Skip to main content

Bunge lapinga ongezeko la ushuru vinywaji baridi

Bunge lapinga ongezeko la ushuru vinywaji baridi

Serikali  imewasilisha bungeni Muswada wa Sheria ya Fedha wa Mwaka 2017 wenye marekebisho ya sheria 15 ikiwamo Sheria ya Ushuru wa Bidhaa.

Kwa mujibu wa marekebisho hayo, ushuru wa bidhaa kwenye vinywaji baridi umeongezeka kutoka Sh 58 kwa lita hadi Sh 61 ikiwa ni sawa na ongezeko la shilingi tatu. 

Aidha, Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti imepinga ongezeko hilo la shilingi tatu kwenye vinywaji baridi ikisema hatua hiyo itazorotesha ukuaji wa viwanda nchini.

Akiwasilisha Muswada huo jana, Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango alisema sheria hizo zinahusu masuala ya fedha, kodi, ushuru, tozo, na mawasiliano ili kupunguza, kurekebisha, au kufuta viwango vya kodi, ushuru, ada na tozo mbalimbali ili kuboresha ukusanyaji wa kodi.

Dk Mpango alisema marekebisho hayo yamezingatia mkakati wa taifa wa kukuza uchumi wa viwanda, na kwamba kiwango cha ushuru kwa baadhi ya bidhaa zinazozalishwa nchini kimepunguzwa au kubakia ilivyo sasa.

Mengine aliyozungumzia ni ongezeko la ushuru katika mafuta ya petroli, dizeli na mafuta ya taa kwa Sh 40, Sheria ya Benki Kuu inayorekebishwa ili kuweka sharti la ulazima kwa taasisi za serikali kufungua akaunti na kuhifadhi mapato na fedha Benki Kuu.

Alisema katika marekebisho hayo, pia ipo Sheria ya Posta na Mawasiliano ya Kielektroniki ili kutoa wigo mpana kupanua wigo wa mauzo ya hisa za asilimia 25 zitakazouzwa na kampuni ya mawasiliano kwenye soko la hisa kwa kutoa fursa kwa Watanzania walio ndani na nje ya nchi, taasisi ya Kitanzania, kampuni zinazomilikiwa kwa pamoja baina ya Watanzania na raia wa nje, raia, kampuni na taasisi za nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki au raia na kampuni kutoka nchi nyingine.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bajeti, Hawa Ghasia alipinga kuongezeka ushuru kwa vinywaji baridi akisema hatua hiyo itapunguza uzalishaji. 

Alitolea mfano hatua ya serikali ya kutoongeza kodi kwenye bidhaa hiyo kwa miaka mitatu iliyopita kuwa uzalishaji na uchumi uliongezeka na serikali kupata kodi; huku akipendekeza tozo 14 zilizobakia katika shule na vyuo binafsi zizidi kuondolewa ili wapunguzia gharama.

Mbunge wa Vwawa, Japhet Hasunga (CCM), alisema muswada huo umejumuisha asilimia 80 ya mapendekezo ya wabunge na kutaka asilimia 15 ya fedha ambazo mashirikia ya umma hutakiwa kuchangia mfuko mkuu wa serikali, zisitozwe kodi kwani mashirika ya umma yanalipa kodi mara mbili.

Mbunge wa Nzega Mjini, Hussein Bashe (CCM) alipendekeza kuongezwa tozo ya asilimia sita hadi 12 kwenye mapato yatokanayo na michezo ya kubahatisha, na asilimia nane hadi 20 kwenye zawadi na pia kuongeza tozo ya leseni.

Popular posts from this blog

Lema ahoji kushikiliwa mmiliki wa shule ya Lucky Vincent

Lema ahoji kushikiliwa mmiliki wa shule ya Lucky Vincent Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema   Dodoma. Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema amehoji sababu za polisi kumshikilia mmiliki wa shule ya Lucky Vincent badala ya trafiki waliokuwa barabarani siku ya ajali iliyoua watu 35. Akiomba mwongozo wa Spika kuhusu jambo hilo leo, amesema katika eneo husika kuna vizuizi vya ukaguzi vinne lakini trafiki hawakuona kuwa basi hilo lilikuwa kimezidisha watoto na hawakuwa wamefunga mikanda. Amesema badala ya trafiki hao kuchukuliwa hatua, anakamatwa mmiliki ambaye hakuwapo. Akijibu mwongozo huo, Naibu Spika, Dk Tulia Ackson amesema suala hilo halijatokea bungeni.

Bei ya unga sasa ni mara 12 ya mfuko wa Simenti

Bei ya unga sasa ni mara 12 ya mfuko wa Simenti WAKATI bei ya unga wa sembe ikipanda mpaka kufikia kuuzwa kati ya Sh. 2,200 na Sh. 2,500 kwa kilo, ile ya mfuko wa saruji wenye uzito wa kilo 50 imeshuka hadi sh. 9,000, sawa na Sh. 180 kwa kilo. Katika masoko na maduka mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam ambayo Nipashe ilitembelea jana, bei ya sembe ilikuwa ikiuzwa kwa kiasi hicho kwa rejareja huku wauzaji wa jumla wakiuza kiroba cha kilo 50 kwa kati ya sh.100,000 na sh.98,000. Ibrahim Omary, mfanyabiashara wa Kariakoo alisema anauza unga wa sembe kwa Sh. 2,400 kwa kuwa hununua kwa bei kubwa kutoka kwa wazalishaji. Alisema kampuni inayojulikana kwa jina la Mkulima huwauzia unga huo kwa Sh. 98,000 na Mama Neema huwauzia kwa sh. 100,000 kwa kiroba cha kilo 50. Kwenye baadhi ya maduka ya kula ya Kinondoni, unga umekuwa ukiuzwa kati ya Sh. 2,200 na Sh. 2,500. Tandika bei ya wastani ni Sh. 2,200, Mwenge Sh. 2,400, Kimara sh. 2,500 na Yombo Vituka sh. 2,200. ...

Jinsi ya kutengeneza SABUNI ya kipande YA KUGANDISHA

Jinsi ya kutengeneza SABUNI ya kipande YA KUGANDISHA Utengenezaji wa sabuni hii una njia nyingi Hatua  ya kwanza Chemsha vipimo 7 vya mafuta ya mawese au mafuta ya shea hadi ifikie hatua ya kimiminika chuja na yaweke kwenye chungu cha mfinyanzi au chombo cha plastiki. Hatua ya pili Pima vipimo 5 vya maji baridi kwenye chombo cha plastiki ongeza kipimo 1cha sodium hydroxide kwa uangalifu mkubwa kwenye maji acha hadi mchanganyiko huo uyeyuke. Subiri mchanganyiko wa sodium hydroxide na mafuta ukaribie kupoa. Hatua ya tatu Taratibu ongeza mchanganyiko wa sodium hydroxide kwenye mawese,huku ukikoroga haraka haraka bila kusitisha ukitumia ubao .hii ni njia nzuri zaidi. Njia ya pili Chemsha mafuta kwenye joto la kadiri ya 55C Changanya maji na sodium hydroxide na uache mchanganyiko huu upoe hadi kufikia joto hilohilo. Baada ya kuandaa mchanyiko wako changanya vimiminika hivyo viwili huku ukikoroga kwanguvu sana kadiri uwezavyo, taratibu sabuni itageuka kuwa laini. Kabla...