Skip to main content

Kujiengua kwa Mtulia haujakishtua chama cha CUF

Kujiengua kwa Mtulia haujakishtua chama cha CUF



Uamuzi wa Maulid Mtulia kujivua ubunge na uanachama haujakishtua chama chake cha CUF, badala yake kimesema bado wengine wawili ambao kingependa waondoke haraka.

Hilo lilisemwa jana na katibu mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad ambaye anaongoza upande mmojapo kati ya mbili zinazokinzana. Upande mwingine unaongozwa na Profesa Ibrahim Lipumba.

Lakini upande wa Profesa Lipumba umesema unatafakari uamuzi huo wa Mtulia ambaye anakuwa mbunge wa pili kujivua uanachama.

Wakati sakata hilo la kuhamahama vyama likipamba moto, aliyekuwa naibu waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana wa Serikali ya Awamu ya Nne, Makongoro Mahanga amesema amekuwa akifuatwa na watu tofauti ambao “pengine hawafahamiani” wakimshawishi arudi CCM, lakini amesema kamwe hataondoka Chadema.

Hamahama ya wanasiasa imesababisha baadhi ya kata kufanya uchaguzi mdogo kujaza nafasi zilizoachwa wazi na madiwani waliohamia CCM, huku jimbo moja likitarajiwa kupata mbunge mpya Januari 13 na sasa Kinondoni imekuwa wazi baada ya Mtulia kujiuzulu juzi.

Hayo yakielezwa, mwenyekiti wa CUF anayetambuliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Profesa Lipumba amesema wanatafakari uamuzi wa Mtulia kujivua ubunge ghafla.

Hata hivyo, naibu katibu mkuu wa CUF (Zanzibar), Nassor Ahmed Mazrui aliliambia gazeti hili kwa njia ya simu jana kuwa, Mtulia ni mmoja wa wabunge watatu wanaomuunga mkono Profesa Lipumba.

“Hatukutarajia kama Mtulia ataondoka wakati huu, bali tulijua ataendelea kudumu. Lakini kama ameondoka ni faraja kwetu kwa sababu katika mipango yetu tulishamuondoa,” alisema Mazrui.

“Tunawaombea dua wale wawili waliobaki waondoke hata leo kwa sababu kuendelea kukaa kwao ndani ya CUF ni kukidhoofisha chama hiki.”

Mazrui aliwataka wabunge kutoshangaa endapo wenzao hao watatangaza kujiuzulu nafasi zao akidai kuna mipango inaendelea kupangwa ili kufanikisha mchakato huo.

“Narudia tena na waondoke, tena waondoke haraka. Ninawahakikishia wana CUF kuwa chama hiki kipo imara na wasiwe na hofu,” alisema Mazrui.

Alisema CUF ni taasisi imara na kati ya wabunge 40, watatu alidai wamekuwa wakikivuruga chama hicho kwa kushirikiana na Profesa Lipumba.

Akizungumzia kuondoka kwa Mtulia, alisema wakati mwingine akifa mgonjwa uliyemuuguza muda mrefu unamshukuru Mungu.

“Tunamshukuru Mungu maana tumeuguza vya kutosha. Haikuwa bahati yetu,” alisema.

Naye Profesa Lipumba alisema kamati ya utendaji ya CUF itakutana kutafakari.

“Siwezi kusema lolote kwa sasa. Bado natafakari kwa sababu nimemtafuta mhusika (Mtulia) sijampata hadi sasa. Kwa kweli imekuwa ghafla na hakuwahi kunidokezea kwamba atahama,” alisema.

“Kamati ya utendaji itakutana kujadiliana kuhusu suala hili. Naomba uwe mvumilivu tunahitaji kujua nini chanzo cha yeye kuondoka, kisha tutatoa taarifa kwa vyombo vya habari.”

Hamidu Bobali, mwenyekiti wa Jumuiya Vijana wa CUF (JuviCUF), ambayo Mtulia alikuwa naibu katibu mkuu alisema kitendo kilichofanywa na mbunge huyo kimemshushia hadhi.

