Skip to main content

Julio ailipua Simba

Julio ailipua Simba



Kocha Jamhuri Kihwelu Julio amesema kwa sasa Simba wanavuna walichokipanda kuhusu usajili wa Shomari Kapombe ambaye tangu amesajiliwa na klabu hiyo bado hajacheza mechi yoyote wala kufanya mazoezi ya pamoja na wachezaji wengine kutokana na kuuguza majeraha.

Jana Jumatatu Nov 13, 2017 alisikika Mwenyekiti wa kamati ya usajili Simba Zacharia Hans Poppe akisema, Kapombe anatakiwa kuchagua kucheza au kutocheza lakini klabu hiyo haitaendelea kumlipa mshahara huku akiwa hafanyi kazi.

“Simba wanavuna walichopanda, wakati Simba wanacheza ligi wakiwa katika kumalizia mzunguko wa pili wa msimu uliopita, mimi nilipata bahati ya kuwa mmoja ya wachezaji au kocha wa zamani wa Simba nikitunguza na timu kwa ajili yak u-motivate wachezaji na kuwajenga kisaikolojia ili tuweze kufanikiwa nadhani matanda yalionekana kiasi kwamba hata Mavugo ambaye alionekana yupo chini lakini nilijaribu kukaa nae na akaanza kufunga”amesikika Julio kupitia kituo kimoja cha redio.

“Kwa upande wa usajili nilikuwa naulizwa Julio kama kocha nikiwa na wenzangu ambao tulikuwa tunashirikiana lakini kuna watu mpira hawaju ndio wanaivuruga Simba, wanajidai wanamapenzi na timu lakini hawajui mpira ndio wanaiharibu Simba kwenye usajili. Mkikaa kupanga mambo ya wachezaji ukitaja mchezaji ambaye hawamtaki wanahamia ndani lakini watu wote mpira hawajui.”

“Sitaki kuwa mnafiki, kuhusu suala la Kapombe nilikuwepo, wakati wanajadili nilisema hapana labda asajiliwe mwakani lakini alikuja kwa maslahi binafsi. Mimi ndiye nilimfanya Kapombe acheze mpira nimemtoa timu ya Polisi Morogoro akiwa kwenye mashindano ya daraja la kwanza, nilipewa ruhusa hiyo na Msafiri Mgoyi akiwa ni msimamizi wa timu za vijana za taifa wakati huo nilikuwa kocha msaidi wa timu ya U17 chini ya Kim Polsen huku nikiwa kocha mkuu wa timu ya taifa ya U23.”

“Kwa majeraha aliyokuwa nayo (Kapombe) hakustahili kucheza Simba lakini watu walikuwa wanamtaka kwa sababu ya ubishi wa kutojua mpira, wangekuwa wanatumia waalimu au scouting wanaojua leo wasingefika hapa kwa kutaka kumdhalilisha Kapombe kwa hiyo hili ni zao la mbegu waliyopanda.”

Popular posts from this blog

Lema ahoji kushikiliwa mmiliki wa shule ya Lucky Vincent

Lema ahoji kushikiliwa mmiliki wa shule ya Lucky Vincent Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema   Dodoma. Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema amehoji sababu za polisi kumshikilia mmiliki wa shule ya Lucky Vincent badala ya trafiki waliokuwa barabarani siku ya ajali iliyoua watu 35. Akiomba mwongozo wa Spika kuhusu jambo hilo leo, amesema katika eneo husika kuna vizuizi vya ukaguzi vinne lakini trafiki hawakuona kuwa basi hilo lilikuwa kimezidisha watoto na hawakuwa wamefunga mikanda. Amesema badala ya trafiki hao kuchukuliwa hatua, anakamatwa mmiliki ambaye hakuwapo. Akijibu mwongozo huo, Naibu Spika, Dk Tulia Ackson amesema suala hilo halijatokea bungeni.

Jinsi Wachawi Wanavyo Tumia Mafiga Mabichi Ya Mti Wa Mfausiku Kupika Uchawi Wa Kumvuta Kimapenzi Mtu Aliye Mbali.

Jinsi Wachawi Wanavyo Tumia Mafiga Mabichi Ya Mti Wa Mfausiku Kupika Uchawi Wa Kumvuta Kimapenzi Mtu Aliye Mbali. Na. DOKTA  MUNGWA  KABILI …0744 -000  473.  Wachawi  wanaweza  kutumia  uchawi  kumvuta  kimapenzi  mtu  aliye  mbali. Moja  kati  ya  vitu  vinavyo  tumika  katika  uchawi  huu  ni  pamoja  na  mafiga  mabichi  ya  mti  wa  mfausiku  ambayo  hukokwa  kwenye  majani  makavu ya  mgomba  ambayo  hutumika  kama  kuni  au  moto,  kipande  cha  sanda  alichovalishwa  maiti, herufi za  moto,  mti wa hina, pamoja na  vitu  vingine  lukuki. Kufahamu  kuhusu  uchawi wa aina  hii  na  jinsi  ya  kujikinga  nao, fuatilia  sehemu  ya  nne  ya  kitabu “ ...

Bei ya unga sasa ni mara 12 ya mfuko wa Simenti

Bei ya unga sasa ni mara 12 ya mfuko wa Simenti WAKATI bei ya unga wa sembe ikipanda mpaka kufikia kuuzwa kati ya Sh. 2,200 na Sh. 2,500 kwa kilo, ile ya mfuko wa saruji wenye uzito wa kilo 50 imeshuka hadi sh. 9,000, sawa na Sh. 180 kwa kilo. Katika masoko na maduka mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam ambayo Nipashe ilitembelea jana, bei ya sembe ilikuwa ikiuzwa kwa kiasi hicho kwa rejareja huku wauzaji wa jumla wakiuza kiroba cha kilo 50 kwa kati ya sh.100,000 na sh.98,000. Ibrahim Omary, mfanyabiashara wa Kariakoo alisema anauza unga wa sembe kwa Sh. 2,400 kwa kuwa hununua kwa bei kubwa kutoka kwa wazalishaji. Alisema kampuni inayojulikana kwa jina la Mkulima huwauzia unga huo kwa Sh. 98,000 na Mama Neema huwauzia kwa sh. 100,000 kwa kiroba cha kilo 50. Kwenye baadhi ya maduka ya kula ya Kinondoni, unga umekuwa ukiuzwa kati ya Sh. 2,200 na Sh. 2,500. Tandika bei ya wastani ni Sh. 2,200, Mwenge Sh. 2,400, Kimara sh. 2,500 na Yombo Vituka sh. 2,200. ...