Skip to main content

Kujiengua kwa Mtulia haujakishtua chama cha CUF

Kujiengua kwa Mtulia haujakishtua chama cha CUF



Uamuzi wa Maulid Mtulia kujivua ubunge na uanachama haujakishtua chama chake cha CUF, badala yake kimesema bado wengine wawili ambao kingependa waondoke haraka.

Hilo lilisemwa jana na katibu mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad ambaye anaongoza upande mmojapo kati ya mbili zinazokinzana. Upande mwingine unaongozwa na Profesa Ibrahim Lipumba.

Lakini upande wa Profesa Lipumba umesema unatafakari uamuzi huo wa Mtulia ambaye anakuwa mbunge wa pili kujivua uanachama.

Wakati sakata hilo la kuhamahama vyama likipamba moto, aliyekuwa naibu waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana wa Serikali ya Awamu ya Nne, Makongoro Mahanga amesema amekuwa akifuatwa na watu tofauti ambao “pengine hawafahamiani” wakimshawishi arudi CCM, lakini amesema kamwe hataondoka Chadema.

Hamahama ya wanasiasa imesababisha baadhi ya kata kufanya uchaguzi mdogo kujaza nafasi zilizoachwa wazi na madiwani waliohamia CCM, huku jimbo moja likitarajiwa kupata mbunge mpya Januari 13 na sasa Kinondoni imekuwa wazi baada ya Mtulia kujiuzulu juzi.

Hayo yakielezwa, mwenyekiti wa CUF anayetambuliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Profesa Lipumba amesema wanatafakari uamuzi wa Mtulia kujivua ubunge ghafla.

Hata hivyo, naibu katibu mkuu wa CUF (Zanzibar), Nassor Ahmed Mazrui aliliambia gazeti hili kwa njia ya simu jana kuwa, Mtulia ni mmoja wa wabunge watatu wanaomuunga mkono Profesa Lipumba.

“Hatukutarajia kama Mtulia ataondoka wakati huu, bali tulijua ataendelea kudumu. Lakini kama ameondoka ni faraja kwetu kwa sababu katika mipango yetu tulishamuondoa,” alisema Mazrui.

“Tunawaombea dua wale wawili waliobaki waondoke hata leo kwa sababu kuendelea kukaa kwao ndani ya CUF ni kukidhoofisha chama hiki.”

Mazrui aliwataka wabunge kutoshangaa endapo wenzao hao watatangaza kujiuzulu nafasi zao akidai kuna mipango inaendelea kupangwa ili kufanikisha mchakato huo.

“Narudia tena na waondoke, tena waondoke haraka. Ninawahakikishia wana CUF kuwa chama hiki kipo imara na wasiwe na hofu,” alisema Mazrui.

Alisema CUF ni taasisi imara na kati ya wabunge 40, watatu alidai wamekuwa wakikivuruga chama hicho kwa kushirikiana na Profesa Lipumba.

Akizungumzia kuondoka kwa Mtulia, alisema wakati mwingine akifa mgonjwa uliyemuuguza muda mrefu unamshukuru Mungu.

“Tunamshukuru Mungu maana tumeuguza vya kutosha. Haikuwa bahati yetu,” alisema.

Naye Profesa Lipumba alisema kamati ya utendaji ya CUF itakutana kutafakari.

“Siwezi kusema lolote kwa sasa. Bado natafakari kwa sababu nimemtafuta mhusika (Mtulia) sijampata hadi sasa. Kwa kweli imekuwa ghafla na hakuwahi kunidokezea kwamba atahama,” alisema.

“Kamati ya utendaji itakutana kujadiliana kuhusu suala hili. Naomba uwe mvumilivu tunahitaji kujua nini chanzo cha yeye kuondoka, kisha tutatoa taarifa kwa vyombo vya habari.”

Hamidu Bobali, mwenyekiti wa Jumuiya Vijana wa CUF (JuviCUF), ambayo Mtulia alikuwa naibu katibu mkuu alisema kitendo kilichofanywa na mbunge huyo kimemshushia hadhi.

Alimtaka Mtulia akumbuke namna ambavyo watu walipambana hadi akaibuka kidedea katika ubunge wakati wa Uchaguzi Mkuu mwaka 2015.

“Tulianza kumpigania ndani ya CUF, hivi mliweza kufikiri kama Mtulia angemshinda (Abdul) Kambaya? Kambaya alikuwa na nguvu na kila sifa, lakini JuviCUF tulimpigania kijana mwenzetu ili ateuliwe kwenye kura ya maoni, ili agombee jimbo lakini matokeo ndiyo haya,” alisema Bobali ambaye pia ni mbunge wa Mchinga mkoani Lindi.

Barua ya kujiuzulu Mtulia

Katika taarifa yake ya kujiuzulu, Mtulia alitoa sababu zinazolingana na wanachama wengine waliohamia CCM, akisema chama hicho kimefanya mambo mengi ambayo wapinzani waliyaahidi.

“Kwa kuwa nia yangu ni kuwatumikia wananchi, sioni sababu ya kuendelea kuwa upinzani na badala yake nimeona ni vyema niungane na juhudi za Serikali kwa kumuunga mkono Rais Magufuli katika kuwaletea wananchi maendeleo na kukabiliana na kero mbalimbali,” alisema.

Aliwashukuru wananchi wa Kinondoni kwa kumpa dhamana ya ubunge katika Uchaguzi Mkuu uliopita na kuwaahidi kuwa yupo tayari kuendelea kushirikiana nao. Hadi jana, katibu wa Bunge, Stephen Kagaigai alikuwa hajapokea barua ya Mtulia kuhusu kujiuzulu kwake.

