Skip to main content

Julio ailipua Simba

Julio ailipua Simba



Kocha Jamhuri Kihwelu Julio amesema kwa sasa Simba wanavuna walichokipanda kuhusu usajili wa Shomari Kapombe ambaye tangu amesajiliwa na klabu hiyo bado hajacheza mechi yoyote wala kufanya mazoezi ya pamoja na wachezaji wengine kutokana na kuuguza majeraha.

Jana Jumatatu Nov 13, 2017 alisikika Mwenyekiti wa kamati ya usajili Simba Zacharia Hans Poppe akisema, Kapombe anatakiwa kuchagua kucheza au kutocheza lakini klabu hiyo haitaendelea kumlipa mshahara huku akiwa hafanyi kazi.

“Simba wanavuna walichopanda, wakati Simba wanacheza ligi wakiwa katika kumalizia mzunguko wa pili wa msimu uliopita, mimi nilipata bahati ya kuwa mmoja ya wachezaji au kocha wa zamani wa Simba nikitunguza na timu kwa ajili yak u-motivate wachezaji na kuwajenga kisaikolojia ili tuweze kufanikiwa nadhani matanda yalionekana kiasi kwamba hata Mavugo ambaye alionekana yupo chini lakini nilijaribu kukaa nae na akaanza kufunga”amesikika Julio kupitia kituo kimoja cha redio.

“Kwa upande wa usajili nilikuwa naulizwa Julio kama kocha nikiwa na wenzangu ambao tulikuwa tunashirikiana lakini kuna watu mpira hawaju ndio wanaivuruga Simba, wanajidai wanamapenzi na timu lakini hawajui mpira ndio wanaiharibu Simba kwenye usajili. Mkikaa kupanga mambo ya wachezaji ukitaja mchezaji ambaye hawamtaki wanahamia ndani lakini watu wote mpira hawajui.”

“Sitaki kuwa mnafiki, kuhusu suala la Kapombe nilikuwepo, wakati wanajadili nilisema hapana labda asajiliwe mwakani lakini alikuja kwa maslahi binafsi. Mimi ndiye nilimfanya Kapombe acheze mpira nimemtoa timu ya Polisi Morogoro akiwa kwenye mashindano ya daraja la kwanza, nilipewa ruhusa hiyo na Msafiri Mgoyi akiwa ni msimamizi wa timu za vijana za taifa wakati huo nilikuwa kocha msaidi wa timu ya U17 chini ya Kim Polsen huku nikiwa kocha mkuu wa timu ya taifa ya U23.”

“Kwa majeraha aliyokuwa nayo (Kapombe) hakustahili kucheza Simba lakini watu walikuwa wanamtaka kwa sababu ya ubishi wa kutojua mpira, wangekuwa wanatumia waalimu au scouting wanaojua leo wasingefika hapa kwa kutaka kumdhalilisha Kapombe kwa hiyo hili ni zao la mbegu waliyopanda.”

Popular posts from this blog

Jinsi Wachawi Wanavyo Tumia Mafiga Mabichi Ya Mti Wa Mfausiku Kupika Uchawi Wa Kumvuta Kimapenzi Mtu Aliye Mbali.

Jinsi Wachawi Wanavyo Tumia Mafiga Mabichi Ya Mti Wa Mfausiku Kupika Uchawi Wa Kumvuta Kimapenzi Mtu Aliye Mbali. Na. DOKTA  MUNGWA  KABILI …0744 -000  473.  Wachawi  wanaweza  kutumia  uchawi  kumvuta  kimapenzi  mtu  aliye  mbali. Moja  kati  ya  vitu  vinavyo  tumika  katika  uchawi  huu  ni  pamoja  na  mafiga  mabichi  ya  mti  wa  mfausiku  ambayo  hukokwa  kwenye  majani  makavu ya  mgomba  ambayo  hutumika  kama  kuni  au  moto,  kipande  cha  sanda  alichovalishwa  maiti, herufi za  moto,  mti wa hina, pamoja na  vitu  vingine  lukuki. Kufahamu  kuhusu  uchawi wa aina  hii  na  jinsi  ya  kujikinga  nao, fuatilia  sehemu  ya  nne  ya  kitabu “ KITANDA  CHA  SOKWE  MTU” kama  ifuatavyo : SEHEMU  YA  PILI   YA  KITABU  “ KITANDA  CHA  SOKWE  MTU “ Wachawi   wakishindwa  kukutengenezea  kesi  kubwa  basi  waatakufunga  kwenye  kifungo  cha  mapenzi.  Katika  vifungo  vyote anavyo  fungwa  mwanadamu  hakuna  kifungo  kibaya  kama  kifungo  cha  mape

Faida nyingine za kula chungwa

Faida nyingine za kula chungwa Siku kadhaa zilizopita tuliangalia kwa uchache kuhusu faida za kula chungwa hivyo, pia siku ya leo naomba tuendelee kwa kuangalia faida nyingine za kula chungwa. 1. Ulaji wa machungwa husaidia kutibu mapafu. Chungwa pia lina kiasi kikubwa cha Vitamin B6 na Madini ya Chuma (iron), virubisho ambavyo ni muhimu kwa uzalishaji wa seli nyekundu za damu, ambazo hufanya kazi ya kusafirisha hewa ya oksjeni mwilini, hivyo kuwa muhimu kwa kujikinga na ugonjwa wa mapafu. 2. Husaidia kuimarisha mifupa ya meno. Chungwa lina kiasi kingi cha madini ya kalisi (calcium) ambayo ni muhimu kwa uimarishaji wa mifupa na meno. 3. Husaidia kupunguza kiwango cha mafuta mwilini. Virutubisho vilivyomo kwenye chungwa, hasa kwenye maganda yake, hupunguza kiwango cha mafuta mabaya mwilini (bad cholesterol). Hivyo kwa wenye tatizo la lehemu wanashauriwa kula machungwa pamoja na nyama zake. 4. Hupunguza kupatwa magonjwa wa figo. Ulaji wa machungwa mara kwa mara, ukusaid

Je, unajua Binadamu anatakiwa kulala masaa mangapi?

Je, unajua Binadamu anatakiwa kulala masaa mangapi? Unafikili ni wazo zuri kuamka  saa 11 za asubuhi na kufanya mazoezi? Je, ingekuwa vipi kama ungetumia muda huo kulala? Wataalamu wa afya wanashauri kuwa binadamu kwa kwaida anapaswa kulala angalau masaa 7 wakati wa usiku ili kuupa mwili afya bora. Kulala kwa muda mfupi au masaa machache husababisha matatizo ya afya, ikiwa ni pamoja na shinikizo la damu, unyogovu, ugonjwa wa kisukari, na kupunguzwa kinga kukabiliana na chanjo. Ni vyema ukatumia muda wako vizuri mchana ili usiku ukapata muda mwafaka wa kuweza kuupumzisha mwili ili kuepukana na magonjwa hatari ya shinikizo la damu, kisukari na kupungua kwa kinga mwilini. Najua mazingira yetu waafrika ya kimaisha wakati mwingine yanachangamoto nyingi, lakini pale upatapo mwanya kidogo tu, basi utumie yani "kila penye tundu, penyeza lupia" au wawenzetu wazungu wanasema "one chance two goals".