Skip to main content

WANANCHI NYANZWA KILOLO WAPONGEZA ASASI YA MMADEA KWA KUWAPATIA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

WANANCHI NYANZWA KILOLO WAPONGEZA ASASI YA MMADEA KWA KUWAPATIA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO




Mkurugenzi mtendaji wa MMADEA Raphael Mtitu akipokea pongezi za wananchi wa Nyanzwa

WANANCHi wa kataya Nyanzwa wilaya ya Kilolo mkoani Iringa wamepongeza asasi yaisiyo ya kiserikali ya mahenge mazombe devolopment association(MMADEA) kwa kusaidia kuelimisha wananchi kuendelea nautamaduni wao wa kuoa wadodo wadogo pamoja na afya ya uzazi kwa mama na mtoto.
Wakizungumza namwandishi wa habari hizi wakati wa mikutano ya tathiminiya mradi shughuli za MMADEA zilizofanyika katika kata hiyojana wananchi hao walisema kuwa awali wananchi katika kata hiyo ilikuwa ni utamaduni wao kwawatu wazima kuoa watoto chini ya miaka 18 ila baada ya kupewa elimu hiyo na MMADEA kwa sasahakuna ndoa za utotoni zinazofungwa wala hakuna mwananchianayejihusisha na mahusiano ya mtoto .
Abdalah Juma mkazi wa kijiji cha Nyanzwaalisema kuwa idadi ya wananchi kuendelea na mahusianona watoto wadogo katika kijiji hicho imepungua baada ya elimu ya mara kwamara iliyotolewa na asiasi hiyo ya MMADEA na hivyo kwa sasa jamii imekuwa na lengo moja la kulinda watoto hao .Hivyo aliomba serikali na asasi hiyo yaMMADEA kuendelea kutoa elimu hiyo mara kwa mara na katika maeneo mengine ya mkoa wa Iringa kwani mbali yakijiji na kata hiyo ya Nyanzwa yapo maeneo ambayo hayajafikiwana elimu hiyo .
Akizungumza kwa niaba ya wanawake wenzake Neema Nzakule (19) alisema kuwa aliolewa akiwa na miaka14 na sasa ana watoto watano na awali alikuwa hakuwa na elimu yeyote juu ya afya ya mama na mtoto ila baada ya kushirikiwarsha mbali mbali ambazo MMADEA wamekuwa wakizitoa katika kijiji chao amekuwani mshiriki mzuri wa kuhudhuria kliniki pamoja na kuwaelimisha wanzake kuepuka ndoa za utotoni .

"Mimi ni mmoja kati ya wanufaika wakubwa wa mafunzo mbali mbaliambayo yamekuwa yakitolewa na shirika la MMADEA na kila napo sikia wanakuja huwa nasitisha shughuli zangu zote ili kushirikimafunzo yao maana na yamenisaidia sana nimeweza kuboreshaafya yangu "

Alisema kuwa alilazimishwa na wazazi wake kuolewa na mwanaume mwenye miaka zaidi ya 40 kutokana na kuwa na pesa na ng'ombe nyingina alipotaka kukataa alitishwa ila alivumilia na kwa sasakupitia elimu ambayoanapatiwa ameweza kumfanya mwenziwake huyo kuhudhuria kliniki pamoja .
Mwenyekiti wa kijiji cha Nyanzwa Samsoni Sambuli alisema kuwa kupitia elimu inayotolewa na MMADEA kijiji kimeweza kuwa na mabadiliko makubwa na hata kujiwekea sheria ndogo ya kuwalea watoto wadogo kwa kuwawajibisha wanaume wanaojihusisha na mapenzi na watoto .
 Alisema kwa kijana au mwanamke atakayekutwa katika mazingira tata na mwanafunzi adhabu yake ni kutozwa faini isiyo pungua shilingi 30000 ama kufikishwa mahakamani na kuwa wapo waliokutwa na adhabu hiyo.

Muuguzi mkuu wilaya ya Kilolo Withnes Mlowe alisema kuwa kasi ya mimba zautotoni kwenye kata hiyo imepungua sana na kuwa suala la afya ya mama na mtoto limepewa kipaumbele huku akitakawananchi kurejesha utamaduni wa unyagokwa vijana wao ili kuwapa elimu ya uzazi mapema.
“ unyago naotaka sio wa ukeketaji niule wa kuwapa elimu juu ya afya zaoili kuwaepusha na majanga mbali mbali “
Mkurungezi wa MMADEA Raphaeli alisema maradi huo unafanyika kwenye kata tatu ya Nyazwa Ibumu Idete .
Mkurugenzi wa MMADEA Bw Mtitu akiahoji walimu wa Shule ya msingi Igunda juu ya mrejesho wa mafunzi waliyopewa juu ya afya ya mama na mtoto 
mwezeshaji Wa MMADEA Winfrida akitoa elimu ya afya ya mama na mtoto kwa wananchi wa Igunda

