Skip to main content

CCM Wampuuza Lowassa.....Wawataka Wananchi Wasidanganyike na Ahadi

CCM Wampuuza Lowassa.....Wawataka Wananchi Wasidanganyike na Ahadi


Wakazi wa Kata ya Moita wameombwa kumchagua mgombea wa CCM ili wapate maendeleo na kuachana na ahadi alizowapa, Waziri Mkuu mstaafu na mjumbe wa kamati kuu, Chadema, Edward Lowassa.

Lowassa aliyewahi kuwa mbunge wa Monduli ndiye aliyezindua kampeni za udiwani za Chadema katika kata hiyo mwishoni mwa wiki iliyopita na kuwaahidi wananchi kuwa hatawasahau na ataendelea kushirikiana nao, kwani aliwaacha wakiwa tayari wana umeme, maji na shule mbili za kata.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Mkoa wa Arusha, Shaban Mdoe akizungumza katika kampeni eneo la Moita Bwawani, alisema wananchi wasidanganyike.

Mdoe alisema kwamba wakimchagua mgombea wa CCM, Prosper Meyani kero zao zitapatiwa ufumbuzi, ikiwamo kero ya maji na barabara.

“Msidanganywe na Chadema, hawawezi kutatua kero zenu, alikuwepo diwani wao, hadi amejiuzulu, mbunge wa zamani Lowassa hivi sasa hawezi tena kuwasaidia,” alisema.

Awali, aliyekuwa diwani wa kata hiyo na kujiuzulu, Edward Sapunyo alisema aliamua kujiuzulu baada ya kunyimwa ushirikiano na madiwani wa Chadema.

Alisema kila mradi ambao alikuwa anaomba katika kata hiyo alinyimwa na hivyo akaona hana sababu ya kubaki bali arejee CCM.

Kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, Sapunyo ambaye alikuwa mwenyekiti wa halmashauri ya Monduli kupitia CCM, alisema chaguo sahihi katika kata hiyo ni mgombea wa CCM.

Halmashauri ya Monduli hadi sasa inaongozwa na Chadema kutokana na kuwa na madiwani 18 na CCM madiwani tisa.

Popular posts from this blog

Jinsi ya kutengeneza SABUNI ya kipande YA KUGANDISHA

Jinsi ya kutengeneza SABUNI ya kipande YA KUGANDISHA Utengenezaji wa sabuni hii una njia nyingi Hatua  ya kwanza Chemsha vipimo 7 vya mafuta ya mawese au mafuta ya shea hadi ifikie hatua ya kimiminika chuja na yaweke kwenye chungu cha mfinyanzi au chombo cha plastiki. Hatua ya pili Pima vipimo 5 vya maji baridi kwenye chombo cha plastiki ongeza kipimo 1cha sodium hydroxide kwa uangalifu mkubwa kwenye maji acha hadi mchanganyiko huo uyeyuke. Subiri mchanganyiko wa sodium hydroxide na mafuta ukaribie kupoa. Hatua ya tatu Taratibu ongeza mchanganyiko wa sodium hydroxide kwenye mawese,huku ukikoroga haraka haraka bila kusitisha ukitumia ubao .hii ni njia nzuri zaidi. Njia ya pili Chemsha mafuta kwenye joto la kadiri ya 55C Changanya maji na sodium hydroxide na uache mchanganyiko huu upoe hadi kufikia joto hilohilo. Baada ya kuandaa mchanyiko wako changanya vimiminika hivyo viwili huku ukikoroga kwanguvu sana kadiri uwezavyo, taratibu sabuni itageuka kuwa laini. Kabla...

Mkuu wa Majeshi mstaafu (CDF), Jenerali George Waitara akemea uwindaji haramu Tarime

Mkuu wa Majeshi mstaafu (CDF), Jenerali George Waitara akemea uwindaji haramu Tarime MWENYEKITI wa Bodi ya Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), Mkuu wa Majeshi mstaafu (CDF), Jenerali George Waitara, amewataka wanachi wilayani Tarime, kuachana na uwindaji haramu, badala yake watumie fursa zilizopo kukuza vipato vyao iii kuondokana na umasikini katika ngazi ya familia.  Pia, amewataka wananchi hao watumie fursa hizo kuwekeza katika miradi na biashara mbalimbali katika maeneo jirani na Hifadhi ya Mbuga ya Serengeti, itakayowawezesha kuwaingizia vipato.  Waitara alitoa wito huo mjini Tarime, juzi, alipokutana na baadhi ya wananchi na kubadilishana nao mawazo, wakati akielekea nyumbani kwake k ij iji cha  Itiry o   kusherekea sikukuu ya Pasaka.  Alitoa ushauri kwa watu wenye nia ya kuwekeza katika miradi mbalimbali ya uzalishaji mali wilayani humo, watumie nafasi hiyo iii kukuza na kuendeleza mji waTarime na wilaya hiyo kwa ...

Bei ya unga sasa ni mara 12 ya mfuko wa Simenti

Bei ya unga sasa ni mara 12 ya mfuko wa Simenti WAKATI bei ya unga wa sembe ikipanda mpaka kufikia kuuzwa kati ya Sh. 2,200 na Sh. 2,500 kwa kilo, ile ya mfuko wa saruji wenye uzito wa kilo 50 imeshuka hadi sh. 9,000, sawa na Sh. 180 kwa kilo. Katika masoko na maduka mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam ambayo Nipashe ilitembelea jana, bei ya sembe ilikuwa ikiuzwa kwa kiasi hicho kwa rejareja huku wauzaji wa jumla wakiuza kiroba cha kilo 50 kwa kati ya sh.100,000 na sh.98,000. Ibrahim Omary, mfanyabiashara wa Kariakoo alisema anauza unga wa sembe kwa Sh. 2,400 kwa kuwa hununua kwa bei kubwa kutoka kwa wazalishaji. Alisema kampuni inayojulikana kwa jina la Mkulima huwauzia unga huo kwa Sh. 98,000 na Mama Neema huwauzia kwa sh. 100,000 kwa kiroba cha kilo 50. Kwenye baadhi ya maduka ya kula ya Kinondoni, unga umekuwa ukiuzwa kati ya Sh. 2,200 na Sh. 2,500. Tandika bei ya wastani ni Sh. 2,200, Mwenge Sh. 2,400, Kimara sh. 2,500 na Yombo Vituka sh. 2,200. ...