Skip to main content

Wafanyabiashara waishauri Halmashauri kuboresha huduma ya Kodi

Wafanyabiashara waishauri Halmashauri kuboresha huduma ya Kodi



Chama cha wafanyabiashara wenye viwanda na kilimo Tanzania (TCCIA) Mkoa wa Mbeya, kimeshauri Jiji la Mbeya kuangalia namna bora ya kuboresha na kukusanya tozo za kodi ya huduma kutoka kwa wafanyabiashara ili kuboresha kiwango cha huduma.

Mratibu wa TCCIA Mkoa wa Mbeya, Emily Malinza alibainisha hilo juzi jioni kwenye mkutano uliowakutanisha uongozi wa jiji la Mbeya, wadau wa masuala ya kodi na wafanyabiashara kwenye majadiliano ya pamoja kuhusu programu ya kukuza uwekezaji na biashara kwa wajasiriamali wadogo na wa kati kwa jiji hilo.

Malinza alisema wafanyabiashara wamekuwa wakifika TCCIA kuuliza tozo za kodi wanazotozwa na jiji namna zinavyowanufaisha, kwa kukuwa wanatozwa tu lakini hawaoni huduma.

Wafanyabiashara wengi wanauliza tozo wanazolipa zinakokwenda, wakati hakuna huduma wanayoipata kutoka jiji kwa mujibu wa sheria inayoelekeza.

“Sasa jibu ni rahisi tu kwamba kodi inayochukuliwa ni chache kiasi hata matokeo yake hayawezi kuonekana,” alisema Malinza na kuongeza:

“Lakini TCCIA tunaamini kabisa kama kutaboreshwa huduma zitokanazo na tozo hizo, mapato yakaongezeka na hata huduma nyingine ambazo jiji linatoa zitaboreshwa.”

Akichangia katika mkutano huo, ofisa biashara Mkoa wa Mbeya, Stanley Kibakaya alisema licha ya majadiliano hayo kujitikiza zaidi kushusha kiwango vya tozo ili kupata makusanyo mengi zaidi, jiji liwe na mpango mkakati kukuza na kutangaza kujua umuhimu wa vyanzo vingine vya mapato.

“Ukiangalia kwenye ada za leseni za biashara, kila mara wanatangaza umuhimu wa kulipa ada za leseni na kuna mbinu kabisa kama hujalipa hatua zinazotakiwa kuchukuliwa,” alisema.

Naye mhasibu wa Jiji la Mbeya, Andrew Kiyungu alisema tayari wameandaa mpango mkakati wa kuwafikia wafanyabiashara ambao hawasajaliwa kwenye mfumo wa Kodi ya Ongezeko la Thamani (Vat) na wana leseni za biashara.

Kiyungu alisema mkakati huo umegawanywa katika makundi matatu ambayo ni wafanyabiashara wakubwa ambao wamesajaliwa na Vat hawataguswa na punguzo la kodi, watabakia kwenye tozo ya asilimia 0.3.

“Kundi la pili ni wafanyabiashara wa kati ambao wanalipa leseni kuanzia Sh100,000 hadi Sh200,000, menejimenti ya jiji ilipendekeza wakilipa Sh30,000 kwa kila mwezi itakuwa na afya kwa halmashauri na watawafikiwa wengi zaidi kwa bei nafuu na itasaidia kukuza mapato ndani,” alisema.

Alisema kundi la tatu ni wafanyabiashara wadogo ambao wanalipa leseni za biashara kuanzia Sh40,000 hadi Sh80,000, menejimenti ya jiji ilipendekeza kundi hiyo kulipa Sh15,000 kwa mwezi.

Alisema hatua zote hizo ni mkakati wa kuwafikia wafanyabiashara wengi wanaopaswa kulipa tozo ili kukuza mapato yatakayosaidia kuboresha huduma mbalimbali za jamii.

