Skip to main content

Wafanyabiashara waishauri Halmashauri kuboresha huduma ya Kodi

Wafanyabiashara waishauri Halmashauri kuboresha huduma ya Kodi



Chama cha wafanyabiashara wenye viwanda na kilimo Tanzania (TCCIA) Mkoa wa Mbeya, kimeshauri Jiji la Mbeya kuangalia namna bora ya kuboresha na kukusanya tozo za kodi ya huduma kutoka kwa wafanyabiashara ili kuboresha kiwango cha huduma.

Mratibu wa TCCIA Mkoa wa Mbeya, Emily Malinza alibainisha hilo juzi jioni kwenye mkutano uliowakutanisha uongozi wa jiji la Mbeya, wadau wa masuala ya kodi na wafanyabiashara kwenye majadiliano ya pamoja kuhusu programu ya kukuza uwekezaji na biashara kwa wajasiriamali wadogo na wa kati kwa jiji hilo.

Malinza alisema wafanyabiashara wamekuwa wakifika TCCIA kuuliza tozo za kodi wanazotozwa na jiji namna zinavyowanufaisha, kwa kukuwa wanatozwa tu lakini hawaoni huduma.

Wafanyabiashara wengi wanauliza tozo wanazolipa zinakokwenda, wakati hakuna huduma wanayoipata kutoka jiji kwa mujibu wa sheria inayoelekeza.

“Sasa jibu ni rahisi tu kwamba kodi inayochukuliwa ni chache kiasi hata matokeo yake hayawezi kuonekana,” alisema Malinza na kuongeza:

“Lakini TCCIA tunaamini kabisa kama kutaboreshwa huduma zitokanazo na tozo hizo, mapato yakaongezeka na hata huduma nyingine ambazo jiji linatoa zitaboreshwa.”

Akichangia katika mkutano huo, ofisa biashara Mkoa wa Mbeya, Stanley Kibakaya alisema licha ya majadiliano hayo kujitikiza zaidi kushusha kiwango vya tozo ili kupata makusanyo mengi zaidi, jiji liwe na mpango mkakati kukuza na kutangaza kujua umuhimu wa vyanzo vingine vya mapato.

“Ukiangalia kwenye ada za leseni za biashara, kila mara wanatangaza umuhimu wa kulipa ada za leseni na kuna mbinu kabisa kama hujalipa hatua zinazotakiwa kuchukuliwa,” alisema.

Naye mhasibu wa Jiji la Mbeya, Andrew Kiyungu alisema tayari wameandaa mpango mkakati wa kuwafikia wafanyabiashara ambao hawasajaliwa kwenye mfumo wa Kodi ya Ongezeko la Thamani (Vat) na wana leseni za biashara.

Kiyungu alisema mkakati huo umegawanywa katika makundi matatu ambayo ni wafanyabiashara wakubwa ambao wamesajaliwa na Vat hawataguswa na punguzo la kodi, watabakia kwenye tozo ya asilimia 0.3.

“Kundi la pili ni wafanyabiashara wa kati ambao wanalipa leseni kuanzia Sh100,000 hadi Sh200,000, menejimenti ya jiji ilipendekeza wakilipa Sh30,000 kwa kila mwezi itakuwa na afya kwa halmashauri na watawafikiwa wengi zaidi kwa bei nafuu na itasaidia kukuza mapato ndani,” alisema.

Alisema kundi la tatu ni wafanyabiashara wadogo ambao wanalipa leseni za biashara kuanzia Sh40,000 hadi Sh80,000, menejimenti ya jiji ilipendekeza kundi hiyo kulipa Sh15,000 kwa mwezi.

Alisema hatua zote hizo ni mkakati wa kuwafikia wafanyabiashara wengi wanaopaswa kulipa tozo ili kukuza mapato yatakayosaidia kuboresha huduma mbalimbali za jamii.

Naye kaimu mkurugenzi wa Jiji la Mbeya, Afrael Manase alisema ili wasonge mbele na kuboresha huduma kwa jamii, lazima sekta binafsi zishirikishwe kila hatua tofauti na hapo watashindwa kumudu utoaji huduma.

Popular posts from this blog

Jinsi Wachawi Wanavyo Tumia Mafiga Mabichi Ya Mti Wa Mfausiku Kupika Uchawi Wa Kumvuta Kimapenzi Mtu Aliye Mbali.

