Skip to main content

Tambwe arejesha furaha Yanga

Tambwe arejesha furaha Yanga


MSHAMBULIAJI AMISSI TAMBWE.

Mshambuliaji Amissi Tambwe amerejesha furaha Yanga baada ya jana kwa mara ya kwanza kuanza mazoezi kufuatia kuwa nje kwa muda mrefu akiuguza majeraha.

Tambwe amekosa mechi zote za Ligi Kuu Yanga tangu kuanza kwa msimu huu, lakini sasa inaelezwa kuwa anaweza kushuka dimbani baada ya mchezo ujao dhidi ya Mbeya City utakaochezwa Jumapili ijayo kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

Mechi ijayo ya Yanga itakuwa dhidi ya Tanzania Prisons itakayopigwa Uwanja wa Uhuru Jumamosi ya Novemba 25, mwaka huu.

Katika mazoezi ya jana asubuhi, Tambwe alifanya mazoezi mepesi ya peke yake na ametakiwa kufanya hivyo kwa angalau siku tatu kabla ya kuanza kujifua kamili na wenzake.

Meneja wa Yanga inayodhaminiwa na Kampuni ya Kubashiri Matokeo Michezoni ya SportPesa, Hafidh Saleh, aliliambia Nipashe baada ya mazoezi hayo jana kwamba, pamoja na Tambwe kuanza kujifua, hatocheza mchezo wa Jumamosi.

“Kwa mchezo wa Jumamosi hatoweza kucheza kwa sababu daktari amemtaka kuanza na mazoezi mepesi kwa siku tatu baada ya hapo ataungana na wenzake kwa program za mwalimu (George Lwandamina),” alisema Saleh.

Usajili sasa siri
Katika hatua nyingine, benchi la ufundi la timu hiyo, bado halijaweka wazi kama litahitaji kufanya usajili katika dirisha dogo la usajili lililofunguliwa leo.

“Kwa kweli suala la usajili bado, kocha amerejea jana na ni mpaka atakapokutana na uongozi ndipo tutajua kama kuna usajili utafanyika,” alisema Saleh.

Alisema kocha Lwandamina alirejea nchini jana alfajiri akitokea kwao Zambia na leo ataungana na kikosi chake kuendelea na program ya mazoezi kujiandaa na mchezo wa Jumamosi huku wachezaji waliokuwa kwenye kikosi cha timu ya Taifa ‘Taifa Stars’ wakipewa mapumziko ya siku moja.

Popular posts from this blog

Lema ahoji kushikiliwa mmiliki wa shule ya Lucky Vincent

Lema ahoji kushikiliwa mmiliki wa shule ya Lucky Vincent Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema   Dodoma. Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema amehoji sababu za polisi kumshikilia mmiliki wa shule ya Lucky Vincent badala ya trafiki waliokuwa barabarani siku ya ajali iliyoua watu 35. Akiomba mwongozo wa Spika kuhusu jambo hilo leo, amesema katika eneo husika kuna vizuizi vya ukaguzi vinne lakini trafiki hawakuona kuwa basi hilo lilikuwa kimezidisha watoto na hawakuwa wamefunga mikanda. Amesema badala ya trafiki hao kuchukuliwa hatua, anakamatwa mmiliki ambaye hakuwapo. Akijibu mwongozo huo, Naibu Spika, Dk Tulia Ackson amesema suala hilo halijatokea bungeni.

Bei ya unga sasa ni mara 12 ya mfuko wa Simenti

Bei ya unga sasa ni mara 12 ya mfuko wa Simenti WAKATI bei ya unga wa sembe ikipanda mpaka kufikia kuuzwa kati ya Sh. 2,200 na Sh. 2,500 kwa kilo, ile ya mfuko wa saruji wenye uzito wa kilo 50 imeshuka hadi sh. 9,000, sawa na Sh. 180 kwa kilo. Katika masoko na maduka mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam ambayo Nipashe ilitembelea jana, bei ya sembe ilikuwa ikiuzwa kwa kiasi hicho kwa rejareja huku wauzaji wa jumla wakiuza kiroba cha kilo 50 kwa kati ya sh.100,000 na sh.98,000. Ibrahim Omary, mfanyabiashara wa Kariakoo alisema anauza unga wa sembe kwa Sh. 2,400 kwa kuwa hununua kwa bei kubwa kutoka kwa wazalishaji. Alisema kampuni inayojulikana kwa jina la Mkulima huwauzia unga huo kwa Sh. 98,000 na Mama Neema huwauzia kwa sh. 100,000 kwa kiroba cha kilo 50. Kwenye baadhi ya maduka ya kula ya Kinondoni, unga umekuwa ukiuzwa kati ya Sh. 2,200 na Sh. 2,500. Tandika bei ya wastani ni Sh. 2,200, Mwenge Sh. 2,400, Kimara sh. 2,500 na Yombo Vituka sh. 2,200. ...

Jinsi ya kutengeneza SABUNI ya kipande YA KUGANDISHA

Jinsi ya kutengeneza SABUNI ya kipande YA KUGANDISHA Utengenezaji wa sabuni hii una njia nyingi Hatua  ya kwanza Chemsha vipimo 7 vya mafuta ya mawese au mafuta ya shea hadi ifikie hatua ya kimiminika chuja na yaweke kwenye chungu cha mfinyanzi au chombo cha plastiki. Hatua ya pili Pima vipimo 5 vya maji baridi kwenye chombo cha plastiki ongeza kipimo 1cha sodium hydroxide kwa uangalifu mkubwa kwenye maji acha hadi mchanganyiko huo uyeyuke. Subiri mchanganyiko wa sodium hydroxide na mafuta ukaribie kupoa. Hatua ya tatu Taratibu ongeza mchanganyiko wa sodium hydroxide kwenye mawese,huku ukikoroga haraka haraka bila kusitisha ukitumia ubao .hii ni njia nzuri zaidi. Njia ya pili Chemsha mafuta kwenye joto la kadiri ya 55C Changanya maji na sodium hydroxide na uache mchanganyiko huu upoe hadi kufikia joto hilohilo. Baada ya kuandaa mchanyiko wako changanya vimiminika hivyo viwili huku ukikoroga kwanguvu sana kadiri uwezavyo, taratibu sabuni itageuka kuwa laini. Kabla...