Skip to main content

Sembe yazidi kupaa Zanzibar

Sembe yazidi kupaa Zanzibar

MFUMKO wa bei za bidhaa Zanzibar umeongezeka kwa mwezi wa Aprili ikilinganishwa na mwezi wa Machi mwaka huu, unga wa sembe ukiongoza.

Akitoa ripoti ya hali ya mfumuko wa bei visiwani humo, Ofisa wa Mtakwimu Mkuu, Khamis Msham, alisema mfumko wa bei kwa mwezi Aprili umepanda kwa asilimiia 7.1 na mwezi Machi ulikuwa asilimia 6.4.

Alisema bei ya unga wa sembe imepanda kwa asilimia 6.7 kwa mwezi Aprili kwa kilo moja kuuzwa kwa Sh. 2000 kwa mwezi Machi Sh. 1,800.

Alisema pia bei ya ndizi mbichi imeongezeka kutoka asilimia 7.2 mwezi wa Machi hadi kufikia asilimia 7.2 kwa mwezi wa Aprili wakati ndizi mbivu imepanda kwa asilimia 19.1 .

Bidhaa zingine zilizopanda bei ni vinywaji visivyo na kilevi ambavyo kwa mwezi April ilikuwa asilimia 2.9 kwa mwezi mchele wa Mbeya umepanda kwa asilimia 2.6 na sukari 27.1,

Hata hivyo matarajio ya kuongzeka zaidi kwa mfumko wa bei wa bidhaa mbalimbali unatarajiwa kuwa mkubwa kwa mwezi wa Mei wakati waumini wa dini ya Kiislamu wakitarajia kufunga mfungo wa mwezi Ramadhani, mwishoni mwa mwezi huu.

Ofisa Mwandamizi wa Uchumi wa Benki Kuu (BOT), Moto Ngwinganele Lubogi, alisema msukumo wa mfumko wa bei za bidhaa hasa vyakula umesababishwa na uzalishaji mdogo kwa wakulima.

Alisema bei ya unga wa sembe imepanda kutokana na uzalishaji wa mahindi kupungua Tanzania bara, kutokana na maeneo kuchelewa kupata mvua.
Alisema wafanyabiashara wamekuwa wakipandisha bei za bidhaa kutokana na kiwango alichonunua kutoka kwa mkulima.

Hata hivyo, alisema kuwa ili mfumko wa bei za bidhaa hasa chakula uweze kushuka, wananchi wanatakiwa kuongeza uzalishaji wa kilimo na kuacha kulima kilimo cha mazoea cha kutegemea mvua.

Popular posts from this blog

Lema ahoji kushikiliwa mmiliki wa shule ya Lucky Vincent

Lema ahoji kushikiliwa mmiliki wa shule ya Lucky Vincent Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema   Dodoma. Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema amehoji sababu za polisi kumshikilia mmiliki wa shule ya Lucky Vincent badala ya trafiki waliokuwa barabarani siku ya ajali iliyoua watu 35. Akiomba mwongozo wa Spika kuhusu jambo hilo leo, amesema katika eneo husika kuna vizuizi vya ukaguzi vinne lakini trafiki hawakuona kuwa basi hilo lilikuwa kimezidisha watoto na hawakuwa wamefunga mikanda. Amesema badala ya trafiki hao kuchukuliwa hatua, anakamatwa mmiliki ambaye hakuwapo. Akijibu mwongozo huo, Naibu Spika, Dk Tulia Ackson amesema suala hilo halijatokea bungeni.

Bei ya unga sasa ni mara 12 ya mfuko wa Simenti

Bei ya unga sasa ni mara 12 ya mfuko wa Simenti WAKATI bei ya unga wa sembe ikipanda mpaka kufikia kuuzwa kati ya Sh. 2,200 na Sh. 2,500 kwa kilo, ile ya mfuko wa saruji wenye uzito wa kilo 50 imeshuka hadi sh. 9,000, sawa na Sh. 180 kwa kilo. Katika masoko na maduka mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam ambayo Nipashe ilitembelea jana, bei ya sembe ilikuwa ikiuzwa kwa kiasi hicho kwa rejareja huku wauzaji wa jumla wakiuza kiroba cha kilo 50 kwa kati ya sh.100,000 na sh.98,000. Ibrahim Omary, mfanyabiashara wa Kariakoo alisema anauza unga wa sembe kwa Sh. 2,400 kwa kuwa hununua kwa bei kubwa kutoka kwa wazalishaji. Alisema kampuni inayojulikana kwa jina la Mkulima huwauzia unga huo kwa Sh. 98,000 na Mama Neema huwauzia kwa sh. 100,000 kwa kiroba cha kilo 50. Kwenye baadhi ya maduka ya kula ya Kinondoni, unga umekuwa ukiuzwa kati ya Sh. 2,200 na Sh. 2,500. Tandika bei ya wastani ni Sh. 2,200, Mwenge Sh. 2,400, Kimara sh. 2,500 na Yombo Vituka sh. 2,200. ...

Jinsi ya kutengeneza SABUNI ya kipande YA KUGANDISHA

Jinsi ya kutengeneza SABUNI ya kipande YA KUGANDISHA Utengenezaji wa sabuni hii una njia nyingi Hatua  ya kwanza Chemsha vipimo 7 vya mafuta ya mawese au mafuta ya shea hadi ifikie hatua ya kimiminika chuja na yaweke kwenye chungu cha mfinyanzi au chombo cha plastiki. Hatua ya pili Pima vipimo 5 vya maji baridi kwenye chombo cha plastiki ongeza kipimo 1cha sodium hydroxide kwa uangalifu mkubwa kwenye maji acha hadi mchanganyiko huo uyeyuke. Subiri mchanganyiko wa sodium hydroxide na mafuta ukaribie kupoa. Hatua ya tatu Taratibu ongeza mchanganyiko wa sodium hydroxide kwenye mawese,huku ukikoroga haraka haraka bila kusitisha ukitumia ubao .hii ni njia nzuri zaidi. Njia ya pili Chemsha mafuta kwenye joto la kadiri ya 55C Changanya maji na sodium hydroxide na uache mchanganyiko huu upoe hadi kufikia joto hilohilo. Baada ya kuandaa mchanyiko wako changanya vimiminika hivyo viwili huku ukikoroga kwanguvu sana kadiri uwezavyo, taratibu sabuni itageuka kuwa laini. Kabla...