Alimtaka Mtulia akumbuke namna ambavyo watu walipambana hadi akaibuka kidedea katika ubunge wakati wa Uchaguzi Mkuu mwaka 2015.

“Tulianza kumpigania ndani ya CUF, hivi mliweza kufikiri kama Mtulia angemshinda (Abdul) Kambaya? Kambaya alikuwa na nguvu na kila sifa, lakini JuviCUF tulimpigania kijana mwenzetu ili ateuliwe kwenye kura ya maoni, ili agombee jimbo lakini matokeo ndiyo haya,” alisema Bobali ambaye pia ni mbunge wa Mchinga mkoani Lindi.

Barua ya kujiuzulu Mtulia

Katika taarifa yake ya kujiuzulu, Mtulia alitoa sababu zinazolingana na wanachama wengine waliohamia CCM, akisema chama hicho kimefanya mambo mengi ambayo wapinzani waliyaahidi.

“Kwa kuwa nia yangu ni kuwatumikia wananchi, sioni sababu ya kuendelea kuwa upinzani na badala yake nimeona ni vyema niungane na juhudi za Serikali kwa kumuunga mkono Rais Magufuli katika kuwaletea wananchi maendeleo na kukabiliana na kero mbalimbali,” alisema.

Aliwashukuru wananchi wa Kinondoni kwa kumpa dhamana ya ubunge katika Uchaguzi Mkuu uliopita na kuwaahidi kuwa yupo tayari kuendelea kushirikiana nao. Hadi jana, katibu wa Bunge, Stephen Kagaigai alikuwa hajapokea barua ya Mtulia kuhusu kujiuzulu kwake.

Dk Mahanga adai CCM inamsaka

Katika hatua nyingine, Dk Mahanga ambaye aliwahi kuwa naibu waziri kwa takriban miaka kumi, amedai kufuatwa na watu tofauti wanaomshawishi arejea CCM.

Dk Mahanga ambaye alihamia Chadema Agosti 2, 2015, baada ya kushindwa katika kura za maoni ya kuwania ubunge wa Segerea, alisema alijitoa CCM kwa sababu utaratibu uliotumika haukuwa sahihi na uligubikwa na vitendo vya rushwa na njama zilizofanywa na viongozi wa kitaifa kuhakikisha anaondolewa, lakini sasa wanamfuata.

“Siwezi kuwataja ni akina nani, wala idadi yao na mara ngapi wamekuja.  Ila umma ujue wameshakuja mara kadhaa  kunishawishi na sidhani kama wanajuana kuwa wanatumwa na kwenda kwa  mtu mmoja,” alisema Dk Mahanga.

“Nawaambia hivi sirudi huko. Huwa ninaishi kwa ninachokiamini na hakuna kinachoweza kunishawishi kubadili imani na dhamira yangu ya Agosti 2 mwaka 2015.”

Kabla ya kuzungumza na gazeti hili, Dk Mahanga aliandika katika ukurasa wake wa Facebook kuhusu harakati hizo.

“Imani yangu, utu wangu na msimamo wangu huwa hauna bei. Kamwe sitorudi CCM acheni kuhangaika,” aliandika Dk Mahanga katika ukurasa huo.

 Mwanasiasa huyo alijifananisha na kiongozi wa upinzani nchini Kenya, Raila Odinga akisema hatabadili msimamo.

Pia alishangaa baadhi ya watu wanaotoka upinzani kwenda CCM wakidai kuridhishwa na utendaji kazi wa Rais Magufuli na kuunga mkono jitihada za Serikali wakati hali ya maisha ni ngumu kwa Watanzania.

Popular posts from this blog

Jinsi Wachawi Wanavyo Tumia Mafiga Mabichi Ya Mti Wa Mfausiku Kupika Uchawi Wa Kumvuta Kimapenzi Mtu Aliye Mbali.

