Skip to main content

Makamba ataka NEMC kutathmini Ngaresero Lodge

Makamba ataka NEMC kutathmini Ngaresero Lodge


WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Mazingira na Muungano, January Makamba ameagiza Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Kanda ya Kaskazini kufanya tathmini ya mazingira katika Hoteli ya Ngaresero Lodge.

Aidha, mmiliki wa hoteli hiyo amepewa siku 10 kufanyiwa tathimini ya mazingira ili kudhibiti matumizi ya maji kwa mwekezaji huyo pamoja na vijiji vinavyozunguka eneo hilo.
Makamba alitoa agizo hilo jijini hapa alipokuwa kwenye ziara ya kujionea hali halisi ya mazingira pamoja na athari zake katika mikoa mbalimbali.
Alisema mmiliki wa hoteli hiyo ana kibali cha mazingira cha awali na hivi sasa sheria hiyo imebadilishwa hivyo anapaswa kujua kuwa sheria zimebadilika na anapaswa kutumia watu sahihi wanaojua mazingira na kufanyiwa tathimini ya mara kwa mara.
“Tumeona uwekezaji ulioufanya lakini hapa kuna dosari kwa nini hujafanyiwa tathimini ya kimazingira, lakini pia ni lazima ujue kibali kinatolewa kama umekidhi viwango vya utunzaji wa mazingira pia haya maji ugawe vijijini muandae utaratibu wa mgawo wa maji na si kuyadhibiti kwako tu,” alisema.
Mmoja kati ya wamiliki wa hoteli hiyo, Tim Litch alikiri kuwapo uzembe katika tathimini ya kimazingira katika eneo hilo na kuomba mamlaka husika kushirikiana naye ili kurekebisha kasoro hizo kwani eneo hilo analitumia kwa ajili ya utalii, kufuga samaki pamoja na kuhakikisha mazingira yakuwa safi.

Popular posts from this blog

Lema ahoji kushikiliwa mmiliki wa shule ya Lucky Vincent

Lema ahoji kushikiliwa mmiliki wa shule ya Lucky Vincent Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema   Dodoma. Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema amehoji sababu za polisi kumshikilia mmiliki wa shule ya Lucky Vincent badala ya trafiki waliokuwa barabarani siku ya ajali iliyoua watu 35. Akiomba mwongozo wa Spika kuhusu jambo hilo leo, amesema katika eneo husika kuna vizuizi vya ukaguzi vinne lakini trafiki hawakuona kuwa basi hilo lilikuwa kimezidisha watoto na hawakuwa wamefunga mikanda. Amesema badala ya trafiki hao kuchukuliwa hatua, anakamatwa mmiliki ambaye hakuwapo. Akijibu mwongozo huo, Naibu Spika, Dk Tulia Ackson amesema suala hilo halijatokea bungeni.

Bei ya unga sasa ni mara 12 ya mfuko wa Simenti

Bei ya unga sasa ni mara 12 ya mfuko wa Simenti WAKATI bei ya unga wa sembe ikipanda mpaka kufikia kuuzwa kati ya Sh. 2,200 na Sh. 2,500 kwa kilo, ile ya mfuko wa saruji wenye uzito wa kilo 50 imeshuka hadi sh. 9,000, sawa na Sh. 180 kwa kilo. Katika masoko na maduka mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam ambayo Nipashe ilitembelea jana, bei ya sembe ilikuwa ikiuzwa kwa kiasi hicho kwa rejareja huku wauzaji wa jumla wakiuza kiroba cha kilo 50 kwa kati ya sh.100,000 na sh.98,000. Ibrahim Omary, mfanyabiashara wa Kariakoo alisema anauza unga wa sembe kwa Sh. 2,400 kwa kuwa hununua kwa bei kubwa kutoka kwa wazalishaji. Alisema kampuni inayojulikana kwa jina la Mkulima huwauzia unga huo kwa Sh. 98,000 na Mama Neema huwauzia kwa sh. 100,000 kwa kiroba cha kilo 50. Kwenye baadhi ya maduka ya kula ya Kinondoni, unga umekuwa ukiuzwa kati ya Sh. 2,200 na Sh. 2,500. Tandika bei ya wastani ni Sh. 2,200, Mwenge Sh. 2,400, Kimara sh. 2,500 na Yombo Vituka sh. 2,200. ...

Jinsi ya kutengeneza SABUNI ya kipande YA KUGANDISHA

Jinsi ya kutengeneza SABUNI ya kipande YA KUGANDISHA Utengenezaji wa sabuni hii una njia nyingi Hatua  ya kwanza Chemsha vipimo 7 vya mafuta ya mawese au mafuta ya shea hadi ifikie hatua ya kimiminika chuja na yaweke kwenye chungu cha mfinyanzi au chombo cha plastiki. Hatua ya pili Pima vipimo 5 vya maji baridi kwenye chombo cha plastiki ongeza kipimo 1cha sodium hydroxide kwa uangalifu mkubwa kwenye maji acha hadi mchanganyiko huo uyeyuke. Subiri mchanganyiko wa sodium hydroxide na mafuta ukaribie kupoa. Hatua ya tatu Taratibu ongeza mchanganyiko wa sodium hydroxide kwenye mawese,huku ukikoroga haraka haraka bila kusitisha ukitumia ubao .hii ni njia nzuri zaidi. Njia ya pili Chemsha mafuta kwenye joto la kadiri ya 55C Changanya maji na sodium hydroxide na uache mchanganyiko huu upoe hadi kufikia joto hilohilo. Baada ya kuandaa mchanyiko wako changanya vimiminika hivyo viwili huku ukikoroga kwanguvu sana kadiri uwezavyo, taratibu sabuni itageuka kuwa laini. Kabla...