Naye kaimu mkurugenzi wa Jiji la Mbeya, Afrael Manase alisema ili wasonge mbele na kuboresha huduma kwa jamii, lazima sekta binafsi zishirikishwe kila hatua tofauti na hapo watashindwa kumudu utoaji huduma.

Popular posts from this blog

Lema ahoji kushikiliwa mmiliki wa shule ya Lucky Vincent

Lema ahoji kushikiliwa mmiliki wa shule ya Lucky Vincent Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema   Dodoma. Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema amehoji sababu za polisi kumshikilia mmiliki wa shule ya Lucky Vincent badala ya trafiki waliokuwa barabarani siku ya ajali iliyoua watu 35. Akiomba mwongozo wa Spika kuhusu jambo hilo leo, amesema katika eneo husika kuna vizuizi vya ukaguzi vinne lakini trafiki hawakuona kuwa basi hilo lilikuwa kimezidisha watoto na hawakuwa wamefunga mikanda. Amesema badala ya trafiki hao kuchukuliwa hatua, anakamatwa mmiliki ambaye hakuwapo. Akijibu mwongozo huo, Naibu Spika, Dk Tulia Ackson amesema suala hilo halijatokea bungeni.

Jinsi Wachawi Wanavyo Tumia Mafiga Mabichi Ya Mti Wa Mfausiku Kupika Uchawi Wa Kumvuta Kimapenzi Mtu Aliye Mbali.

Jinsi Wachawi Wanavyo Tumia Mafiga Mabichi Ya Mti Wa Mfausiku Kupika Uchawi Wa Kumvuta Kimapenzi Mtu Aliye Mbali. Na. DOKTA  MUNGWA  KABILI …0744 -000  473.  Wachawi  wanaweza  kutumia  uchawi  kumvuta  kimapenzi  mtu  aliye  mbali. Moja  kati  ya  vitu  vinavyo  tumika  katika  uchawi  huu  ni  pamoja  na  mafiga  mabichi  ya  mti  wa  mfausiku  ambayo  hukokwa  kwenye  majani  makavu ya  mgomba  ambayo  hutumika  kama  kuni  au  moto,  kipande  cha  sanda  alichovalishwa  maiti, herufi za  moto,  mti wa hina, pamoja na  vitu  vingine  lukuki. Kufahamu  kuhusu  uchawi wa aina  hii  na  jinsi  ya  kujikinga  nao, fuatilia  sehemu  ya  nne  ya  kitabu “ ...

Bei ya unga sasa ni mara 12 ya mfuko wa Simenti

Bei ya unga sasa ni mara 12 ya mfuko wa Simenti WAKATI bei ya unga wa sembe ikipanda mpaka kufikia kuuzwa kati ya Sh. 2,200 na Sh. 2,500 kwa kilo, ile ya mfuko wa saruji wenye uzito wa kilo 50 imeshuka hadi sh. 9,000, sawa na Sh. 180 kwa kilo. Katika masoko na maduka mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam ambayo Nipashe ilitembelea jana, bei ya sembe ilikuwa ikiuzwa kwa kiasi hicho kwa rejareja huku wauzaji wa jumla wakiuza kiroba cha kilo 50 kwa kati ya sh.100,000 na sh.98,000. Ibrahim Omary, mfanyabiashara wa Kariakoo alisema anauza unga wa sembe kwa Sh. 2,400 kwa kuwa hununua kwa bei kubwa kutoka kwa wazalishaji. Alisema kampuni inayojulikana kwa jina la Mkulima huwauzia unga huo kwa Sh. 98,000 na Mama Neema huwauzia kwa sh. 100,000 kwa kiroba cha kilo 50. Kwenye baadhi ya maduka ya kula ya Kinondoni, unga umekuwa ukiuzwa kati ya Sh. 2,200 na Sh. 2,500. Tandika bei ya wastani ni Sh. 2,200, Mwenge Sh. 2,400, Kimara sh. 2,500 na Yombo Vituka sh. 2,200. ...