Jinsi Wachawi Wanavyo Tumia Mafiga Mabichi Ya Mti Wa Mfausiku Kupika Uchawi Wa Kumvuta Kimapenzi Mtu Aliye Mbali. Na. DOKTA  MUNGWA  KABILI …0744 -000  473.  Wachawi  wanaweza  kutumia  uchawi  kumvuta  kimapenzi  mtu  aliye  mbali. Moja  kati  ya  vitu  vinavyo  tumika  katika  uchawi  huu  ni  pamoja  na  mafiga  mabichi  ya  mti  wa  mfausiku  ambayo  hukokwa  kwenye  majani  makavu ya  mgomba  ambayo  hutumika  kama  kuni  au  moto,  kipande  cha  sanda  alichovalishwa  maiti, herufi za  moto,  mti wa hina, pamoja na  vitu  vingine  lukuki. Kufahamu  kuhusu  uchawi wa aina  hii  na  jinsi  ya  kujikinga  nao, fuatilia  sehemu  ya  nne  ya  kitabu “ KITANDA  CHA  SOKWE  MTU” kama  ifuatavyo : SEHEMU  YA  PILI   YA  KITABU  “ KITANDA  CHA  SOKWE  MTU “ Wachawi   wakishindwa  kukutengenezea  kesi  kubwa  basi  waatakufunga  kwenye  kifungo  cha  mapenzi.  Katika  vifungo  vyote anavyo  fungwa  mwanadamu  hakuna  kifungo  kibaya  kama  kifungo  cha  mape

Faida nyingine za kula chungwa

Faida nyingine za kula chungwa Siku kadhaa zilizopita tuliangalia kwa uchache kuhusu faida za kula chungwa hivyo, pia siku ya leo naomba tuendelee kwa kuangalia faida nyingine za kula chungwa. 1. Ulaji wa machungwa husaidia kutibu mapafu. Chungwa pia lina kiasi kikubwa cha Vitamin B6 na Madini ya Chuma (iron), virubisho ambavyo ni muhimu kwa uzalishaji wa seli nyekundu za damu, ambazo hufanya kazi ya kusafirisha hewa ya oksjeni mwilini, hivyo kuwa muhimu kwa kujikinga na ugonjwa wa mapafu. 2. Husaidia kuimarisha mifupa ya meno. Chungwa lina kiasi kingi cha madini ya kalisi (calcium) ambayo ni muhimu kwa uimarishaji wa mifupa na meno. 3. Husaidia kupunguza kiwango cha mafuta mwilini. Virutubisho vilivyomo kwenye chungwa, hasa kwenye maganda yake, hupunguza kiwango cha mafuta mabaya mwilini (bad cholesterol). Hivyo kwa wenye tatizo la lehemu wanashauriwa kula machungwa pamoja na nyama zake. 4. Hupunguza kupatwa magonjwa wa figo. Ulaji wa machungwa mara kwa mara, ukusaid

Je, unajua Binadamu anatakiwa kulala masaa mangapi?

Je, unajua Binadamu anatakiwa kulala masaa mangapi? Unafikili ni wazo zuri kuamka  saa 11 za asubuhi na kufanya mazoezi? Je, ingekuwa vipi kama ungetumia muda huo kulala? Wataalamu wa afya wanashauri kuwa binadamu kwa kwaida anapaswa kulala angalau masaa 7 wakati wa usiku ili kuupa mwili afya bora. Kulala kwa muda mfupi au masaa machache husababisha matatizo ya afya, ikiwa ni pamoja na shinikizo la damu, unyogovu, ugonjwa wa kisukari, na kupunguzwa kinga kukabiliana na chanjo. Ni vyema ukatumia muda wako vizuri mchana ili usiku ukapata muda mwafaka wa kuweza kuupumzisha mwili ili kuepukana na magonjwa hatari ya shinikizo la damu, kisukari na kupungua kwa kinga mwilini. Najua mazingira yetu waafrika ya kimaisha wakati mwingine yanachangamoto nyingi, lakini pale upatapo mwanya kidogo tu, basi utumie yani "kila penye tundu, penyeza lupia" au wawenzetu wazungu wanasema "one chance two goals".