa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu kwa kulipa Sh 30 000 kama ada ya maombi ya kusajiliwa kuomba mkopo.

Hata hivyo, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako amesema  Serikali haitambui taasisi hiyo na kuahidi kufanya uchunguzi.

Akizungumza leo Jumanne, Ole Nasha amesema baada ya uchunguzi huo wamebaini kuwa taasisi hiyo haina uwezo wa kutoa mikopo kwa wanafunzi 50,000 ambao ilitangaza kutoa.

Amesema katika mahojiano na taasisi hiyo viongozi hao walisema kuwa fedha za kuwakopesha wanafunzi hao watazipata kutoka nje ya nchi baada ya kupeleka kiasi cha fedha.

Hata hivyo, amesema mkataba wa taasisi hiyo na wafadhili hao unaonyesha kuwa wamefikia makubaliano ya kufanya utafiti wa jinsi wanavyoweza kukusanya fedha na si kuwapa fedha kwa ajili ya kutoa mikopo.

Amesema tayari taasisi hiyo imekusanya fedha kwa wanafunzi 600 na imepeleka wanafunzi 198 katika vyuo mbalimbali nchini kwa makubaliano ada zao wangelipa Desemba mwaka huu.

Hata hivyo, amesema hakuna uthibitisho kama wana fedha kweli za kuwalipia wanafunzi hao ada ingawa wanadai kuwa katika akaunti zao za benki wana fedha kati ya Sh 600 milioni na 700 milioni.

Amesema kufuatia hilo wanaagiza vyombo vya dola kuchunguza jambo hilo na wakati wakifanya hivyo ni marufuku kwa vyuo kuwapokea wanafunzi wanaopewa mikopo na taasisi hiyo.

Pia ameagiza akaunti zao zote kufungiwa hadi hapo watakapomaliza uchunguzi sambamba na taasisi hiyo kutojihusisha na shughuli yoyote.

Baada ya kumaliza mkutano huo polisi kutoka makao makuu ya polisi waliingia ndani ya ukumbi wa mkutano na kuwaeleza wako chini ya ulinzi.

Polisi hao mmoja akiwa na sare na mwingine akiwa na nguo za kiraia waliwakamata na kuondoka nao.

Popular posts from this blog

Jinsi Wachawi Wanavyo Tumia Mafiga Mabichi Ya Mti Wa Mfausiku Kupika Uchawi Wa Kumvuta Kimapenzi Mtu Aliye Mbali.

Jinsi Wachawi Wanavyo Tumia Mafiga Mabichi Ya Mti Wa Mfausiku Kupika Uchawi Wa Kumvuta Kimapenzi Mtu Aliye Mbali. Na. DOKTA  MUNGWA  KABILI …0744 -000  473.  Wachawi  wanaweza  kutumia  uchawi  kumvuta  kimapenzi  mtu  aliye  mbali. Moja  kati  ya  vitu  vinavyo  tumika  katika  uchawi  huu  ni  pamoja  na  mafiga  mabichi  ya  mti  wa  mfausiku  ambayo  hukokwa  kwenye  majani  makavu ya  mgomba  ambayo  hutumika  kama  kuni  au  moto,  kipande  cha  sanda  alichovalishwa  maiti, herufi za  moto,  mti wa hina, pamoja na  vitu  vingine  lukuki. Kufahamu  kuhusu  uchawi wa aina  hii  na  jinsi  ya  kujikinga  nao, fuatilia  sehemu  ya  nne  ya  kitabu “ KITANDA  CHA  SOKWE  MTU” kama  ifuatavyo : SEHEMU  YA  PILI   YA  KITABU  “ KITANDA  CHA  SOKWE  MTU “ Wachawi   wakishindwa  kukutengenezea  kesi  kubwa  basi  waatakufunga  kwenye  kifungo  cha  mapenzi.  Katika  vifungo  vyote anavyo  fungwa  mwanadamu  hakuna  kifungo  kibaya  kama  kifungo  cha  mape

Faida nyingine za kula chungwa

Faida nyingine za kula chungwa Siku kadhaa zilizopita tuliangalia kwa uchache kuhusu faida za kula chungwa hivyo, pia siku ya leo naomba tuendelee kwa kuangalia faida nyingine za kula chungwa. 1. Ulaji wa machungwa husaidia kutibu mapafu. Chungwa pia lina kiasi kikubwa cha Vitamin B6 na Madini ya Chuma (iron), virubisho ambavyo ni muhimu kwa uzalishaji wa seli nyekundu za damu, ambazo hufanya kazi ya kusafirisha hewa ya oksjeni mwilini, hivyo kuwa muhimu kwa kujikinga na ugonjwa wa mapafu. 2. Husaidia kuimarisha mifupa ya meno. Chungwa lina kiasi kingi cha madini ya kalisi (calcium) ambayo ni muhimu kwa uimarishaji wa mifupa na meno. 3. Husaidia kupunguza kiwango cha mafuta mwilini. Virutubisho vilivyomo kwenye chungwa, hasa kwenye maganda yake, hupunguza kiwango cha mafuta mabaya mwilini (bad cholesterol). Hivyo kwa wenye tatizo la lehemu wanashauriwa kula machungwa pamoja na nyama zake. 4. Hupunguza kupatwa magonjwa wa figo. Ulaji wa machungwa mara kwa mara, ukusaid

Je, unajua Binadamu anatakiwa kulala masaa mangapi?

Je, unajua Binadamu anatakiwa kulala masaa mangapi? Unafikili ni wazo zuri kuamka  saa 11 za asubuhi na kufanya mazoezi? Je, ingekuwa vipi kama ungetumia muda huo kulala? Wataalamu wa afya wanashauri kuwa binadamu kwa kwaida anapaswa kulala angalau masaa 7 wakati wa usiku ili kuupa mwili afya bora. Kulala kwa muda mfupi au masaa machache husababisha matatizo ya afya, ikiwa ni pamoja na shinikizo la damu, unyogovu, ugonjwa wa kisukari, na kupunguzwa kinga kukabiliana na chanjo. Ni vyema ukatumia muda wako vizuri mchana ili usiku ukapata muda mwafaka wa kuweza kuupumzisha mwili ili kuepukana na magonjwa hatari ya shinikizo la damu, kisukari na kupungua kwa kinga mwilini. Najua mazingira yetu waafrika ya kimaisha wakati mwingine yanachangamoto nyingi, lakini pale upatapo mwanya kidogo tu, basi utumie yani "kila penye tundu, penyeza lupia" au wawenzetu wazungu wanasema "one chance two goals".