Skip to main content

Julio ailipua Simba

Julio ailipua Simba



Kocha Jamhuri Kihwelu Julio amesema kwa sasa Simba wanavuna walichokipanda kuhusu usajili wa Shomari Kapombe ambaye tangu amesajiliwa na klabu hiyo bado hajacheza mechi yoyote wala kufanya mazoezi ya pamoja na wachezaji wengine kutokana na kuuguza majeraha.

Jana Jumatatu Nov 13, 2017 alisikika Mwenyekiti wa kamati ya usajili Simba Zacharia Hans Poppe akisema, Kapombe anatakiwa kuchagua kucheza au kutocheza lakini klabu hiyo haitaendelea kumlipa mshahara huku akiwa hafanyi kazi.

“Simba wanavuna walichopanda, wakati Simba wanacheza ligi wakiwa katika kumalizia mzunguko wa pili wa msimu uliopita, mimi nilipata bahati ya kuwa mmoja ya wachezaji au kocha wa zamani wa Simba nikitunguza na timu kwa ajili yak u-motivate wachezaji na kuwajenga kisaikolojia ili tuweze kufanikiwa nadhani matanda yalionekana kiasi kwamba hata Mavugo ambaye alionekana yupo chini lakini nilijaribu kukaa nae na akaanza kufunga”amesikika Julio kupitia kituo kimoja cha redio.

“Kwa upande wa usajili nilikuwa naulizwa Julio kama kocha nikiwa na wenzangu ambao tulikuwa tunashirikiana lakini kuna watu mpira hawaju ndio wanaivuruga Simba, wanajidai wanamapenzi na timu lakini hawajui mpira ndio wanaiharibu Simba kwenye usajili. Mkikaa kupanga mambo ya wachezaji ukitaja mchezaji ambaye hawamtaki wanahamia ndani lakini watu wote mpira hawajui.”

“Sitaki kuwa mnafiki, kuhusu suala la Kapombe nilikuwepo, wakati wanajadili nilisema hapana labda asajiliwe mwakani lakini alikuja kwa maslahi binafsi. Mimi ndiye nilimfanya Kapombe acheze mpira nimemtoa timu ya Polisi Morogoro akiwa kwenye mashindano ya daraja la kwanza, nilipewa ruhusa hiyo na Msafiri Mgoyi akiwa ni msimamizi wa timu za vijana za taifa wakati huo nilikuwa kocha msaidi wa timu ya U17 chini ya Kim Polsen huku nikiwa kocha mkuu wa timu ya taifa ya U23.”

“Kwa majeraha aliyokuwa nayo (Kapombe) hakustahili kucheza Simba lakini watu walikuwa wanamtaka kwa sababu ya ubishi wa kutojua mpira, wangekuwa wanatumia waalimu au scouting wanaojua leo wasingefika hapa kwa kutaka kumdhalilisha Kapombe kwa hiyo hili ni zao la mbegu waliyopanda.”

Popular posts from this blog

Jinsi ya kutengeneza SABUNI ya kipande YA KUGANDISHA

Jinsi ya kutengeneza SABUNI ya kipande YA KUGANDISHA Utengenezaji wa sabuni hii una njia nyingi Hatua  ya kwanza Chemsha vipimo 7 vya mafuta ya mawese au mafuta ya shea hadi ifikie hatua ya kimiminika chuja na yaweke kwenye chungu cha mfinyanzi au chombo cha plastiki. Hatua ya pili Pima vipimo 5 vya maji baridi kwenye chombo cha plastiki ongeza kipimo 1cha sodium hydroxide kwa uangalifu mkubwa kwenye maji acha hadi mchanganyiko huo uyeyuke. Subiri mchanganyiko wa sodium hydroxide na mafuta ukaribie kupoa. Hatua ya tatu Taratibu ongeza mchanganyiko wa sodium hydroxide kwenye mawese,huku ukikoroga haraka haraka bila kusitisha ukitumia ubao .hii ni njia nzuri zaidi. Njia ya pili Chemsha mafuta kwenye joto la kadiri ya 55C Changanya maji na sodium hydroxide na uache mchanganyiko huu upoe hadi kufikia joto hilohilo. Baada ya kuandaa mchanyiko wako changanya vimiminika hivyo viwili huku ukikoroga kwanguvu sana kadiri uwezavyo, taratibu sabuni itageuka kuwa laini. Kabla...

Mkuu wa Majeshi mstaafu (CDF), Jenerali George Waitara akemea uwindaji haramu Tarime

Mkuu wa Majeshi mstaafu (CDF), Jenerali George Waitara akemea uwindaji haramu Tarime MWENYEKITI wa Bodi ya Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), Mkuu wa Majeshi mstaafu (CDF), Jenerali George Waitara, amewataka wanachi wilayani Tarime, kuachana na uwindaji haramu, badala yake watumie fursa zilizopo kukuza vipato vyao iii kuondokana na umasikini katika ngazi ya familia.  Pia, amewataka wananchi hao watumie fursa hizo kuwekeza katika miradi na biashara mbalimbali katika maeneo jirani na Hifadhi ya Mbuga ya Serengeti, itakayowawezesha kuwaingizia vipato.  Waitara alitoa wito huo mjini Tarime, juzi, alipokutana na baadhi ya wananchi na kubadilishana nao mawazo, wakati akielekea nyumbani kwake k ij iji cha  Itiry o   kusherekea sikukuu ya Pasaka.  Alitoa ushauri kwa watu wenye nia ya kuwekeza katika miradi mbalimbali ya uzalishaji mali wilayani humo, watumie nafasi hiyo iii kukuza na kuendeleza mji waTarime na wilaya hiyo kwa ...

Bei ya unga sasa ni mara 12 ya mfuko wa Simenti

Bei ya unga sasa ni mara 12 ya mfuko wa Simenti WAKATI bei ya unga wa sembe ikipanda mpaka kufikia kuuzwa kati ya Sh. 2,200 na Sh. 2,500 kwa kilo, ile ya mfuko wa saruji wenye uzito wa kilo 50 imeshuka hadi sh. 9,000, sawa na Sh. 180 kwa kilo. Katika masoko na maduka mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam ambayo Nipashe ilitembelea jana, bei ya sembe ilikuwa ikiuzwa kwa kiasi hicho kwa rejareja huku wauzaji wa jumla wakiuza kiroba cha kilo 50 kwa kati ya sh.100,000 na sh.98,000. Ibrahim Omary, mfanyabiashara wa Kariakoo alisema anauza unga wa sembe kwa Sh. 2,400 kwa kuwa hununua kwa bei kubwa kutoka kwa wazalishaji. Alisema kampuni inayojulikana kwa jina la Mkulima huwauzia unga huo kwa Sh. 98,000 na Mama Neema huwauzia kwa sh. 100,000 kwa kiroba cha kilo 50. Kwenye baadhi ya maduka ya kula ya Kinondoni, unga umekuwa ukiuzwa kati ya Sh. 2,200 na Sh. 2,500. Tandika bei ya wastani ni Sh. 2,200, Mwenge Sh. 2,400, Kimara sh. 2,500 na Yombo Vituka sh. 2,200. ...