Skip to main content

Tambwe arejesha furaha Yanga

Tambwe arejesha furaha Yanga


MSHAMBULIAJI AMISSI TAMBWE.

Mshambuliaji Amissi Tambwe amerejesha furaha Yanga baada ya jana kwa mara ya kwanza kuanza mazoezi kufuatia kuwa nje kwa muda mrefu akiuguza majeraha.

Tambwe amekosa mechi zote za Ligi Kuu Yanga tangu kuanza kwa msimu huu, lakini sasa inaelezwa kuwa anaweza kushuka dimbani baada ya mchezo ujao dhidi ya Mbeya City utakaochezwa Jumapili ijayo kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

Mechi ijayo ya Yanga itakuwa dhidi ya Tanzania Prisons itakayopigwa Uwanja wa Uhuru Jumamosi ya Novemba 25, mwaka huu.

Katika mazoezi ya jana asubuhi, Tambwe alifanya mazoezi mepesi ya peke yake na ametakiwa kufanya hivyo kwa angalau siku tatu kabla ya kuanza kujifua kamili na wenzake.

Meneja wa Yanga inayodhaminiwa na Kampuni ya Kubashiri Matokeo Michezoni ya SportPesa, Hafidh Saleh, aliliambia Nipashe baada ya mazoezi hayo jana kwamba, pamoja na Tambwe kuanza kujifua, hatocheza mchezo wa Jumamosi.

“Kwa mchezo wa Jumamosi hatoweza kucheza kwa sababu daktari amemtaka kuanza na mazoezi mepesi kwa siku tatu baada ya hapo ataungana na wenzake kwa program za mwalimu (George Lwandamina),” alisema Saleh.

Usajili sasa siri
Katika hatua nyingine, benchi la ufundi la timu hiyo, bado halijaweka wazi kama litahitaji kufanya usajili katika dirisha dogo la usajili lililofunguliwa leo.

“Kwa kweli suala la usajili bado, kocha amerejea jana na ni mpaka atakapokutana na uongozi ndipo tutajua kama kuna usajili utafanyika,” alisema Saleh.

Alisema kocha Lwandamina alirejea nchini jana alfajiri akitokea kwao Zambia na leo ataungana na kikosi chake kuendelea na program ya mazoezi kujiandaa na mchezo wa Jumamosi huku wachezaji waliokuwa kwenye kikosi cha timu ya Taifa ‘Taifa Stars’ wakipewa mapumziko ya siku moja.

Popular posts from this blog

Jinsi ya kutengeneza SABUNI ya kipande YA KUGANDISHA

Jinsi ya kutengeneza SABUNI ya kipande YA KUGANDISHA Utengenezaji wa sabuni hii una njia nyingi Hatua  ya kwanza Chemsha vipimo 7 vya mafuta ya mawese au mafuta ya shea hadi ifikie hatua ya kimiminika chuja na yaweke kwenye chungu cha mfinyanzi au chombo cha plastiki. Hatua ya pili Pima vipimo 5 vya maji baridi kwenye chombo cha plastiki ongeza kipimo 1cha sodium hydroxide kwa uangalifu mkubwa kwenye maji acha hadi mchanganyiko huo uyeyuke. Subiri mchanganyiko wa sodium hydroxide na mafuta ukaribie kupoa. Hatua ya tatu Taratibu ongeza mchanganyiko wa sodium hydroxide kwenye mawese,huku ukikoroga haraka haraka bila kusitisha ukitumia ubao .hii ni njia nzuri zaidi. Njia ya pili Chemsha mafuta kwenye joto la kadiri ya 55C Changanya maji na sodium hydroxide na uache mchanganyiko huu upoe hadi kufikia joto hilohilo. Baada ya kuandaa mchanyiko wako changanya vimiminika hivyo viwili huku ukikoroga kwanguvu sana kadiri uwezavyo, taratibu sabuni itageuka kuwa laini. Kabla...

Mkuu wa Majeshi mstaafu (CDF), Jenerali George Waitara akemea uwindaji haramu Tarime

Mkuu wa Majeshi mstaafu (CDF), Jenerali George Waitara akemea uwindaji haramu Tarime MWENYEKITI wa Bodi ya Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), Mkuu wa Majeshi mstaafu (CDF), Jenerali George Waitara, amewataka wanachi wilayani Tarime, kuachana na uwindaji haramu, badala yake watumie fursa zilizopo kukuza vipato vyao iii kuondokana na umasikini katika ngazi ya familia.  Pia, amewataka wananchi hao watumie fursa hizo kuwekeza katika miradi na biashara mbalimbali katika maeneo jirani na Hifadhi ya Mbuga ya Serengeti, itakayowawezesha kuwaingizia vipato.  Waitara alitoa wito huo mjini Tarime, juzi, alipokutana na baadhi ya wananchi na kubadilishana nao mawazo, wakati akielekea nyumbani kwake k ij iji cha  Itiry o   kusherekea sikukuu ya Pasaka.  Alitoa ushauri kwa watu wenye nia ya kuwekeza katika miradi mbalimbali ya uzalishaji mali wilayani humo, watumie nafasi hiyo iii kukuza na kuendeleza mji waTarime na wilaya hiyo kwa ...

SADC YALIPONGEZA BARAZA LA USALAMA LA UN KWA KUONGEZA MUDA KWA MISHENI YA ULINZI DRC

SADC YALIPONGEZA BARAZA LA USALAMA LA UN KWA KUONGEZA MUDA KWA MISHENI YA ULINZI DRC 1 2 3 4 5 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) kuhusu mkutano wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa uliofanyika New York, Marekani na kupitisha Azimio la kuongeza muda kwa vikosi vya usalama vilivyopo DRC. Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy. Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza Mhe. Mahiga (hayupo pichani). Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mwenyekiti wa Kamati ya Mawaziri ya Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (Mb). akihutubia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa Jijini New York, Marekani. TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ambaye pia ni Mwenyekiti wa...