Dk Mahanga adai CCM inamsaka

Katika hatua nyingine, Dk Mahanga ambaye aliwahi kuwa naibu waziri kwa takriban miaka kumi, amedai kufuatwa na watu tofauti wanaomshawishi arejea CCM.

Dk Mahanga ambaye alihamia Chadema Agosti 2, 2015, baada ya kushindwa katika kura za maoni ya kuwania ubunge wa Segerea, alisema alijitoa CCM kwa sababu utaratibu uliotumika haukuwa sahihi na uligubikwa na vitendo vya rushwa na njama zilizofanywa na viongozi wa kitaifa kuhakikisha anaondolewa, lakini sasa wanamfuata.

“Siwezi kuwataja ni akina nani, wala idadi yao na mara ngapi wamekuja.  Ila umma ujue wameshakuja mara kadhaa  kunishawishi na sidhani kama wanajuana kuwa wanatumwa na kwenda kwa  mtu mmoja,” alisema Dk Mahanga.

“Nawaambia hivi sirudi huko. Huwa ninaishi kwa ninachokiamini na hakuna kinachoweza kunishawishi kubadili imani na dhamira yangu ya Agosti 2 mwaka 2015.”

Kabla ya kuzungumza na gazeti hili, Dk Mahanga aliandika katika ukurasa wake wa Facebook kuhusu harakati hizo.

“Imani yangu, utu wangu na msimamo wangu huwa hauna bei. Kamwe sitorudi CCM acheni kuhangaika,” aliandika Dk Mahanga katika ukurasa huo.

 Mwanasiasa huyo alijifananisha na kiongozi wa upinzani nchini Kenya, Raila Odinga akisema hatabadili msimamo.

Pia alishangaa baadhi ya watu wanaotoka upinzani kwenda CCM wakidai kuridhishwa na utendaji kazi wa Rais Magufuli na kuunga mkono jitihada za Serikali wakati hali ya maisha ni ngumu kwa Watanzania.

Popular posts from this blog

Jinsi ya kutengeneza SABUNI ya kipande YA KUGANDISHA

Jinsi ya kutengeneza SABUNI ya kipande YA KUGANDISHA Utengenezaji wa sabuni hii una njia nyingi Hatua  ya kwanza Chemsha vipimo 7 vya mafuta ya mawese au mafuta ya shea hadi ifikie hatua ya kimiminika chuja na yaweke kwenye chungu cha mfinyanzi au chombo cha plastiki. Hatua ya pili Pima vipimo 5 vya maji baridi kwenye chombo cha plastiki ongeza kipimo 1cha sodium hydroxide kwa uangalifu mkubwa kwenye maji acha hadi mchanganyiko huo uyeyuke. Subiri mchanganyiko wa sodium hydroxide na mafuta ukaribie kupoa. Hatua ya tatu Taratibu ongeza mchanganyiko wa sodium hydroxide kwenye mawese,huku ukikoroga haraka haraka bila kusitisha ukitumia ubao .hii ni njia nzuri zaidi. Njia ya pili Chemsha mafuta kwenye joto la kadiri ya 55C Changanya maji na sodium hydroxide na uache mchanganyiko huu upoe hadi kufikia joto hilohilo. Baada ya kuandaa mchanyiko wako changanya vimiminika hivyo viwili huku ukikoroga kwanguvu sana kadiri uwezavyo, taratibu sabuni itageuka kuwa laini. Kabla...

Mkuu wa Majeshi mstaafu (CDF), Jenerali George Waitara akemea uwindaji haramu Tarime

Mkuu wa Majeshi mstaafu (CDF), Jenerali George Waitara akemea uwindaji haramu Tarime MWENYEKITI wa Bodi ya Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), Mkuu wa Majeshi mstaafu (CDF), Jenerali George Waitara, amewataka wanachi wilayani Tarime, kuachana na uwindaji haramu, badala yake watumie fursa zilizopo kukuza vipato vyao iii kuondokana na umasikini katika ngazi ya familia.  Pia, amewataka wananchi hao watumie fursa hizo kuwekeza katika miradi na biashara mbalimbali katika maeneo jirani na Hifadhi ya Mbuga ya Serengeti, itakayowawezesha kuwaingizia vipato.  Waitara alitoa wito huo mjini Tarime, juzi, alipokutana na baadhi ya wananchi na kubadilishana nao mawazo, wakati akielekea nyumbani kwake k ij iji cha  Itiry o   kusherekea sikukuu ya Pasaka.  Alitoa ushauri kwa watu wenye nia ya kuwekeza katika miradi mbalimbali ya uzalishaji mali wilayani humo, watumie nafasi hiyo iii kukuza na kuendeleza mji waTarime na wilaya hiyo kwa ...

SADC YALIPONGEZA BARAZA LA USALAMA LA UN KWA KUONGEZA MUDA KWA MISHENI YA ULINZI DRC

SADC YALIPONGEZA BARAZA LA USALAMA LA UN KWA KUONGEZA MUDA KWA MISHENI YA ULINZI DRC 1 2 3 4 5 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) kuhusu mkutano wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa uliofanyika New York, Marekani na kupitisha Azimio la kuongeza muda kwa vikosi vya usalama vilivyopo DRC. Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy. Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza Mhe. Mahiga (hayupo pichani). Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mwenyekiti wa Kamati ya Mawaziri ya Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (Mb). akihutubia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa Jijini New York, Marekani. TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ambaye pia ni Mwenyekiti wa...