Skip to main content

Wafanyabiashara waishauri Halmashauri kuboresha huduma ya Kodi

Wafanyabiashara waishauri Halmashauri kuboresha huduma ya Kodi



Chama cha wafanyabiashara wenye viwanda na kilimo Tanzania (TCCIA) Mkoa wa Mbeya, kimeshauri Jiji la Mbeya kuangalia namna bora ya kuboresha na kukusanya tozo za kodi ya huduma kutoka kwa wafanyabiashara ili kuboresha kiwango cha huduma.

Mratibu wa TCCIA Mkoa wa Mbeya, Emily Malinza alibainisha hilo juzi jioni kwenye mkutano uliowakutanisha uongozi wa jiji la Mbeya, wadau wa masuala ya kodi na wafanyabiashara kwenye majadiliano ya pamoja kuhusu programu ya kukuza uwekezaji na biashara kwa wajasiriamali wadogo na wa kati kwa jiji hilo.

Malinza alisema wafanyabiashara wamekuwa wakifika TCCIA kuuliza tozo za kodi wanazotozwa na jiji namna zinavyowanufaisha, kwa kukuwa wanatozwa tu lakini hawaoni huduma.

Wafanyabiashara wengi wanauliza tozo wanazolipa zinakokwenda, wakati hakuna huduma wanayoipata kutoka jiji kwa mujibu wa sheria inayoelekeza.

“Sasa jibu ni rahisi tu kwamba kodi inayochukuliwa ni chache kiasi hata matokeo yake hayawezi kuonekana,” alisema Malinza na kuongeza:

“Lakini TCCIA tunaamini kabisa kama kutaboreshwa huduma zitokanazo na tozo hizo, mapato yakaongezeka na hata huduma nyingine ambazo jiji linatoa zitaboreshwa.”

Akichangia katika mkutano huo, ofisa biashara Mkoa wa Mbeya, Stanley Kibakaya alisema licha ya majadiliano hayo kujitikiza zaidi kushusha kiwango vya tozo ili kupata makusanyo mengi zaidi, jiji liwe na mpango mkakati kukuza na kutangaza kujua umuhimu wa vyanzo vingine vya mapato.

“Ukiangalia kwenye ada za leseni za biashara, kila mara wanatangaza umuhimu wa kulipa ada za leseni na kuna mbinu kabisa kama hujalipa hatua zinazotakiwa kuchukuliwa,” alisema.

Naye mhasibu wa Jiji la Mbeya, Andrew Kiyungu alisema tayari wameandaa mpango mkakati wa kuwafikia wafanyabiashara ambao hawasajaliwa kwenye mfumo wa Kodi ya Ongezeko la Thamani (Vat) na wana leseni za biashara.

Kiyungu alisema mkakati huo umegawanywa katika makundi matatu ambayo ni wafanyabiashara wakubwa ambao wamesajaliwa na Vat hawataguswa na punguzo la kodi, watabakia kwenye tozo ya asilimia 0.3.

“Kundi la pili ni wafanyabiashara wa kati ambao wanalipa leseni kuanzia Sh100,000 hadi Sh200,000, menejimenti ya jiji ilipendekeza wakilipa Sh30,000 kwa kila mwezi itakuwa na afya kwa halmashauri na watawafikiwa wengi zaidi kwa bei nafuu na itasaidia kukuza mapato ndani,” alisema.

Alisema kundi la tatu ni wafanyabiashara wadogo ambao wanalipa leseni za biashara kuanzia Sh40,000 hadi Sh80,000, menejimenti ya jiji ilipendekeza kundi hiyo kulipa Sh15,000 kwa mwezi.

Alisema hatua zote hizo ni mkakati wa kuwafikia wafanyabiashara wengi wanaopaswa kulipa tozo ili kukuza mapato yatakayosaidia kuboresha huduma mbalimbali za jamii.

Naye kaimu mkurugenzi wa Jiji la Mbeya, Afrael Manase alisema ili wasonge mbele na kuboresha huduma kwa jamii, lazima sekta binafsi zishirikishwe kila hatua tofauti na hapo watashindwa kumudu utoaji huduma.