Popular posts from this blog

Jinsi ya kutengeneza SABUNI ya kipande YA KUGANDISHA

Jinsi ya kutengeneza SABUNI ya kipande YA KUGANDISHA Utengenezaji wa sabuni hii una njia nyingi Hatua  ya kwanza Chemsha vipimo 7 vya mafuta ya mawese au mafuta ya shea hadi ifikie hatua ya kimiminika chuja na yaweke kwenye chungu cha mfinyanzi au chombo cha plastiki. Hatua ya pili Pima vipimo 5 vya maji baridi kwenye chombo cha plastiki ongeza kipimo 1cha sodium hydroxide kwa uangalifu mkubwa kwenye maji acha hadi mchanganyiko huo uyeyuke. Subiri mchanganyiko wa sodium hydroxide na mafuta ukaribie kupoa. Hatua ya tatu Taratibu ongeza mchanganyiko wa sodium hydroxide kwenye mawese,huku ukikoroga haraka haraka bila kusitisha ukitumia ubao .hii ni njia nzuri zaidi. Njia ya pili Chemsha mafuta kwenye joto la kadiri ya 55C Changanya maji na sodium hydroxide na uache mchanganyiko huu upoe hadi kufikia joto hilohilo. Baada ya kuandaa mchanyiko wako changanya vimiminika hivyo viwili huku ukikoroga kwanguvu sana kadiri uwezavyo, taratibu sabuni itageuka kuwa laini. Kabla...

Bei ya unga sasa ni mara 12 ya mfuko wa Simenti

Bei ya unga sasa ni mara 12 ya mfuko wa Simenti WAKATI bei ya unga wa sembe ikipanda mpaka kufikia kuuzwa kati ya Sh. 2,200 na Sh. 2,500 kwa kilo, ile ya mfuko wa saruji wenye uzito wa kilo 50 imeshuka hadi sh. 9,000, sawa na Sh. 180 kwa kilo. Katika masoko na maduka mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam ambayo Nipashe ilitembelea jana, bei ya sembe ilikuwa ikiuzwa kwa kiasi hicho kwa rejareja huku wauzaji wa jumla wakiuza kiroba cha kilo 50 kwa kati ya sh.100,000 na sh.98,000. Ibrahim Omary, mfanyabiashara wa Kariakoo alisema anauza unga wa sembe kwa Sh. 2,400 kwa kuwa hununua kwa bei kubwa kutoka kwa wazalishaji. Alisema kampuni inayojulikana kwa jina la Mkulima huwauzia unga huo kwa Sh. 98,000 na Mama Neema huwauzia kwa sh. 100,000 kwa kiroba cha kilo 50. Kwenye baadhi ya maduka ya kula ya Kinondoni, unga umekuwa ukiuzwa kati ya Sh. 2,200 na Sh. 2,500. Tandika bei ya wastani ni Sh. 2,200, Mwenge Sh. 2,400, Kimara sh. 2,500 na Yombo Vituka sh. 2,200. ...

Mkuu wa Majeshi mstaafu (CDF), Jenerali George Waitara akemea uwindaji haramu Tarime

Mkuu wa Majeshi mstaafu (CDF), Jenerali George Waitara akemea uwindaji haramu Tarime MWENYEKITI wa Bodi ya Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), Mkuu wa Majeshi mstaafu (CDF), Jenerali George Waitara, amewataka wanachi wilayani Tarime, kuachana na uwindaji haramu, badala yake watumie fursa zilizopo kukuza vipato vyao iii kuondokana na umasikini katika ngazi ya familia.  Pia, amewataka wananchi hao watumie fursa hizo kuwekeza katika miradi na biashara mbalimbali katika maeneo jirani na Hifadhi ya Mbuga ya Serengeti, itakayowawezesha kuwaingizia vipato.  Waitara alitoa wito huo mjini Tarime, juzi, alipokutana na baadhi ya wananchi na kubadilishana nao mawazo, wakati akielekea nyumbani kwake k ij iji cha  Itiry o   kusherekea sikukuu ya Pasaka.  Alitoa ushauri kwa watu wenye nia ya kuwekeza katika miradi mbalimbali ya uzalishaji mali wilayani humo, watumie nafasi hiyo iii kukuza na kuendeleza mji waTarime na wilaya hiyo kwa ...