Jinsi Wachawi Wanavyo Tumia Mafiga Mabichi Ya Mti Wa Mfausiku Kupika Uchawi Wa Kumvuta Kimapenzi Mtu Aliye Mbali. Na. DOKTA  MUNGWA  KABILI …0744 -000  473.  Wachawi  wanaweza  kutumia  uchawi  kumvuta  kimapenzi  mtu  aliye  mbali. Moja  kati  ya  vitu  vinavyo  tumika  katika  uchawi  huu  ni  pamoja  na  mafiga  mabichi  ya  mti  wa  mfausiku  ambayo  hukokwa  kwenye  majani  makavu ya  mgomba  ambayo  hutumika  kama  kuni  au  moto,  kipande  cha  sanda  alichovalishwa  maiti, herufi za  moto,  mti wa hina, pamoja na  vitu  vingine  lukuki. Kufahamu  kuhusu  uchawi wa aina  hii  na  jinsi  ya  kujikinga  nao, fuatilia  sehemu  ya  nne  ya  kitabu “ KITANDA  CHA  SOKWE  MTU” kama  ifuatavyo : SEHEMU  YA  PILI   YA  KITABU  “ KITANDA  CHA  SOKWE  MTU “ Wachawi   wakishindwa  kukutengenezea  kesi  kubwa  basi  waatakufunga  kwenye  kifungo  cha  mapenzi.  Katika  vifungo  vyote anavyo  fungwa  mwanadamu  hakuna  kifungo  kibaya  kama  kifungo  cha  mape

Faida nyingine za kula chungwa

Faida nyingine za kula chungwa Siku kadhaa zilizopita tuliangalia kwa uchache kuhusu faida za kula chungwa hivyo, pia siku ya leo naomba tuendelee kwa kuangalia faida nyingine za kula chungwa. 1. Ulaji wa machungwa husaidia kutibu mapafu. Chungwa pia lina kiasi kikubwa cha Vitamin B6 na Madini ya Chuma (iron), virubisho ambavyo ni muhimu kwa uzalishaji wa seli nyekundu za damu, ambazo hufanya kazi ya kusafirisha hewa ya oksjeni mwilini, hivyo kuwa muhimu kwa kujikinga na ugonjwa wa mapafu. 2. Husaidia kuimarisha mifupa ya meno. Chungwa lina kiasi kingi cha madini ya kalisi (calcium) ambayo ni muhimu kwa uimarishaji wa mifupa na meno. 3. Husaidia kupunguza kiwango cha mafuta mwilini. Virutubisho vilivyomo kwenye chungwa, hasa kwenye maganda yake, hupunguza kiwango cha mafuta mabaya mwilini (bad cholesterol). Hivyo kwa wenye tatizo la lehemu wanashauriwa kula machungwa pamoja na nyama zake. 4. Hupunguza kupatwa magonjwa wa figo. Ulaji wa machungwa mara kwa mara, ukusaid

Je, unajua Binadamu anatakiwa kulala masaa mangapi?

Je, unajua Binadamu anatakiwa kulala masaa mangapi? Unafikili ni wazo zuri kuamka  saa 11 za asubuhi na kufanya mazoezi? Je, ingekuwa vipi kama ungetumia muda huo kulala? Wataalamu wa afya wanashauri kuwa binadamu kwa kwaida anapaswa kulala angalau masaa 7 wakati wa usiku ili kuupa mwili afya bora. Kulala kwa muda mfupi au masaa machache husababisha matatizo ya afya, ikiwa ni pamoja na shinikizo la damu, unyogovu, ugonjwa wa kisukari, na kupunguzwa kinga kukabiliana na chanjo. Ni vyema ukatumia muda wako vizuri mchana ili usiku ukapata muda mwafaka wa kuweza kuupumzisha mwili ili kuepukana na magonjwa hatari ya shinikizo la damu, kisukari na kupungua kwa kinga mwilini. Najua mazingira yetu waafrika ya kimaisha wakati mwingine yanachangamoto nyingi, lakini pale upatapo mwanya kidogo tu, basi utumie yani "kila penye tundu, penyeza lupia" au wawenzetu wazungu wanasema "one chance two goals".