Popular posts from this blog

Jinsi ya kutengeneza SABUNI ya kipande YA KUGANDISHA

Jinsi ya kutengeneza SABUNI ya kipande YA KUGANDISHA Utengenezaji wa sabuni hii una njia nyingi Hatua  ya kwanza Chemsha vipimo 7 vya mafuta ya mawese au mafuta ya shea hadi ifikie hatua ya kimiminika chuja na yaweke kwenye chungu cha mfinyanzi au chombo cha plastiki. Hatua ya pili Pima vipimo 5 vya maji baridi kwenye chombo cha plastiki ongeza kipimo 1cha sodium hydroxide kwa uangalifu mkubwa kwenye maji acha hadi mchanganyiko huo uyeyuke. Subiri mchanganyiko wa sodium hydroxide na mafuta ukaribie kupoa. Hatua ya tatu Taratibu ongeza mchanganyiko wa sodium hydroxide kwenye mawese,huku ukikoroga haraka haraka bila kusitisha ukitumia ubao .hii ni njia nzuri zaidi. Njia ya pili Chemsha mafuta kwenye joto la kadiri ya 55C Changanya maji na sodium hydroxide na uache mchanganyiko huu upoe hadi kufikia joto hilohilo. Baada ya kuandaa mchanyiko wako changanya vimiminika hivyo viwili huku ukikoroga kwanguvu sana kadiri uwezavyo, taratibu sabuni itageuka kuwa laini. Kabla...

Mkuu wa Majeshi mstaafu (CDF), Jenerali George Waitara akemea uwindaji haramu Tarime

Mkuu wa Majeshi mstaafu (CDF), Jenerali George Waitara akemea uwindaji haramu Tarime MWENYEKITI wa Bodi ya Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), Mkuu wa Majeshi mstaafu (CDF), Jenerali George Waitara, amewataka wanachi wilayani Tarime, kuachana na uwindaji haramu, badala yake watumie fursa zilizopo kukuza vipato vyao iii kuondokana na umasikini katika ngazi ya familia.  Pia, amewataka wananchi hao watumie fursa hizo kuwekeza katika miradi na biashara mbalimbali katika maeneo jirani na Hifadhi ya Mbuga ya Serengeti, itakayowawezesha kuwaingizia vipato.  Waitara alitoa wito huo mjini Tarime, juzi, alipokutana na baadhi ya wananchi na kubadilishana nao mawazo, wakati akielekea nyumbani kwake k ij iji cha  Itiry o   kusherekea sikukuu ya Pasaka.  Alitoa ushauri kwa watu wenye nia ya kuwekeza katika miradi mbalimbali ya uzalishaji mali wilayani humo, watumie nafasi hiyo iii kukuza na kuendeleza mji waTarime na wilaya hiyo kwa ...

Bei ya unga sasa ni mara 12 ya mfuko wa Simenti

Bei ya unga sasa ni mara 12 ya mfuko wa Simenti WAKATI bei ya unga wa sembe ikipanda mpaka kufikia kuuzwa kati ya Sh. 2,200 na Sh. 2,500 kwa kilo, ile ya mfuko wa saruji wenye uzito wa kilo 50 imeshuka hadi sh. 9,000, sawa na Sh. 180 kwa kilo. Katika masoko na maduka mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam ambayo Nipashe ilitembelea jana, bei ya sembe ilikuwa ikiuzwa kwa kiasi hicho kwa rejareja huku wauzaji wa jumla wakiuza kiroba cha kilo 50 kwa kati ya sh.100,000 na sh.98,000. Ibrahim Omary, mfanyabiashara wa Kariakoo alisema anauza unga wa sembe kwa Sh. 2,400 kwa kuwa hununua kwa bei kubwa kutoka kwa wazalishaji. Alisema kampuni inayojulikana kwa jina la Mkulima huwauzia unga huo kwa Sh. 98,000 na Mama Neema huwauzia kwa sh. 100,000 kwa kiroba cha kilo 50. Kwenye baadhi ya maduka ya kula ya Kinondoni, unga umekuwa ukiuzwa kati ya Sh. 2,200 na Sh. 2,500. Tandika bei ya wastani ni Sh. 2,200, Mwenge Sh. 2,400, Kimara sh. 2,500 na Yombo Vituka sh. 2,200. ...